< 2 Wathesalonike 2 >

1 Sasa yahusu kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo na kukusanywa kwetu pamoja tukae naye. Ndugu, tunawaombeni sana
Quant à l'apparition de notre Seigneur Jésus-Christ et à notre réunion à lui, frères, nous vous en supplions,
2 msifadhaike upesi moyoni, na wala msitiwe wasiwasi kwa sababu ya madai kwamba Siku ya Bwana imekwisha fika. Labda inadhaniwa kwamba jambo hili limetokana na uaguzi fulani, mahubiri au barua inayosemekana kuwa imetoka kwetu.
n'allez pas vite vous monter l'imagination, ne vous laissez pas troubler par de fausses inspirations, ou par des paroles ou par de prétendues lettres de nous, vous annonçant que nous sommes arrivés au jour du Seigneur.
3 Msikubali kudanganywa na mtu yeyote kwa namna yoyote ile. Maana Siku hiyo haitakuja mpaka kwanza ule Uasi Mkuu utokee na yule Mwovu aonekane ambaye mwisho wake ni kuangamizwa kabisa.
Ne vous laissez tromper par rien ni par personne: il n'arrivera rien avant qu'ait eu lieu la grande apostasie et que se soit révélé l'homme de l'iniquité, le fils de la perdition,
4 Yeye atapinga kila kitu wanachokiona watu kuwa ni mungu, au wanachokiabudu. Naam, hata ataingia na kuketi ndani ya Hekalu la Mungu akijidai kuwa Mungu.
le grand adversaire «s'élevant au-dessus de tout ce qu'on appelle Dieu» et qu'on adore, jusqu'à s'installer dans le temple de Dieu et se présenter comme étant Dieu lui-même.
5 Je, hamkumbuki kwamba niliwaambieni haya yote wakati nilipokuwa pamoja nanyi?
Ne vous souvenez-vous pas que je vous disais cela quand j'étais encore auprès de vous?
6 Lakini kuna kitu kinachomzuia sasa, nanyi mwakijua kitu hicho. Basi, huyo Mwovu ataonekana wakati wake ufaao.
Vous savez bien ce qui l'empêche de paraître et pourquoi il ne se révélera que lorsque son heure sera venue.
7 Hata hivyo, Mwovu huyo aliyefichika anafanya kazi sasa, lakini hataonekana mpaka yule anayemzuia aondolewe.
L'iniquité exerce déjà sa mystérieuse action; elle éclatera quand celui qui l'arrête encore aura disparu.
8 Hapo ndipo Mwovu atakapotokea; lakini Bwana Yesu anapokuja atamuua kwa pumzi ya kinywa chake na kumwangamiza kwa mng'ao wa kuja kwake.
Alors se révélera l'impie que le Seigneur Jésus «Tuera du souffle de sa bouche» et anéantira par l'éclat de son apparition.
9 Huyo Mwovu atakuja na nguvu za Shetani na kufanya kila namna ya miujiza na maajabu ya uongo,
Quant à l'apparition de l'impie, elle se fera par la puissance de Satan, avec toutes sortes de miracles, de signes, de prodiges menteurs
10 na kutumia udanganyifu wa kila namna kwa wale walio katika mkumbo wa kupotea. Hao watapotea kwa sababu hawakuupokea na kuupenda ule ukweli ili waokolewe.
et une foule de séductions coupables pour les hommes qui vont périr, qui n'ont pas voulu accepter et aimer la vérité qui les eût sauvés.
11 Ndiyo maana Mungu amewaweka chini ya nguvu ya upotovu, wauamini uongo.
Voilà pourquoi Dieu leur envoie un formidable penchant pour l'erreur qui les fait croire au mensonge,
12 Matokeo yake ni kwamba wote wasioamini ukweli, ila wafurahia dhambi, watahukumiwa.
afin que tous ceux qui n'auront pas cru à la vérité et se seront complus dans le mal tombent sous son jugement.
13 Tunapaswa kumshukuru Mungu daima kwa ajili yenu ninyi ndugu, ninyi mnaopendwa na Bwana, kwa maana Mungu amewateua tangu mwanzo mpate kuokolewa kwa nguvu ya Roho mfanywe watu wake watakatifu kwa imani yenu katika ukweli.
Quant à nous, frères chéris du Seigneur, nous devons rendre à Dieu, pour vous, de continuelles actions de grâces de ce qu'il vous a choisis depuis le commencement pour vous sauver par la sanctification de l'Esprit et par la foi en la vérité;
14 Mungu aliwaitieni jambo hili kwa njia ya Habari Njema tuliyowahubirieni; aliwaiteni mpate kupokea sehemu yenu katika utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.
il vous a appelés à cet état par notre prédication de l'Évangile, afin que vous prissiez part à la gloire de notre Seigneur Jésus-Christ.
15 Basi, ndugu, simameni imara na zingatieni yale mafundisho tuliyowafundisheni kwa mahubiri yetu na barua zetu.
Restez donc fermes, frères, et retenez les enseignements que nous vous avons donnés soit de vive voix, soit dans notre lettre.
16 Tunamwomba Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu ambaye alitupenda, na kwa neema yake akatujalia faraja ya milele na tumaini jema, (aiōnios g166)
Que notre Seigneur Jésus-Christ lui-même et que Dieu notre Père, qui nous a aimés et nous a donné dans sa grâce une consolation éternelle et une douce espérance, (aiōnios g166)
17 aifariji mioyo yenu na kuwaimarisheni ili mweze daima kutenda na kusema yaliyo mema.
consolent vos coeurs et vous affermissent en toute bonne oeuvre et en toute bonne parole.

< 2 Wathesalonike 2 >