< 2 Wathesalonike 2 >

1 Sasa yahusu kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo na kukusanywa kwetu pamoja tukae naye. Ndugu, tunawaombeni sana
Now concerning the coming of our Lord Jesus Christ and our being gathered to him, we ask you, brothers,
2 msifadhaike upesi moyoni, na wala msitiwe wasiwasi kwa sababu ya madai kwamba Siku ya Bwana imekwisha fika. Labda inadhaniwa kwamba jambo hili limetokana na uaguzi fulani, mahubiri au barua inayosemekana kuwa imetoka kwetu.
not to be quickly shaken from your understanding or alarmed by any spirit or message or by any letter supposedly from us alleging that the day of Christ has already come.
3 Msikubali kudanganywa na mtu yeyote kwa namna yoyote ile. Maana Siku hiyo haitakuja mpaka kwanza ule Uasi Mkuu utokee na yule Mwovu aonekane ambaye mwisho wake ni kuangamizwa kabisa.
Let no one deceive you in any manner, for that day cannot come unless the apostasy comes first and the man of sin is revealed, the son of destruction.
4 Yeye atapinga kila kitu wanachokiona watu kuwa ni mungu, au wanachokiabudu. Naam, hata ataingia na kuketi ndani ya Hekalu la Mungu akijidai kuwa Mungu.
He will oppose and exalt himself above every so-called god and object of worship, so that he sits as God in the temple of God, proclaiming himself to be God.
5 Je, hamkumbuki kwamba niliwaambieni haya yote wakati nilipokuwa pamoja nanyi?
Do you not remember that I told you these things when I was still with you?
6 Lakini kuna kitu kinachomzuia sasa, nanyi mwakijua kitu hicho. Basi, huyo Mwovu ataonekana wakati wake ufaao.
And you know what is now restraining him so that he will be revealed in his own time.
7 Hata hivyo, Mwovu huyo aliyefichika anafanya kazi sasa, lakini hataonekana mpaka yule anayemzuia aondolewe.
For the mystery of lawlessness is already at work, but the one who now restrains will do so until he is taken out of the way.
8 Hapo ndipo Mwovu atakapotokea; lakini Bwana Yesu anapokuja atamuua kwa pumzi ya kinywa chake na kumwangamiza kwa mng'ao wa kuja kwake.
And then the lawless one will be revealed, whom the Lord will destroy with the breath of his mouth and annihilate by the appearance of his coming.
9 Huyo Mwovu atakuja na nguvu za Shetani na kufanya kila namna ya miujiza na maajabu ya uongo,
The coming of the lawless one will be in accordance with the working of Satan, with all kinds of counterfeit miracles, signs, and wonders,
10 na kutumia udanganyifu wa kila namna kwa wale walio katika mkumbo wa kupotea. Hao watapotea kwa sababu hawakuupokea na kuupenda ule ukweli ili waokolewe.
and with every kind of wicked deception among those who are perishing, because they refused to love the truth and so be saved.
11 Ndiyo maana Mungu amewaweka chini ya nguvu ya upotovu, wauamini uongo.
For this reason God will send them a powerful delusion, leading them to believe what is false,
12 Matokeo yake ni kwamba wote wasioamini ukweli, ila wafurahia dhambi, watahukumiwa.
so that all who have not believed the truth but have taken pleasure in unrighteousness will be condemned.
13 Tunapaswa kumshukuru Mungu daima kwa ajili yenu ninyi ndugu, ninyi mnaopendwa na Bwana, kwa maana Mungu amewateua tangu mwanzo mpate kuokolewa kwa nguvu ya Roho mfanywe watu wake watakatifu kwa imani yenu katika ukweli.
But we must always give thanks to God for you, brothers beloved by the Lord, because God chose you from the beginning for salvation through sanctification by the Spirit and belief in the truth.
14 Mungu aliwaitieni jambo hili kwa njia ya Habari Njema tuliyowahubirieni; aliwaiteni mpate kupokea sehemu yenu katika utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.
He called you to this through our gospel, so that you might obtain the glory of our Lord Jesus Christ.
15 Basi, ndugu, simameni imara na zingatieni yale mafundisho tuliyowafundisheni kwa mahubiri yetu na barua zetu.
So then, brothers, stand firm and hold fast to the teachings that were passed on to you, whether by word of mouth or by a letter from us.
16 Tunamwomba Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu ambaye alitupenda, na kwa neema yake akatujalia faraja ya milele na tumaini jema, (aiōnios g166)
Now may our Lord Jesus Christ himself and God our Father, who has loved us and given us eternal comfort and good hope by his grace, (aiōnios g166)
17 aifariji mioyo yenu na kuwaimarisheni ili mweze daima kutenda na kusema yaliyo mema.
comfort your hearts and establish you in every good word and work.

< 2 Wathesalonike 2 >