< 2 Petro 2 >

1 Palitokea manabii wa uongo kati ya watu, na vivyo hivyo walimu wa uongo watatokea kati yenu. Watu hao wataingiza mafundisho maharibifu na kumkana Bwana aliyewakomboa, na kwa njia hiyo watasababisha ghafla maangamizi yao wenyewe.
However, there were also false prophets among the people, just as, indeed, there will be false teachers among you, who will introduce destructive heresies, even denying the Owner who bought them (bringing on themselves swift destruction).
2 Tena watu wengi watazifuata hizo njia zao mbaya, kwa sababu yao, wengine wataipuuza Njia ya ukweli.
And many will follow their licentious ways, because of which the way of the Truth will be defamed.
3 Kwa tamaa yao mbaya watajipatia faida kwa kuwaambieni hadithi za uongo. Lakini kwa muda mrefu sasa Hakimu wao yu tayari, na Mwangamizi wao yu macho!
And in covetousness they will exploit you with deceptive words; since way back the judgment for such people is not slack, and their destruction will not sleep.
4 Malaika walipotenda dhambi, Mungu hakuwahurumia, bali aliwatupa katika moto wa Jehanamu ambako wamefungwa wakingojea Siku ile ya Hukumu. (Tartaroō g5020)
Because if God did not spare angels when they sinned, but delivered them into chains of darkness, confining them in Tartarus to be reserved for judgment, (Tartaroō g5020)
5 Mungu hakuihurumia dunia ya hapo kale, bali alileta gharika kuu juu ya nchi ile ya watu wasiomcha Mungu; lakini Noa ambaye alihubiri uadilifu, Mungu alimwokoa pamoja na watu wengine saba.
and did not spare the ancient world but preserved Noah, with seven others, a preacher of righteousness, when He brought a flood on the world of the ungodly,
6 Mungu aliadhibu miji ya Sodoma na Gomora, akaiteketeza kwa moto, akaifanya iwe mfano wa mambo yatakayowapata watu wasiomcha Mungu.
and condemned the cities of Sodom and Gomorrah to destruction, reducing them to ashes (providing a warning to those who are intent on being ungodly),
7 Alimwokoa Loti, mtu mwema, ambaye alisikitishwa sana na mwenendo mbaya wa watu hao waasi.
while He rescued upright Lot, who was distressed by the licentious lifestyle of the wicked
8 Loti aliishi miongoni mwa watu hao, na kwa siku nyingi moyo wake ulikuwa katika wasiwasi mkuu aliposikia matendo yao maovu.
(for that upright man, dwelling among them, tormented an upright soul from day to day by seeing and hearing lawless deeds)
9 Kwa hiyo, basi, Bwana anajua jinsi ya kuwaokoa katika majaribu watu wanaomcha Mungu, na jinsi ya kuwaweka waovu katika adhabu hadi Siku ile ya hukumu,
—then the Lord knows how to deliver the godly out of testings and to reserve the unjust under punishment for the day of judgment,
10 hasa wale wanaofuata tamaa mbaya za mwili na kupuuza mamlaka. Watu hao ni washupavu na wenye majivuno, huvitukana na hawaviheshimu viumbe vitukufu vya juu.
and especially those who go after the flesh in the lust for defilement, and despise authority. They are audacious, self-willed; they are not afraid to revile majestic beings,
11 Lakini malaika, ambao wana uwezo na nguvu zaidi kuliko hao walimu wa uongo, hawawashtaki na kuwatukana hao mbele ya Bwana.
whereas angels, though being greater in might and power, do not bring a reviling accusation against them before the Lord.
12 Watu hao ambao hutukana chochote kile wasichoelewa, ni sawa na wanyama wasio na akili, ambao huzaliwa na baadaye hukamatwa na kuchinjwa! Wataangamizwa kutokana na uharibifu wao wenyewe,
But these, as unreasoning animals, creatures of instinct made to be caught and destroyed, spouting off in matters of which they are ignorant, will be destroyed by their own depravity,
13 na watalipwa mateso kwa mateso ambayo wameyasababisha. Furaha yao ni kufanya, tena mchana kabisa, chochote kinachotosheleza anasa zao za mwili. Hao ni fedheha na aibu tupu kwa jumuiya yenu wakati wanapojiunga nanyi katika karamu zenu, bali wakifurahia njia zao za udanganyifu.
receiving the wages of unrighteousness. Counting it a pleasure to carouse in the daytime, they are stains and blemishes, reveling in their own deceptions while they feast with you,
14 Macho yao yamejaa uzinzi na uwezo wao wa kutenda dhambi hauna kikomo. Huwaongoza watu walio dhaifu mpaka mitegoni. Mioyo yao imezoea kuwa na tamaa ya mali. Wapo chini ya laana ya Mungu!
having eyes full of adultery and that cannot cease from sin, enticing unstable souls; having a heart trained in greediness they are children of a curse;
15 Wameiacha njia iliyonyoka, wakapotoka na kuifuata njia aliyofuata Balaamu, mwana wa Beori, ambaye alipendelea kupata faida kwa kufanya udanganyifu,
having forsaken the right way they have gone astray, having followed the way of Balaam of Bosor, who loved the wages of unrighteousness;
16 akakaripiwa kwa ajili ya uovu wake. Punda ambaye hasemi alinena kwa sauti ya binadamu, akaukomesha wazimu wa huyo nabii.
but he got a rebuke for his wrongdoing—a mute donkey speaking with a human voice restrained the insanity of the prophet.
17 Watu hao ni kama chemchemi zilizokauka, kama mawingu yanayopeperushwa na tufani; makao yao waliyowekewa ni mahali pa giza kuu.
These are waterless springs, clouds driven by a storm, for whom the blackest of the darkness has been reserved forever. (questioned)
18 Husema maneno ya majivuno na yasiyo na maana, na kutumia tamaa zao mbaya za kimwili kuwatega wale ambao wamejitenga hivi karibuni na watu waishio katika udanganyifu.
Because speaking pompous words of emptiness they entice through fleshly lusts, through licentiousness, those who have actually escaped from those who are living in error,
19 Huwaahidi watu wengine eti watakuwa huru, kumbe wao wenyewe ni watumwa wa upotovu—maana mtu ni mtumwa wa chochote kile kinachomtawala.
promising them freedom while they themselves are slaves of corruption; for by whom a person is overcome, by him also he is brought into bondage.
20 Watu waliokwisha ponyoka katika upotovu wa ulimwengu kwa kupata kumjua Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, kisha wakakubali kunaswa na kutawaliwa tena na upotovu huo, hali yao itakuwa mbaya zaidi kuliko awali.
For if, after they have escaped the defilements of the world through the real knowledge of the Lord and Savior Jesus Christ, they are again entangled in them and overcome, the latter circumstances have become worse for them than the first ones.
21 Ingalikuwa afadhali kwao kama wasingalijua kamwe njia hiyo ya uadilifu kuliko kujua na kisha kuiacha na kupoteza amri takatifu waliyopokea.
For it would have been better for them not to have really known the way of the righteousness, than having really known it to turn back from the holy commandment delivered to them.
22 Ipo mithali isemayo: “Mbwa huyarudia matapishi yake mwenyewe,” na nyingine isemayo: “Nguruwe aliyekwisha oshwa hugaagaa tena katika matope!” Ndivyo ilivyo kwao sasa.
But it has happened to them according to the true proverb: a dog returns to its own vomit and a bathed sow to wallowing in mud.

< 2 Petro 2 >