< 2 Wakorintho 9 >

1 Si lazima kuandika zaidi kuhusu huduma hiyo yenu kwa ajili ya watu wa Mungu.
For of the relief which is for the saints, it is needless for me to write to you.
2 Ninajua jinsi mlivyo na moyo wa kusaidia, na nilijivuna juu yenu kuhusu jambo hilo mbele ya watu wa Makedonia. Niliwaambia: “Ndugu zetu wa Akaya wako tayari tangu mwaka jana.” Hivyo, moto wenu umekwisha wahimiza watu wengi zaidi.
For I know your readiness of mind, on account of which I boasted of you to the Macedonians, that Achaia was ready a year ago: and your zeal has incited very many.
3 Basi, nimewatuma ndugu zetu hao, ili fahari yetu juu yenu ionekane kwamba si maneno matupu, na kwamba mko tayari kabisa na msaada wenu kama nilivyosema.
But I have sent the brethren, that our boasting of you in this respect may not be in vain; that you may be ready, as I said:
4 Isije ikawa kwamba watu wa Makedonia watakapokuja pamoja nami tukawakuta hamko tayari, hapo sisi tutaaibika—bila kutaja aibu mtakayopata ninyi wenyewe—kwa sababu tutakuwa tumewatumainia kupita kiasi.
lest, possibly, should the Macedonians come with me, and find you unprepared, we (not to say you) might be made ashamed by this same confident boasting.
5 Kwa hiyo, nimeona ni lazima kuwaomba hawa ndugu watutangulie kuja kwenu, wapate kuweka tayari zawadi yenu kubwa mliyoahidi; nayo ionyeshe kweli kwamba ni zawadi iliyotolewa kwa hiari na si kwa kulazimishwa.
Therefore, I thought it necessary to exhort the brethren to go before to you, and make ready beforehand your bounty, which has been so much talked of before, that this might be ready as a bounty, and not as a gift extorted from you.
6 Kumbukeni: “Apandaye kidogo huvuna kidogo; apandaye kwa wingi huvuna kwa wingi.”
But remember this, that he who sows sparingly, shall also reap sparingly; and he who sows bountifully, shall also reap bountifully.
7 Kila mmoja, basi, na atoe kadiri alivyoamua, kwa moyo na wala si kwa huzuni au kwa kulazimishwa, maana Mungu humpenda yule mwenye kutoa kwa furaha.
Let each one give, as he purposes in his heart; not with grief, nor from necessity: for God loves a cheerful giver.
8 Mungu anaweza kuwapeni ninyi zaidi ya yale mnayoyahitaji, mpate daima kuwa na kila kitu mnachohitaji, na hivyo mzidi kusaidia katika kila kazi njema.
And God is able to confer every gift upon you abundantly, that you, always having all sufficiency in every thing, may have enough for every good work;
9 Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Yeye hutoa kwa ukarimu, huwapa maskini, wema wahudumu milele.” (aiōn g165)
as it is written: He has scattered abroad; he has given to the poor; his righteousness remains forever. (aiōn g165)
10 Na Mungu ampaye mkulima mbegu na mkate kwa chakula, atawapa ninyi pia mbegu mnazohitaji, na atazifanya ziote, ziwe na kuwapa mavuno mengi ya ukarimu wenu.
Now, he that furnishes seed to the sower will both furnish bread for food, and multiply your seed sown, and increase the fruits of your righteousness;
11 Yeye atawatajirisha ninyi daima kwa kila kitu, ili watu wapate kumshukuru Mungu kwa ajili ya zawadi zenu wanazozipokea kwa mikono yetu.
that you may be enriched in every thing, for all liberality which produces through us thanksgiving to God;
12 Maana huduma hii takatifu mnayoifanya si tu kwamba itasaidia mahitaji ya watu wa Mungu, bali pia itasababisha watu wengi wamshukuru Mungu.
because the administration of this service not only supplies the wants of the saints, but also abounds in many thanksgivings to God;
13 Kutokana na uthibitisho unaoonyeshwa kwa huduma hii yetu, watu watamtukuza Mungu kwa sababu ya uaminifu wenu kwa Habari Njema ya Kristo mnayoiungama, na pia kwa sababu ya ukarimu mnaowapa wao na watu wote.
(since through the proof which this service gives, they glorify God for your acknowledged subjection to the gospel of Christ, and for the liberality of your contribution for them, and for all; )
14 Kwa hiyo watawaombea ninyi kwa moyo kwa sababu ya neema ya pekee aliyowajalieni Mungu.
and in their prayer for you, since they have strong affection for you on account of the eminent grace of God that is in you.
15 Tumshukuru Mungu kwa ajili ya zawadi yake isiyo na kifani!
Thanks be to God for his unspeakable gift.

< 2 Wakorintho 9 >