< 2 Wathesalonike 1 >
1 Mimi Paulo, Silwano na Timotheo tunawaandikia ninyi jumuiya ya kanisa la Thesalonike, ambao ni watu wake Mungu Baba yetu na wa Bwana Yesu Kristo.
To the Thessalonian Church in union with God our Father and the Lord Jesus Christ, From Paul, Silas, and Timothy.
2 Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
May God, the Father, and the Lord Jesus Christ bless you and give you peace.
3 Ndugu, tunapaswa kushukuru Mungu daima kwa ajili yenu. Inafaa kwetu kufanya hivyo kwani imani yenu inakua sana na kupendana kwenu kunaongezeka sana.
Brothers, it is our duty always to thank God about you, as is but right, considering the wonderful growth of your faith, and because, without exception, your love for one another is continually increasing.
4 Ndio maana sisi tunajivunia ninyi katika makanisa ya Mungu. Tunaona fahari juu ya jinsi mnavyoendelea kuamini na kustahimili katika udhalimu wote na mateso mnayopata.
So much is this the case that we ourselves speak with pride, before the Churches of God, of the patience and faith which you have shown, in spite of all the persecutions and troubles that you are enduring.
5 Hayo yote yanathibitisha kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki, na matokeo yake ninyi mtastahili Utawala wake ambao kwa ajili yake mnateseka.
These persecutions will vindicate the justice of God’s judgment, and will result in your being reckoned worthy of God’s Kingdom, for the sake of which you are now afflicted;
6 Mungu atafanya jambo la haki: atawalipa mateso wale wanaowatesa ninyi,
since God deems it just to inflict suffering upon those who are now inflicting suffering upon you,
7 na kuwapeni nafuu ninyi mnaoteseka, na sisi pia. Atafanya jambo hilo wakati Bwana atakapotokea kutoka mbinguni pamoja na malaika wake na wakuu
and to give relief to you who are suffering, as well as to us, at the Appearing of the Lord Jesus from Heaven with his mighty angels, ‘in flaming fire.’
8 na miali ya moto, kuwaadhibu wale wanaomkataa Mungu na wale wasiotii Habari Njema ya Bwana wetu Yesu.
Then he will ‘inflict punishment upon those who refuse to know God, and upon those who turn a deaf ear’ to the Good News of Jesus, our Lord.
9 Adhabu yao itakuwa kuangamizwa milele na kutengwa mbali na utukufu wake mkuu, (aiōnios )
These men will pay the penalty of unutterable Ruin — banished ‘from the presence of the Lord and from the glorious manifestation of his might, (aiōnios )
10 wakati atakapokuja Siku ile kupokea utukufu kutoka kwa watu wake na heshima kutoka kwa wote wanaoamini. Ninyi pia mtakuwa miongoni mwao, kwani mmeuamini ule ujumbe tuliowaletea.
when he comes to be honour ed in his People,’ and to be revered in all who have learned to believe in him (for you also believed our testimony) — as he will be on ‘That Day.’
11 Ndiyo maana tunawaombeeni daima. Tunamwomba Mungu wetu awawezeshe muyastahili maisha aliyowaitia myaishi. Tunamwomba, kwa uwezo wake, atimize nia yenu ya kutenda mema na kukamilisha kazi yenu ya imani.
With this in view, our constant prayer for you is that our God may count you worthy of the Call that you have received, and by his power make perfect your delight in all goodness and the efforts that have resulted from your faith.
12 Kwa namna hiyo, jina la Bwana wetu Yesu litapata utukufu kutoka kwenu, nanyi mtapata utukufu kutoka kwake kwa neema ya Mungu wetu na ya Bwana Yesu Kristo.
Then, in the loving-kindness of our God and the Lord Jesus Christ, will the name of Jesus, our Lord, be honoured in you, and you in him.