< 3 Yohana 1 >
1 Mimi mzee nakuandikia wewe Gayo, rafiki yangu, ninayekupenda kweli.
L'ancien à Gaïus le bien-aimé, que j'aime véritablement.
2 Mpenzi wangu, nakutakia mafanikio mema ya kila aina; nakutakia afya njema ya mwili kama ulivyo nayo rohoni.
Bien-aimé, je souhaite que tu prospères en toutes choses, et que la santé de ton corps soit aussi bonne que celle de ton âme.
3 Nimefurahi sana ndugu kadhaa walipofika hapa, wakaiambia juu ya uaminifu wako kuhusu ukweli; naam, wewe unaishi daima katika ukweli.
En effet, j'ai éprouvé une grande joie en voyant arriver des frères qui ont rendu témoignage à ton attachement à la vérité, et à la manière dont tu marches dans cette vérité.
4 Hakuna kitu kinachonifurahisha zaidi kuliko kusikia kwamba watoto wangu wanaishi katika ukweli.
Je n'ai pas de plus grande joie que d'apprendre que mes enfants marchent dans la vérité.
5 Mpenzi wangu, wewe ni mwaminifu kila mara unapowahudumia ndugu, hata kama ni wageni.
Bien-aimé, tu agis fidèlement dans tout ce que tu fais pour les frères, et même pour des frères étrangers.
6 Ndugu hao wamelieleza kanisa hapa habari za upendo wako. Tafadhali uwasaidie waendelee na safari yao kwa namna itakayompendeza Mungu,
Ils ont rendu témoignage à ta charité en présence de l'Eglise. Tu feras bien de pourvoir à leur voyage d'une manière digne de Dieu;
7 Maana wanaanza safari yao katika utumishi wa Kristo bila kupokea msaada wowote kutoka kwa watu wasioamini.
car c'est pour le nom de Jésus-Christ qu'ils se sont mis en route, sans rien recevoir des Païens.
8 Basi, sisi tunapaswa kuwasaidia watu hawa, ili nasi tupate kushiriki katika kazi yao kwa ajili ya ukweli.
Aussi devons-nous accueillir de tels hommes, afin que nous travaillions avec eux pour la vérité.
9 Niliandika barua fupi kwa hilo kanisa; lakini Diotrefe, ambaye hupenda kuwa kiongozi wao, hataki kabisa kunisikiliza.
J'ai écrit quelques mots à l'Église; mais Diotrèphe, qui aime à y tenir le premier rang, ne veut pas nous recevoir.
10 Basi, nitakapokuja nitayafichua mambo yote anayofanya, maneno mabaya anayotutolea na uongo anaosema juu yetu. Isitoshe, yeye hukataa kuwakaribisha hao ndugu walio safarini, na hata huwazuia watu wengine wanaotaka kuwakaribisha, na hujaribu kuwafukuzia nje ya kanisa.
C'est pourquoi, si je viens, je signalerai le mal qu'il fait, en tenant contre nous de méchants propos. Non content de cela, il ne reçoit pas les frères; et ceux qui voudraient le faire, il les en empêche et les chasse de l'Église.
11 Mpenzi wangu, usifuate mfano mbaya, bali mfano mwema. Kila atendaye mema ni wa Mungu; lakini anayetenda mabaya hajapata kumwona Mungu.
Bien-aimé, n'imite pas le mal, mais imite le bien. Celui qui fait le bien, est de Dieu; celui qui fait le mal, n'a point vu Dieu.
12 Kila mtu anamsifu Demetrio; naam, ukweli wenyewe unamsifu. Nasi pia tunatoa ushahidi wetu juu yake, nawe wajua kwamba tunachosema ni kweli.
Tous rendent un bon témoignage à Démétrius, et la vérité elle-même le lui rend; nous y joignons notre propre témoignage, et tu sais qu'il est conforme à la vérité.
13 Ninayo bado mengi ya kukwambia, lakini sipendi kuyaandika kwa kalamu na wino.
J'aurais bien des choses à te dire; mais je ne veux pas le faire avec l'encre et la plume.
14 Natumaini kukuona karibuni na hapo tutazungumza ana kwa ana. Nakutakia amani. Rafiki zako wanakusalimu. Wasalimu rafiki zetu wote kila mmoja binafsi.
J'espère te voir bientôt, et nous nous entretiendrons de vive voix. Que la paix soit avec toi! Les amis te saluent. Salue les amis, chacun en particulier.