< 2 Wathesalonike 1 >
1 Mimi Paulo, Silwano na Timotheo tunawaandikia ninyi jumuiya ya kanisa la Thesalonike, ambao ni watu wake Mungu Baba yetu na wa Bwana Yesu Kristo.
This letter comes from Paul, Silvanus, and Timothy to the church of the Thessalonians who belong to God our Father and the Lord Jesus Christ.
2 Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
May you have grace and peace from God the Father and the Lord Jesus Christ.
3 Ndugu, tunapaswa kushukuru Mungu daima kwa ajili yenu. Inafaa kwetu kufanya hivyo kwani imani yenu inakua sana na kupendana kwenu kunaongezeka sana.
We keep on thanking God for you, brothers and sisters—we just have to! This is the right thing to do because your trust in God is growing in leaps and bounds, and the love you all have for each other increases more and more.
4 Ndio maana sisi tunajivunia ninyi katika makanisa ya Mungu. Tunaona fahari juu ya jinsi mnavyoendelea kuamini na kustahimili katika udhalimu wote na mateso mnayopata.
We speak so proudly of you among the churches of God because of your patient courage and trust in God during all the persecution and trouble you're going through.
5 Hayo yote yanathibitisha kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki, na matokeo yake ninyi mtastahili Utawala wake ambao kwa ajili yake mnateseka.
For this is evidence that God is right in the decisions he makes, and that you deserve the kingdom of God for which you are suffering.
6 Mungu atafanya jambo la haki: atawalipa mateso wale wanaowatesa ninyi,
Since God does what's right he will deal appropriately with those who cause you trouble.
7 na kuwapeni nafuu ninyi mnaoteseka, na sisi pia. Atafanya jambo hilo wakati Bwana atakapotokea kutoka mbinguni pamoja na malaika wake na wakuu
He will free you from your suffering—and us too—when the Lord Jesus appears from heaven in blazing fire with his powerful angels,
8 na miali ya moto, kuwaadhibu wale wanaomkataa Mungu na wale wasiotii Habari Njema ya Bwana wetu Yesu.
bringing judgment on those who reject God and refuse to accept the good news of our Lord Jesus.
9 Adhabu yao itakuwa kuangamizwa milele na kutengwa mbali na utukufu wake mkuu, (aiōnios )
They will rightly experience the consequence of eternal loss, separated from the presence of the Lord and his glorious power, (aiōnios )
10 wakati atakapokuja Siku ile kupokea utukufu kutoka kwa watu wake na heshima kutoka kwa wote wanaoamini. Ninyi pia mtakuwa miongoni mwao, kwani mmeuamini ule ujumbe tuliowaletea.
on the day when he comes to receive glory from his people, admired by all those who trust in him. This includes you because you were convinced about what we told you.
11 Ndiyo maana tunawaombeeni daima. Tunamwomba Mungu wetu awawezeshe muyastahili maisha aliyowaitia myaishi. Tunamwomba, kwa uwezo wake, atimize nia yenu ya kutenda mema na kukamilisha kazi yenu ya imani.
That's why we continue to pray for you, that our God may make you worthy of what he's called us to do. May God powerfully fulfill every desire you have to do good and every action that comes from trusting him
12 Kwa namna hiyo, jina la Bwana wetu Yesu litapata utukufu kutoka kwenu, nanyi mtapata utukufu kutoka kwake kwa neema ya Mungu wetu na ya Bwana Yesu Kristo.
so that the name of our Lord Jesus may be honored by what you do—and in turn you are honored by him through the grace of our God and the Lord Jesus Christ.