< 2 Wathesalonike 3 >
1 Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili ujumbe wa Bwana uzidi kuenea upesi na kupokelewa kwa heshima kama vile ulivyo kati yenu.
Finally, brothers, pray for us, that the word of the Lord may spread rapidly and be glorified, even as also with you;
2 Ombeni pia ili Mungu atuokoe na watu wapotovu na waovu, maana si wote wanaoamini ujumbe huu.
and that we may be delivered from unreasonable and evil people; for not all have faith.
3 Lakini Bwana ni mwaminifu. Yeye atawaimarisheni na kuwalinda salama na yule Mwovu.
But the Lord is faithful, who will establish you, and guard you from the evil one.
4 Naye Bwana anatupatia tumaini kubwa juu yenu, na hatuna shaka kwamba mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaambieni.
We have confidence in the Lord concerning you, that you both do and will do the things we command.
5 Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika uvumilivu tunaopewa na Kristo.
May the Lord direct your hearts into the love of God, and into the patience of Christ.
6 Ndugu, tunawaamuru kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, mjiepushe na ndugu wote walio wavivu na ambao hawafuati maagizo tuliyowapa.
Now we command you, brothers, in the name of our Lord Jesus Christ, that you withdraw yourselves from every brother who lives an undisciplined life, and not after the tradition which they received from us.
7 Ninyi wenyewe mnajua kwamba mnapaswa kufuata mfano wetu. Sisi tulipokuwa nanyi hatukuwa wavivu;
For you know how you ought to imitate us. For we were not undisciplined among you,
8 hatukula chakula kwa mtu yeyote bila ya kumlipa. Tulifanya kazi kwa bidii na taabu mchana na usiku ili tusiwe mzigo kwa mtu yeyote kati yenu.
neither did we eat bread from anyone's hand without paying for it, but in labor and travail worked night and day, that we might not burden any of you;
9 Tulifanya hivyo si kwa kuwa hatuna haki ya kutaka msaada wenu, ila kwa sababu tunataka kuwapeni mfano.
not because we do not have the right, but to make ourselves an example to you, that you should imitate us.
10 Tulipokuwa pamoja nanyi tulikuwa tukiwaambieni, “Mtu asiyefanya kazi, asile.”
For even when we were with you, we commanded you this: "If anyone will not work, neither let him eat."
11 Tunasema mambo hayo kwa sababu tumesikia kwamba wako baadhi yenu ambao ni wavivu na ambao hawafanyi chochote, isipokuwa tu kujiingiza katika mambo ya watu wengine.
For we hear that some among you are living an undisciplined life, who do not work at all, but are busybodies.
12 Kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo tunawaamuru na kuwaonya watu hao wawe na nidhamu na kufanya kazi ili wajipatie maslahi yao wenyewe.
Now those who are that way, we command and exhort in the Lord Jesus Christ, that with quietness they work, and eat their own bread.
13 Lakini ninyi ndugu, msichoke kutenda mema.
But you, brothers, do not be weary in doing well.
14 Huenda kwamba huko kuna mtu ambaye hatautii huu ujumbe tunaowapelekeeni katika barua hii. Ikiwa hivyo, basi, mfichueni mtu huyo na msiwe na uhusiano wowote naye kusudi aone aibu.
If anyone does not obey our word in this letter, note that person, that you have no company with him, to the end that he may be ashamed.
15 Lakini msimtendee mtu huyo kama adui, bali mwonyeni kama ndugu.
Do not count him as an enemy, but admonish him as a brother.
16 Bwana mwenyewe ndiye chanzo cha amani, awajalieni amani siku zote kwa kila namna. Bwana awe nanyi nyote.
Now may the Lord of peace himself give you peace at all times in all ways. The Lord be with you all.
17 Kwa mkono wangu mwenyewe naandika hivi: Salamu kutoka kwa Paulo! Hivi ndivyo ninavyotia sahihi kila barua; ndivyo ninavyoandika.
The greeting of me, Paul, with my own hand, which is the sign in every letter: this is how I write.
18 Tunawatakieni nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.
The grace of our Lord Jesus Christ be with you all.