< 2 Wakorintho 8 >
1 Ndugu, tunapenda kuwapa habari juu ya neema ambazo Mungu ameyajalia makanisa ya Makedonia.
Men vi kundgøre eder, Brødre! den Guds Naade, som er given i Makedoniens Menigheder,
2 Waumini wa huko walijaribiwa sana kwa taabu; lakini furaha yao ilikuwa kubwa hivi hata wakawa wakarimu kupita kiasi, ingawaje walikuwa maskini sana.
at under megen Trængsels Prøvelse har deres overstrømmende Glæde og deres dybe Fattigdom strømmet over i deres Gavmildheds Rigdom.
3 Naweza kushuhudia kwamba walikuwa wakarimu kadiri ya nguvu zao na hata zaidi. Kwa hiari yao wenyewe,
Thi efter Evne (det vidner jeg) gave de, ja, over Evne, af egen Drift,
4 walitusihi sana wapewe nafasi ya kushiriki katika huduma hii ya kuwasaidia watu wa Mungu.
idet de med megen Overtalelse bade os om den Naade at maatte tage Del i Hjælpen til de hellige,
5 Hilo lilikuwa jambo ambalo hatukulitazamia kabisa! Kwanza walijitolea wao wenyewe kwa Bwana, kisha wakajitolea wenyewe kwetu pia, kufuatana na mapenzi ya Mungu.
og ikke alene som vi havde haabet, men sig selv gav de først og fremmest til Herren og saa til os, ved Guds Villie,
6 Kwa sababu hiyo, tulimsihi Tito aliyeianza kazi hiyo awasaidieni pia muitekeleze huduma hii ya upendo miongoni mwenu.
saa at vi opfordrede Titus til, ligesom han forhen havde begyndt, saaledes ogsaa at tilendebringe hos eder ogsaa denne Gave.
7 Ninyi mna kila kitu: imani, uwezo wa kusema, elimu; bidii yote ya kutenda mema, na upendo wenu kwetu. Hivyo, tunatazamia muwe wakarimu katika huduma hii ya upendo.
Men ligesom I ere rige i alt, i Tro og Tale og Erkendelse og al Iver og i eders Kærlighed til os: Maatte I da være rige ogsaa i denne Gave!
8 Siwapi ninyi amri, lakini nataka tu kuonyesha jinsi wengine walivyo na bidii ya kusaidia ili nipate kujua jinsi upendo wenu ulivyo wa kweli.
Jeg siger det ikke som en Befaling, men for ved andres Iver at prøve ogsaa eders Kærligheds Ægthed.
9 Maana, ninyi mnajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo: yeye, ingawa alikuwa na kila kitu, alijifanya maskini kwa ajili yenu, ili kutokana na umaskini wake, awatajirishe.
I kende jo vor Herres Jesu Kristi Naade, at han for eders Skyld blev fattig, da han var rig, for at I ved hans Fattigdom skulde blive rige.
10 Kuhusu jambo hili, basi, nawapeni shauri hili: inafaa kwenu kutekeleza sasa yale mliyoanza mwaka jana. Ninyi mlikuwa wa kwanza kuchukua hatua na kuamua kufanya hivyo.
Og jeg giver min Mening herom til Kende; thi dette er eder gavnligt, I, som jo i Fjor vare de første til at begynde, ikke alene med Gerningen, men endogsaa med Villien dertil.
11 Basi, kamilisheni shughuli hiyo; na kama vile mlivyokuwa na hamu kubwa ya kusaidia, basi, fanyeni bidii vivyo hivyo, kadiri ya uwezo wenu, kuikamilisha.
Men fuldbringer da nu ogsaa Gerningen, for at, ligesom I vare redebonne til at ville, I ogsaa maa fuldbringe det efter eders Evne.
12 Maana ikiwa mtu ana moyo wa kusaidia, Mungu hupokea kila anachoweza kutoa: hadai zaidi.
Thi naar Redebonheden er til Stede, da er den velbehagelig efter, hvad den evner, ikke efter, hvad den ikke evner.
13 Ninyi hampaswi kuongezewa taabu kusudi wengine wapunguziwe mzigo wao; sivyo, ila ni lazima tujali usawa na haki.
Det er nemlig ikke Meningen, at andre skulle have Lettelse og I Trængsel; nej, det skal være ligeligt. Nu for Tiden maa eders Overflod komme hines Trang til Hjælp,
14 Kila mlicho nacho sasa cha ziada kiwasaidie wale wanaohitaji, ili nao wakati watakapokuwa na ziada, wawasaidie ninyi katika mahitaji yenu, na hivyo kuwe na usawa.
for at ogsaa hines Overflod kan komme eders Trang til Hjælp, for at der kan blive Ligelighed,
15 Kama Maandiko yasemavyo: “Aliyekusanya kwa wingi hakuwa na ziada, na yule aliyekusanya kidogo hakupungukiwa.”
som der er skrevet: „Den, som sankede meget, fik ikke for meget, og den, som sankede lidet, fik ikke for lidt.”
16 Namshukuru Mungu aliyeweka ndani ya moyo wa Tito hamu hiyo niliyo nayo mimi ya kuwasaidia.
Men Gud ske Tak, som giver den samme Iver for eder i Titus's Hjerte!
17 Si tu kwamba alikubali ombi letu, ila pia alikuwa na hamu kubwa ya kusaidia, hata akaamua kwa hiari yake mwenyewe kuja kwenu.
Thi vel har han modtaget min Opfordring; men da han er saa ivrig, saa er det af egen Drift, at han rejser til eder.
18 Pamoja naye, tunamtuma ndugu mmoja ambaye sifa zake katika kueneza Habari Njema zimeenea katika makanisa yote.
Og sammen med ham sende vi den Broder, hvis Ros i Evangeliet gaar igennem alle Menighederne,
19 Zaidi ya hayo, yeye amechaguliwa na makanisa awe mwenzetu safarini wakati tunapopeleka huduma hii yetu ya upendo, huduma tunayoifanya kwa ajili ya utukufu wa Bwana na uthibitisho wa nia yetu njema.
og ikke det alene, men han er ogsaa udvalgt af Menederne til at rejse med os med denne Gave, som besørges af os, for at fremme selve Herrens Ære og vor Redebonhed,
20 Tunataka kuepa lawama zinazoweza kutokea kuhusu usimamizi wetu juu ya zawadi hii karimu.
idet vi undgaa dette, at nogen skulde kunne laste os i Anledning af denne rige Hjælp, som besørges af os;
21 Nia yetu ni kufanya vema, si tu mbele ya Bwana, lakini pia mbele ya watu.
thi vi lægge Vind paa, hvad der er godt ikke alene i Herrens, men ogsaa i Menneskers Øjne.
22 Basi, pamoja na ndugu hao, tumemtuma ndugu yetu mwingine ambaye mara nyingi tumempa majaribio mbalimbali, tukamwona kuwa ni mwenye hamu kubwa ya kusaidia; hata sasa amekuwa na moyo zaidi kwa sababu ana imani sana nanyi.
Men sammen med dem sende vi vor Broder, hvis Iver vi ofte i mange Maader have prøvet, men som nu er langt ivrigere paa Grund af sin store Tillid til eder.
23 Tito ni mwenzangu; tunafanya kazi pamoja kwa ajili yenu; lakini kuhusu hawa ndugu zetu wengine, wanaokuja pamoja nao, hao ni wajumbe wa makanisa, na utukufu kwa Kristo.
Hvad Titus angaar, da er han min Fælle og Medarbejder hos eder, og hvad vore Brødre angaar, da ere de Menighedsudsendinge, Kristi Ære.
24 Basi, waonyesheni uthabiti wa upendo wenu, makanisa yapate kuona kweli kwamba fahari ninayoona juu yenu ni ya halali.
Saa giver dem da for Menighedernes Aasyn Beviset paa eders Kærlighed og for det, vi have rost eder for.