< 2 Wakorintho 7 >

1 Basi, wapenzi wangu, tukiwa tumepewa ahadi hizi zote, na tujitakase na chochote kiwezacho kuchafua miili na roho zetu, tuwe watakatifu kabisa, na tuishi kwa kumcha Mungu.
亲爱的朋友们,由于我们做出了这样的承诺,就应该洁净自己,除去身体和心灵上的一切污秽,通过敬畏上帝达成圣洁。
2 Tunaomba mtupe nafasi mioyoni mwenu! Hatujamkosea mtu yeyote, hatujamdhuru wala kumdanganya mtu yeyote.
请接纳我们作为你们的朋友!我们未做过任何措施,没有让任何人堕落,也没有利用过谁。
3 Sisemi mambo haya kwa ajili ya kumhukumu mtu; maana, kama nilivyokwisha sema, ninyi mko mioyoni mwetu, tufe pamoja, tuishi pamoja.
我这样说不是为了定你们的罪,正如我之前所说,你们对我们如此重要,我们与你们可以同生共死。
4 Nina imani kubwa sana ninaposema nanyi; naona fahari kubwa juu yenu! Katika taabu zetu nimepata kitulizo kikubwa na kufurahi mno.
我愿为你们振臂高呼,因为你们让我感到如此光荣。你们就是对我最大的激励,尽管我们经历各种患难,你们让我格外欢喜。
5 Hata baada ya kufika Makedonia hatukuweza kupumzika. Kila upande tulikabiliwa na taabu: nje ugomvi; ndani hofu.
我们抵达马其顿的时候,没有感到片刻的安宁。相反,我们受到了来自各方的攻击,外有争战,内有恐惧。
6 Lakini Mungu, mwenye kuwapa shime wanyonge alitupa moyo sisi pia kwa kuja kwake Tito.
尽管如此,上帝总能给沮丧之人带来鼓励。提多的到来就是我们最大的安慰。
7 Si tu kwa kule kuja kwake Tito, bali pia kwa sababu ya moyo mliompa ninyi. Yeye ametuarifu jinsi mnavyotamani kuniona, jinsi mlivyo na huzuni, na mnavyotaka kunitetea. Jambo hili linanifurahisha sana.
我们的安慰不仅因为他的到来,还因为你们给予他的鼓励。他告诉我们,你们渴望见到我,还因为我而感到难过和忧愁,这让我更加欢喜。
8 Maana, hata kama kwa barua ile yangu nimewahuzunisha, sioni sababu ya kujuta. Naam, naona kwamba barua hiyo iliwatia huzuni lakini kwa muda.
尽管我写的那封信让你们忧伤,但我并不后悔——其实我曾经感到后悔,因为那封信伤害了你们,但只是很短的一段时间。
9 Sasa nafurahi, si kwa sababu mmehuzunika, ila kwa kuwa huzuni yenu imewafanya mbadili nia zenu na kutubu. Mmehuzunishwa kadiri ya mpango wa Mungu, na kwa sababu hiyo hatukuwadhuru ninyi kwa vyovyote.
现在我很快乐,不是因为伤害你们,而是因为这种痛苦让你们改变了心意。你们按照上帝的旨意感到难过,所以不会因为我们而受到任何伤害。
10 Kuwa na huzuni jinsi atakavyo Mungu, husababisha badiliko la moyo, badiliko lenye kuleta wokovu; hivyo hakuna sababu ya kujuta. Lakini huzuni ya kidunia huleta kifo.
上帝希望我们感受到的忧伤,让我们可以改变心意,获得救赎。这种忧伤不会留下遗憾,但世俗的忧伤却会招致死亡。
11 Sasa mnaweza kuona matokeo ya kuona huzuni jinsi Mungu atakavyo: ninyi mmepata kuwa sasa watu wenye jitihada, wenye hoja, mnashtuka na kuogopa, mna bidii na mko tayari kuona kwamba haki yatekelezwa. Ninyi mmethibitisha kwa kila njia kwamba hamna hatia kuhusu jambo hili.
当你们依照上帝的旨意感受到了这种忧伤,看看你们都发生了什么。还记得你们变得多么热情,渴望为自己辩护,对已经发生的事情感到愤怒,认真对待这一切,渴望做正确的事情,关注自己是谁,渴望实现正义。你们通过所有这些改变,表明你们多么诚心地渴望恢复良善正直。
12 Hivyo, ingawa niliandika ile barua, haikuwa kwa ajili ya yule aliyekosa, au kwa ajili ya yule aliyekosewa. Niliandika kusudi ionekane wazi mbele ya Mungu jinsi mlivyo na bidii kwa ajili yetu.
因此,以往我写信给你们,并未讨论谁做错事或被错误对待,而是表达了你们如何在上帝的面前为我们做出奉献。
13 Ndiyo maana sisi tulifarijika sana. Siyo kwamba tulifarijika tu, ila pia Tito alitufurahisha kwa furaha aliyokuwa nayo kutokana na jinsi mlivyomchangamsha moyo.
这让我们备受鼓舞。我们除了感受到鼓舞之外,还很高兴看到提多的欢喜,因为你们让他心安。
14 Mimi nimewasifu sana mbele yake, na katika jambo hilo sikudanganyika. Tumewaambieni ukweli daima, na kule kuwasifia ninyi mbele ya Tito kumekuwa jambo la ukweli mtupu.
我向他夸赞你们,你们没有让我失望。我对你们所说的都是真话,同样,我向提多夸赞你们也是出自真心。
15 Hivyo upendo wake wa moyo kwenu unaongezeka zaidi akikumbuka jinsi ninyi nyote mlivyo tayari kutii, na jinsi mlivyomkaribisha kwa hofu nyingi na kutetemeka.
提多还记起你们如何按照他所说的行事,如何以尊重的方式迎接他。这让他更加关爱你们。
16 Nafurahi sana kwamba naweza kuwategemea ninyi kabisa katika kila jambo.
很高兴我可以对你们怀有充分的信心。

< 2 Wakorintho 7 >