< 2 Yohana 1 >

1 Mimi Mzee nakuandikia wewe Bimkubwa mteule, pamoja na watoto wako ninaowapenda kweli. Wala si mimi tu ninayewapenda, bali pia wote wanaoujua ule ukweli wanawapenda ninyi,
The elder to the chosen lady and her children, whom I love in truth—and not only I, but also all who know the truth—
2 kwa sababu ukweli unakaa nasi milele. (aiōn g165)
because of the truth that abides in us and will be with us forever: (aiōn g165)
3 Neema na huruma na amani zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo, Mwana wa Baba, zitakuwa pamoja nasi katika ukweli na upendo.
Grace, mercy, and peace will be with us from God the Father and from the Lord Jesus Christ, the Son of the Father, in truth and love.
4 Nilifurahi sana kuona kwamba baadhi ya watoto wako wanaishi katika ukweli kama Baba alivyotuamuru.
I was overjoyed to find some of yoʋr children walking in the truth, just as we have been commanded by the Father.
5 Basi, Bimkubwa, ninalo ombi moja kwako: tupendane. Ombi hili si amri mpya, bali ni amri ileile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo.
And now I ask yoʋ, dear lady—not as writing yoʋ a new commandment, but one we have had from the beginning—that we love one another.
6 Upendo maana yake ni kuishi kwa kuzitii amri zake Mungu. Amri niliyoisikia tangu mwanzo ndiyo hii: mnapaswa nyote kuishi katika upendo.
Now this is love, that we walk according to his commandments. This is the commandment, just as you have heard it from the beginning, that you should walk in it.
7 Wadanganyifu wengi wamezuka duniani, watu ambao hawakiri kwamba Yesu Kristo amekuja kwetu akawa binadamu. Mtu asemaye hivyo ni mdanganyifu na ni Adui wa Kristo.
For many deceivers have come into the world, who do not confess that Jesus Christ has come in the flesh. This is the deceiver and the antichrist.
8 Basi, jihadharini ninyi wenyewe ili msije mkapoteza kile mlichokishugulikia, bali mpate tuzo lenu kamili.
Watch yourselves, so that we do not lose what we have worked for, but may receive a full reward.
9 Asiyezingatia na kudumu katika mafundisho ya Kristo, bali anayakiuka, hana Mungu. Lakini anayedumu katika mafundisho hayo anaye Baba na Mwana.
Everyone who transgresses and does not abide in the teaching of Christ does not have God. Whoever abides in the teaching of Christ has both the Father and the Son.
10 Basi, kama mtu akija kwenu bila kuwaleteeni mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani kwenu, wala msimsalimu.
If anyone comes to you and does not bring this teaching, do not receive him into your house, and do not greet him;
11 Maana anayemsalimu mtu huyo, anashirikiana naye katika matendo yake maovu.
for whoever greets him takes part in his evil works.
12 Ninayo mengi ya kuwaambieni lakini sipendi kufanya hivyo kwa karatasi na wino; badala yake, natumaini kuwatembeleeni na kuzungumza nanyi ana kwa ana, ili furaha yetu ikamilike.
Although I have much to write to you, I would rather not use paper and ink. Instead, I hope to come to you and speak face to face, so that our joy may be full.
13 Watoto wa dada yako mteule wanakusalimu.
The children of yoʋr chosen sister greet yoʋ. Amen.

< 2 Yohana 1 >