< 2 Timotheo 1 >

1 Mimi Paulo, ambaye Mungu alitaka niwe mtume wa Kristo Yesu ili niutangaze ule uzima tulioahidiwa katika kuungana na Kristo Yesu,
Paul, an apostle of Jesus Christ through the will of God, according to the commandment of life which is in Christ Jesus,
2 nakuandikia wewe mwanangu mpenzi Timotheo. Nakutakia neema, huruma na amani kutoka kwa Mungu Baba na Kristo Yesu Bwana wetu.
to Timothy, my beloved child. Grace, mercy, peace from God our Father and Jesus Christ our Lord.
3 Ninamshukuru Mungu ambaye ninamtumikia kwa dhamiri safi kama walivyofanya wazee wangu; namshukuru kila ninapokukumbuka daima katika sala zangu.
I give thanks to God, whom I serve from my ancestors with a clean conscience, as I have incessant mention of you in my prayers, night and day
4 Nakumbuka machozi yako na ninatamani usiku na mchana kukuona, ili nijazwe furaha.
longing to see you, remembering your tears, in order that I may be filled with joy;
5 Naikumbuka imani yako ya kweli, imani aliyokuwa nayo nyanya yako Loisi, na pia mama yako Eunike. Nina hakika kwamba wewe pia unayo.
having received the remembrance of the unhypocritical faith which is in you; which dwelt first in your grandmother Lois, and your mother Eunice; and, I am persuaded that it is in you also.
6 Ndio maana nakukumbusha ukiweke motomoto kile kipaji ulichopewa na Mungu wakati nilipokuwekea mikono yangu.
On account of which cause I remind you to revive and refire the gift of God which is in you by the laying on of my hands.
7 Kwa maana Mungu hakutupa Roho wa kutufanya tuwe waoga, bali alitupa Roho wa kutujalia nguvu, upendo na nidhamu.
For God has not given us the spirit of cowardice; but of power and divine love and prudence.
8 Basi, usione haya kumshuhudia Bwana wetu, wala usione haya kwa sababu yangu mimi niliye mfungwa kwa ajili yake. Lakini shiriki katika mateso kwa ajili ya Habari Njema, kadiri ya nguvu unazopewa na Mungu.
Therefore do not be ashamed of the testimony of our Lord, nor me his prisoner: but suffer affliction for the sake of the gospel according to the power of God;
9 Yeye alituokoa, akatuita tuwe watu wake yeye mwenyewe, si kwa sababu ya matendo yetu wenyewe bali kwa sababu ya kusudi lake na neema yake. Alitujalia neema hiyo katika Kristo Yesu kabla mwanzo wa nyakati; (aiōnios g166)
the one having saved us, and called us with a holy calling, not according to our works, but according to his own purpose and grace, which was given to us in Christ Jesus before the eternal times, (aiōnios g166)
10 lakini sasa imefunuliwa kwetu kwa kuja kwake Mwokozi wetu Yesu Kristo. Yeye amekomesha nguvu za kifo, na kwa njia ya Habari Njema akadhihirisha uzima usio kufa.
but now having been made manifest through the appearing of Jesus Christ our Saviour, the one having indeed destroyed death, and lighted up life and immortality through the gospel,
11 Mungu amenichagua mimi niwe mtume na mwalimu kwa ajili ya kuhubiri Habari Njema,
unto which I have been placed a herald, and an apostle, and teacher:
12 nami nateseka mambo haya kwa sababu hiyo. Lakini niko bado timamu kabisa kwani namjua yule niliyemwamini, tena nina hakika kwamba yeye aweza kukilinda salama kile alichonikabidhi, mpaka Siku ile.
on account of which cause I indeed suffer these things: but I am not ashamed; for I know whom I have believed, and am persuaded that he is able to stand guard over that which is committed unto me unto that day.
13 Shika kwa makini mafundisho yale ya kweli niliyokufundisha, na kubaki katika hiyo imani na huo upendo wetu katika kuungana na Kristo Yesu.
Hold fast the form of sound words which you heard with me, in the faith and divine love which is in Christ Jesus:
14 Jambo lile bora ulilokabidhiwa lilinde kwa nguvu ya Roho Mtakatifu anayeishi ndani yetu.
stand guard over the beautiful deposit through the Holy Ghost who dwells in us.
15 Kama unavyojua, watu wote mkoani Asia wameniacha, miongoni mwao wakiwa Fugelo na Hermogene.
You know this, that all who are in Asia, of whom are Phygelus and Hermogenes have turned away from me.
16 Bwana aihurumie jamaa ya Onesiforo, kwa sababu aliniburudisha rohoni mara nyingi, wala hakuona haya kwa kuwa nilikuwa kifungoni,
May the Lord grant mercy to the family of Onesiphorus, because frequently he refreshed me, and was not ashamed of my chain,
17 ila mara tu alipofika Roma, alianza kunitafuta kwa bidii mpaka akanipata.
and, being in Rome, he diligently sought me, and found me.
18 Bwana amjalie huruma katika Siku ile! Nawe wajua vizuri mengi aliyonifanyia huko Efeso.
May the Lord grant unto him to find mercy with the Lord in that day. And so many things as he ministered in Ephesus, you know better.

< 2 Timotheo 1 >