< 2 Timotheo 2 >

1 Basi, wewe mwanangu, uwe na nguvu katika neema tunayopata katika kuungana na Kristo Yesu.
Therefore, my child, be thou filled up with dynamite in the grace which is in Christ Jesus,
2 Chukua yale mafundisho uliyonisikia nikitangaza mbele ya mashahidi wengi, uyakabidhi kwa watu wanaoaminika, ambao wataweza kuwafundisha wengine pia.
and whatsoever things thou hast heard with me through many witnesses, commit thou the same to faithful men, who will be able also to teach others.
3 Shiriki katika mateso kama askari mwaminifu wa Kristo yesu.
Suffer affliction, as a good soldier of Jesus Christ.
4 Mwanajeshi vitani hujiepusha na shughuli za maisha ya kawaida ili aweze kumpendeza mkuu wa jeshi.
No one operating as a soldier is entangled with the affairs of life; in order that he may please his commander.
5 Mwanariadha yeyote hawezi kushinda na kupata zawadi ya ushindi kama asipozitii sheria za michezo.
But if indeed any one may fight, he is not crowned unless he may fight lawfully.
6 Mkulima ambaye amefanya kazi ngumu anastahili kupata sehemu ya kwanza ya mavuno.
It behooves the toiling farmer first to partake of the fruits.
7 Fikiria hayo ninayosema, kwani Bwana atakuwezesha uyaelewe yote.
Know what I say; for the Lord will give you understanding in all things.
8 Mkumbuke Yesu Kristo aliyefufuliwa kutoka wafu, aliyekuwa wa ukoo wa Daudi, kama isemavyo Habari Njema ninayoihubiri.
Remember Jesus Christ, who is risen from the dead, from the seed of David, according to my gospel:
9 Kwa sababu ya kuihubiri Habari Njema mimi nateseka na nimefungwa minyororo kama mhalifu. Lakini neno la Mungu haliwezi kufungwa minyororo,
in whom I suffer affliction as an evil-doer, even unto bonds; but the word of God is not bound.
10 na hivyo navumilia kila kitu kwa ajili ya wateule wa Mungu, ili wao pia wapate ukombozi upatikanao kwa njia ya Yesu Kristo, na ambao huleta utukufu wa milele. (aiōnios g166)
On account of this I endure all things for the sake of the elect, in order that they may also have the salvation which is in Christ Jesus with eternal glory. (aiōnios g166)
11 Usemi huu ni wa kweli: “Ikiwa tulikufa pamoja naye, tutaishi pia pamoja naye.
It is a faithful saying: For if we die along with him, we will also live with him:
12 Tukiendelea kuvumilia, tutatawala pia pamoja naye. Tukimkana, naye pia atatukana.
if we endure, we will truly reign with him: if we shall deny him, he will also deny us:
13 Tukikosa kuwa waaminifu, yeye hubaki mwaminifu daima, maana yeye hawezi kujikana mwenyewe.”
if we are unfaithful, he remains faithful; for he is not able to deny himself.
14 Basi, wakumbushe watu wako mambo haya, na kuwaonya mbele ya Mungu waache ubishi juu ya maneno. Ubishi huo haufai, ila huleta tu uharibifu mkuu kwa wale wanaousikia.
Remember these things, testifying before God, that they shall not fight with words, profitable unto nothing, for the overturning of those who hear.
15 Jitahidi kupata kibali kamili mbele ya Mungu kama mfanyakazi ambaye haoni haya juu ya kazi yake, na ambaye hufundisha sawa ule ujumbe wa kweli.
Study to present yourself to God approved, a workman not to be ashamed, rightly dividing the word of truth.
16 Jiepushe na majadiliano ya kidunia na ya kipumbavu; kwani hayo huzidi kuwatenga watu mbali na Mungu.
But reject the unsanctified empty talks: for they will proceed unto more of ungodliness,
17 Mafundisho ya aina hiyo ni kama donda linalokula mwili. Miongoni mwa hao waliofundisha hayo ni Humenayo na Fileto.
and their word like gangrene will have eating. Of whom are Hymenaeus and Phyletus;
18 Hawa wamepotoka kabisa mbali na ukweli, na wanatia imani ya watu wengine katika wasiwasi kwa kusema ati ufufuo wetu umekwisha fanyika.
who have made shipwreck concerning the truth, saying that the resurrection has already come, and they overturn the faith of some.
19 Lakini msingi thabiti uliowekwa na Mungu uko imara, na juu yake yameandikwa maneno haya: “Bwana anawafahamu wale walio wake,” na “Kila asemaye yeye ni wa Bwana, ni lazima aachane na uovu.”
The foundation of God stands solid indeed, having this seal, The Lord knows them that are his: and; Let every one naming the name of the Lord depart from iniquity.
20 Katika nyumba kubwa kuna mabakuli na vyombo vya kila namna: vingine ni vya fedha na dhahabu, vingine vya mbao na udongo, vingine ni vya matumizi ya pekee na vingine kwa ajili ya matumizi ya kawaida.
But in a great house there are not only gold and silver vessels, but also wood and stone, the former truly indeed unto honor, but the latter unto dishonor.
21 Basi, kama mtu atajitakasa kwa kujitenga mbali na mambo hayo yote maovu, atakuwa chombo cha matumizi ya pekee, kwa sababu amewekwa wakfu, anamfaa Bwana wake na yupo tayari kwa kila kazi njema.
Therefore if any one may cleanse himself from these, he shall be a vessel unto honor, having been sanctified, well pleasing to the Lord, having been prepared unto every good work.
22 Jiepushe na tamaa za ujana, fuata uadilifu, imani, upendo, amani, pamoja na watu wote ambao wanamwomba Bwana kwa moyo safi.
But fly from youthful lusts, and pursue righteousness, faith, divine love, peace, with those who call upon the Lord out of a clean heart.
23 Epuka ubishi wa kijinga na kipumbavu; wajua kwamba hayo huleta magomvi.
But reject foolish and undisciplinary questions, knowing that they gender strife.
24 Mtumishi wa Bwana asigombane. Anapaswa kuwa mpole kwa watu wote, mwalimu mwema na mvumilivu,
But it does not behoove the servant of the Lord to strive, but to be gentle toward all, competent to teach, enduring evil,
25 ambaye ni mpole anapowaonya wapinzani wake, kwani huenda Mungu akawajalia nafasi ya kutubu, wakapata kuujua ukweli.
in meekness correcting the adversaries; if peradventure God may grant unto them repentance into the perfect knowledge of the truth,
26 Hapo fahamu zao zitawarudia tena, wakaponyoka katika mtego wa Ibilisi aliyewanasa na kuwafanya wayatii matakwa yake.
and they may escape from the snare of the devil, having been taken captive by him (the Lord's servant) according to his will.

< 2 Timotheo 2 >