< 2 Yohana 1 >

1 Mimi Mzee nakuandikia wewe Bimkubwa mteule, pamoja na watoto wako ninaowapenda kweli. Wala si mimi tu ninayewapenda, bali pia wote wanaoujua ule ukweli wanawapenda ninyi,
Starejšina gospé izvoljeni in otrokom njenim, katere jaz ljubim v resnici, (in ne jaz sam, nego tudi vsi, ki so spoznali resnico),
2 kwa sababu ukweli unakaa nasi milele. (aiōn g165)
Po resnici, katera ostaja v nas, in z nami bode vekomaj; (aiōn g165)
3 Neema na huruma na amani zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo, Mwana wa Baba, zitakuwa pamoja nasi katika ukweli na upendo.
Z vami bode milost, usmiljenje, mir od Boga očeta in od Gospoda Jezusa Kristusa, sina očetovega, v resnici in ljubezni.
4 Nilifurahi sana kuona kwamba baadhi ya watoto wako wanaishi katika ukweli kama Baba alivyotuamuru.
Veselil sem se močno, ker sem našel izmed otrok tvojih, ki hodijo v resnici, kakor smo zapoved dobili od očeta.
5 Basi, Bimkubwa, ninalo ombi moja kwako: tupendane. Ombi hili si amri mpya, bali ni amri ileile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo.
In sedaj te prosim, pospá, ne da bi ti pisal novo zapoved, nego katero smo imeli od začetka, da se ljubimo med seboj.
6 Upendo maana yake ni kuishi kwa kuzitii amri zake Mungu. Amri niliyoisikia tangu mwanzo ndiyo hii: mnapaswa nyote kuishi katika upendo.
In to je ljubezen, da živimo po zapovedih njegovih. To je zapoved, kakor ste slišali od začetka, da v njej živite;
7 Wadanganyifu wengi wamezuka duniani, watu ambao hawakiri kwamba Yesu Kristo amekuja kwetu akawa binadamu. Mtu asemaye hivyo ni mdanganyifu na ni Adui wa Kristo.
Ker mnogi sleparji prišli so na svet, kateri ne spoznavajo Jezusa Kristusa, da je prišel v mesu. Ta je slepar in protikrist.
8 Basi, jihadharini ninyi wenyewe ili msije mkapoteza kile mlichokishugulikia, bali mpate tuzo lenu kamili.
Pazite, da ne izgubimo, kar smo pridelali, nego dobimo polno plačilo.
9 Asiyezingatia na kudumu katika mafundisho ya Kristo, bali anayakiuka, hana Mungu. Lakini anayedumu katika mafundisho hayo anaye Baba na Mwana.
Vsak, kdor prestopa in ne ostaja v uku Kristusovem, nima Boga; kdor ostaja v uku Kristusovem, ta ima očeta in sina.
10 Basi, kama mtu akija kwenu bila kuwaleteeni mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani kwenu, wala msimsalimu.
Če kdo pride k vam, in ne prinese tega uka, ne sprejemajte ga v hišo, in ne pozdravljajte ga;
11 Maana anayemsalimu mtu huyo, anashirikiana naye katika matendo yake maovu.
Kajti kdor ga pozdravlja, udeležuje se hudobnih del njegovih.
12 Ninayo mengi ya kuwaambieni lakini sipendi kufanya hivyo kwa karatasi na wino; badala yake, natumaini kuwatembeleeni na kuzungumza nanyi ana kwa ana, ili furaha yetu ikamilike.
Mnogo sem imel vam pisati, a nisem hotel s papirjem in črnilom; ali upam priti k vam, in iz ust do ust govoriti, da bode veselje vaše popolno.
13 Watoto wa dada yako mteule wanakusalimu.
Pozdravljajo te otroci sestre tvoje izvoljene. Amen.

< 2 Yohana 1 >