< Matendo 13 >

1 Katika kanisa la Antiokia kulikuwa na watu wengine waliokuwa manabii na walimu; miongoni mwao akiwa Barnaba, Simoni aitwaye pia Mweusi, Lukio wa Kurene, Manaeni ambaye alikuwa amelelewa pamoja na mfalme Herode, na Saulo.
Now there were in the church in Antioch prophets and teachers; Barnabas and Symeon, surnamed "the Black," Lucius of Cyrene, Manaen, the foster-brother of Herod the Tetrarch, and Saul.
2 Walipokuwa wanafanya ibada yao kwa Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu alisema: “Niteulieni Barnaba na Saulo kwa ajili ya kazi niliyowaitia.”
And as they were worshiping the Lord, and fasting, the Holy Spirit said to them, "Separate me Barnabas and Saul for the work to which I have called them."
3 Basi, baada ya kusali na kufunga zaidi, wakawawekea mikono, wakawaacha waende zao.
So after fasting and praying, they laid their hands on them, and let them go.
4 Basi, Barnaba na Saulo walipokwisha tumwa na Roho Mtakatifu, walishuka hadi Seleukia, na kutoka huko walipanda meli hadi kisiwa cha Kupro.
So they, sent forth by the Holy Spirit, went down to Seleucia, and from thence they sailed to Cyprus.
5 Walipofika Salami walihubiri neno la Mungu katika masunagogi ya Kiyahudi. Yohane (Marko) alikuwa msaidizi wao.
And while they were in Salamis, they proclaimed the word of God in the synagogues of the Jews.
6 Walitembea toka upande mmoja wa kisiwa mpaka Pafo upande wa pili, na huko walimkuta mchawi mmoja Myahudi aitwaye Baryesu ambaye alijisingizia kuwa nabii.
They had John Mark as an assistant; and after going through the whole island as far as Paphos, they found a certain Jewish sorcerer and false prophet, named Bar-Jesus,
7 Huyu alikuwa pamoja na Sergio Paulo, mkuu wa kile kisiwa, ambaye alikuwa mtu mwelewa sana. Sergio Paulo aliwaita Barnaba na Saulo ili asikie neno la Mungu.
who belonged to the suite of the proconsul, Sergius Paulus, an intelligent man. He summoned Barnabas and Saul, and sought to hear the word of God.
8 Lakini huyo mchawi Elima (kama alivyokuwa anaitwa kwa Kigiriki), alijaribu kuwapinga ili kumzuia huyo mkuu wa kisiwa asije akaigeukia imani ya Kikristo.
But Elymas, "the sorcerer," for that is the translation of his name, opposed them, and tried to divert the proconsul from the faith.
9 Basi, Saulo ambaye aliitwa pia Paulo, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alimkodolea macho huyo mchawi,
So Saul, who is also called Paul, filled with the Holy Spirit, gazed steadily at him, and said.
10 akasema, “Mdanganyifu wa kupindukia na mlaghai wewe! Wewe ni mtoto wa Ibilisi! Wewe ni adui wa chochote kile kilicho cha kweli; hukomi hata mara moja kujaribu kuzipotosha njia za Bwana zilizonyoka.
"O full of all craft and cunning, you son of the devil! You enemy of all goodness! Will you never stop perverting the right ways of the Lord?
11 Sasa, mkono wa Bwana utakuadhibu: utakuwa kipofu na hutaweza kuuona mwanga wa jua kwa kitambo.” Mara kila kitu kikawa kama ukungu na giza kwake, akaanza kwenda huku na huku akitafuta mtu wa kumshika mkono amwongoze.
"The Lord’s hand is now upon you, and you shall be blind, not seeing the sun for a season." Instantly there fell on him a mist and a darkness, and groping about, he sought some one to lead him by the hand.
12 Yule mkuu wa kisiwa alipoona hayo, aliongoka akawa muumini; akastaajabia sana mafundisho aliyosikia juu ya Bwana.
Then the proconsul, seeing what had happened, believed. He was astounded at the teaching of the Lord.
13 Kutoka Pafo, Paulo na wenzake walipanda meli wakaenda hadi Perga katika Pamfulia; lakini Yohane (Marko) aliwaacha, akarudi Yerusalemu.
From Paphos Paul and his party set sail for Perga in Pamphylia; but John Mark left them and went back to Jerusalem.
14 Lakini wao waliendelea na safari toka Pisga hadi mjini Antiokia Pisidia. Siku ya Sabato waliingia ndani ya Sunagogi, wakakaa.
Then they themselves, passing through from Perga, came to Antioch in Pisidia. Here they went into the synagogue on the Sabbath Day and sat down.
15 Baada ya masomo katika kitabu cha Sheria ya Mose na katika maandiko ya manabii, wakuu wa lile sunagogi waliwapelekea ujumbe huu: “Ndugu, kama mnalo jambo la kuwaambia watu ili kuwapa moyo, semeni.”
And, after the reading of the Law and the Prophets, the wardens of the synagogue sent word to them. "Brothers," they said, "if you have any word of encouragement to the people, say it."
16 Basi, Paulo alisimama, akatoa ishara kwa mkono, akaanza kuongea: “Wananchi wa Israeli na wengine wote mnaomcha Mungu, sikilizeni!
So Paul stood up, and motioning with his hand, said. "Men of Israel, and you who fear God, listen.
17 Mungu wa taifa hili la Israeli aliwateua babu zetu na kuwafanya wawe taifa kubwa walipokuwa ugenini kule Misri. Mungu aliwatoa huko kwa uwezo wake mkuu.
"The God of this people of Israel chose our forefathers and made this people great, while they sojourned in the land of Egypt. And with an uplifted arm he led them out of it.
18 Aliwavumilia kwa muda wa miaka arobaini kule jangwani.
"For about forty years he bore with them in the desert,
19 Aliyaangamiza mataifa ya nchi ya Kanaani akawapa hao watu wake ile nchi kuwa mali yao.
"and when he had destroyed seven nations in the land of Canaan, he gave them their land as an inheritance for about four hundred and fifty years.
20 Miaka mia nne na hamsini ilipita, halafu akawapatia waamuzi wawaongoze mpaka wakati wa nabii Samweli.
"And afterwards he gave them Judges, until Samuel, the prophet.
21 Hapo wakapendelea kuwa na mfalme, na Mungu akawapa Saulo, mtoto wa Kishi wa kabila la Benyamini, awe mfalme wao kwa muda wa miaka arobaini.
"Then they asked for a king, and he gave them Saul, the son of Kish, a Benjamite for forty years.
22 Baada ya kumwondoa Saulo, Mungu alimteua Daudi kuwa mfalme wao. Mungu alionyesha kibali chake kwake akisema: Nimemwona Daudi mtoto wa Yese; ni mtu anayepatana na moyo wangu; mtu ambaye atatimiza yale yote ninayotaka kuyatenda.
After deposing him, he raised up David to be their king, to whom he also bore witness, when he said, "I have found David, the son of Jesse, a man after my own heart, and who will obey all my will.
23 Kutokana na ukoo wake mtu huyu, Mungu, kama alivyoahidi, amewapelekea watu wa Israeli Mwokozi, ndiye Yesu.
"Of this man’s descendants God has brought unto Israel, according to his promise, a Savior, Jesus;
24 Kabla ya kuja kwake Yesu, Yohane alimtangulia akiwahubiria watu wote wa Israeli kwamba ni lazima watubu na kubatizwa.
"before whose coming John had already preached a baptism of repentance to all the people of Israel.
25 Yohane alipokuwa anamaliza ujumbe wake aliwaambia watu: Mnadhani mimi ni nani? Mimi si yule mnayemtazamia. Huyo anakuja baada yangu na mimi sistahili hata kuzifungua kamba za viatu vyake.
"And John, when he was finishing his race, repeatedly asked the people. "‘Who do you suppose that I am? I am not He. But behold there comes One after me, whose sandal I am not worthy to unfasten.’
26 “Ndugu, ninyi mlio watoto wa ukoo wa Abrahamu, na wengine wote mnaomcha Mungu! Ujumbe huu wa wokovu umeletwa kwetu.
"Brothers, sons of Abraham’s race, and all among you who reverence God, to us has the word of this salvation been sent.
27 Kwa maana wenyeji wa Yerusalemu na wakuu wao hawakumtambua yeye kuwa Mwokozi. Wala hawakuelewa maneno ya manabii yanayosomwa kila Sabato. Hata hivyo, waliyafanya maneno ya manabii yatimie kwa kumhukumu Yesu adhabu ya kifo.
"For those who dwell in Jerusalem, and their rulers, because they knew him not, nor the utterances of the prophets which are read every Sabbath, fulfilled them by condemning him.
28 Ingawa hawakumpata na hatia inayostahili auawe, walimwomba Pilato amhukumu auawe.
"Though they found no cause of death in him, yet they asked Pilate to put him to death.
29 Na baada ya kutekeleza yote yaliyokuwa yameandikwa kumhusu yeye, walimshusha kutoka msalabani, wakamweka kaburini.
"And when they had fulfilled everything which had been written concerning him, they took him down from the tree and laid him in a tomb.
30 Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu.
"But God raised him from the dead.
31 Naye, kwa siku nyingi aliwatokea wale waliofuatana naye kutoka Galilaya mpaka Yerusalemu. Hao ndio walio sasa mashahidi wake kwa watu wa Israeli.
"For many days he was seen by those that came up with him from Galilee to Jerusalem, and are now his witnesses to the people.
32 Sisi tumekuja hapa kuwaleteeni Habari Njema: jambo lile Mungu alilowaahidia babu zetu amelitimiza sasa kwa ajili yetu sisi tulio wajukuu wao kwa kumfufua Yesu kutoka wafu.
"And we bring you glad tidings of the promise made to our forefathers,
33 Kama ilivyoandikwa katika zaburi ya pili: Wewe ni Mwanangu, mimi leo nimekuwa baba yako.
"how that God fulfilled it for us their children in raising up Jesus; as it is also written in the second Psalm, "Thou art my son, today have I become thy Father.
34 Na juu ya kumfufua kutoka wafu, asipate tena kurudi huko na kuoza, Mungu alisema hivi: Nitakupa baraka takatifu na za kweli nilizomwahidia Daudi.
"And as to his having raised him from among the dead, now no more to return to corruption, he has said this, "I will give thee the holy and sure blessings of David.
35 Naam, na katika sehemu nyingine za zaburi asema: Hutamwacha Mtakatifu wako aoze.
"Because in another psalm he says, "Thou wilt not give thy Holy One to see corruption.
36 Sasa, Daudi mwenyewe alitimiza mapenzi ya Mungu wakati wake; kisha akafa na kuzikwa karibu na wazee wake, na mwili wake ukaoza.
"For David, after he had served his own generation according to the will of God, fell on sleep, and was gathered to his forefathers, and did see corruption;
37 Lakini yule ambaye Mungu alimfufua kutoka wafu hakupata kuoza.
but he whom God raised up saw no corruption.
38 Jueni wazi, ndugu zangu, kwamba ujumbe kuhusu kusamehewa dhambi unahubiriwa kwenu kwa njia ya Yesu Kristo;
"Be it known unto you therefore, brothers, that remission of sins is proclaimed to you through this man;
39 na ya kwamba kila mmoja anayemwamini Yesu anasamehewa dhambi zote, jambo ambalo halingewezekana kwa njia ya Sheria ya Mose.
"and that by him every one that believes is justified from all things from which you could never be justified by the law of Moses.
40 Jihadharini basi, msije mkapatwa na yale yaliyosemwa na manabii:
"Beware, then, lest that spoken of in the prophets come upon you.
41 Sikilizeni enyi wenye madharau, shangaeni mpotee! Kwa maana kitu ninachofanya sasa, nyakati zenu, ni kitu ambacho hamtakiamini hata kama mtu akiwaelezeni.”
"Behold, ye despisers, and wonder, and perish, For in your days I will do a deed, A deed which you will never believe, Though one should declare it unto you."
42 Paulo na Barnaba walipokuwa wanatoka katika ile sunagogi, wale watu waliwaalika waje tena siku ya Sabato iliyofuata, waongee zaidi juu ya mambo hayo.
As Paul and Barnabas left the synagogue, the people earnestly begged that these words might be repeated to them on the following Sabbath.
43 Mkutano huo ulipomalizika, Wayahudi wengi na watu wa mataifa mengine waliokuwa wameongokea dini ya Kiyahudi waliwafuata Paulo na Barnaba. Hao mitume waliongea nao, wakawatia moyo waendelee kuishi wakitegemea neema ya Mungu.
When the congregation broke up, many of the Jews, and of the devout proselytes, followed Paul and Barnabas, who talked to them, and urged them to continue in the grace of God.
44 Siku ya Sabato iliyofuata, karibu kila mtu katika ule mji alikuja kusikiliza neno la Bwana.
On the next Sabbath almost the entire city was gathered together to know the word of God.
45 Lakini Wayahudi walipoliona hilo kundi la watu walijaa wivu, wakapinga alichokuwa anasema Paulo na kumtukana.
When they saw the crowds, the Jews were filled with jealousy, and began to contradict Paul’s statements, and to abuse him.
46 Hata hivyo, Paulo na Barnaba waliongea kwa uhodari zaidi, wakasema, “Ilikuwa ni lazima neno la Mungu liwafikieni ninyi kwanza; lakini kwa kuwa mmelikataa na kujiona hamstahili uzima wa milele, basi, tunawaacheni na kuwaendea watu wa mataifa mengine. (aiōnios g166)
So Paul and Barnabas spoke out boldly. "It was necessary," they said, "first to proclaim the word of God to you. But since you push it away from you, and judge yourselves unworthy of eternal life, lo, we turn to the Gentiles. (aiōnios g166)
47 Maana Bwana alituagiza hivi: Nimekuteua wewe uwe mwanga kwa mataifa, uwe njia ya wokovu kwa ulimwengu wote.”
"For such is God’s command to us, saying, "I have set thee for a light to the Gentiles, That thou shouldest be for salvation to the uttermost part of the earth."
48 Watu wa mataifa mengine waliposikia jambo hilo walifurahi, wakausifu ujumbe wa Mungu; na wale waliokuwa wamechaguliwa kupata uzima wa milele, wakawa waumini. (aiōnios g166)
When the Gentiles heard this, they were glad, and glorified the word of the Lord, and all who had been ordained to eternal life, believed. (aiōnios g166)
49 Neno la Bwana likaenea kila mahali katika sehemu ile.
So the Lord’s message went far and wide, through the whole district.
50 Lakini Wayahudi waliwachochea wanawake wa tabaka ya juu wa mataifa mengine ambao walikuwa wacha Mungu, na wanaume maarufu wa mji huo. Wakaanza kuwatesa Paulo na Barnaba, wakawafukuza kutoka katika eneo lao.
But the Jews urged on the devout women of high rank, and the leading citizens, and stirred up a persecution against Paul and Barnabas, and drove them out of the district,
51 Basi, mitume wakayakung'uta mavumbi yaliyokuwa katika miguu yao kama onyo, kisha wakaenda Ikonio.
But they shook off the dust of their feet against them, and came to Iconium.
52 Lakini hao wafuasi walikuwa wamejaa furaha na Roho Mtakatifu.
As for the disciples, they were continually filled with joy, and with the Holy Spirit.

< Matendo 13 >