< 2 Wakorintho 6 >

1 Basi, tukiwa wafanyakazi pamoja na Mungu, tunawasihi msikubali ile neema mliyopokea kutoka kwa Mungu ipotee bure.
Working together, we entreat also that you not receive the grace of God in vain,
2 Mungu asema hivi: “Wakati wa kufaa nimekusikiliza, wakati wa wokovu nikakusaidia.” Basi, sasa ndio wakati wa kufaa, sasa ndiyo siku ya wokovu!
for he says, "At an acceptable time I listened to you, and in a day of salvation I helped you." Look, now is the "acceptable time." Look, now is the "day of salvation."
3 Kusudi tusiwe na lawama yoyote katika utumishi wetu, hatupendi kumwekea mtu yeyote kizuio chochote.
We give no occasion of stumbling in anything, that our service may not be blamed,
4 Badala yake, tunajionyesha kuwa kweli watumishi wa Mungu kwa kila kitu: kwa uvumilivu mwingi wakati wa mateso, shida na taabu.
but in everything commending ourselves, as servants of God, in great endurance, in afflictions, in hardships, in distresses,
5 Tumepigwa, tumetiwa gerezani na kuzomewa hadharani; tumefanya kazi tukachoka; tumekesha na kukaa bila kula.
in beatings, in imprisonments, in riots, in labors, in watchings, in fastings;
6 Tunajionyesha kuwa watumishi wa Mungu kwa usafi wa moyo, elimu, uvumilivu na wema; kwa Roho Mtakatifu, kwa upendo usio na unafiki,
in pureness, in knowledge, in patience, in kindness, in the Holy Spirit, in sincere love,
7 kwa ujumbe wa kweli na kwa nguvu ya Mungu. Uadilifu ndiyo silaha yetu upande wa kulia na upande wa kushoto.
in the word of truth, in the power of God; by the armor of righteousness on the right hand and on the left,
8 Tuko tayari kupata heshima na kudharauliwa, kulaumiwa na kusifiwa. Twadhaniwa kuwa waongo, kumbe twasema kweli;
by glory and dishonor, by evil report and good report; as deceivers, and yet true;
9 kama wasiojulikana, kumbe twajulikana kwa wote, kama waliokufa, lakini mwonavyo, sisi ni wazima kabisa.
as unknown, and yet well known; as dying, and look, we live; as punished, and not killed;
10 Ingawa tumeadhibiwa, hatukuuawa; ingawa tunayo huzuni, twafurahi daima; ingawa tu maskini hohehahe, lakini twatajirisha watu wengi; twaonekana kuwa watu tusio na chochote, kumbe tuna kila kitu.
as sorrowful, yet always rejoicing; as poor, yet making many rich; as having nothing, and yet possessing all things.
11 Ndugu Wakorintho, tumezungumza nanyi kwa unyofu; mioyo yetu iko wazi kabisa.
Our mouth is open to you, Corinthians. Our heart is enlarged.
12 Kama mnaona kuna kizuizi chochote kile, kizuizi hicho kiko kwenu ninyi wenyewe, na si kwa upande wetu.
You are not restricted by us, but you are restricted by your own affections.
13 Sasa nasema nanyi kama watoto wangu, wekeni mioyo yenu wazi kama nasi tulivyofanya.
Now in return, I speak as to my children, you also be open wide.
14 Msiambatane na watu wasioamini. Je, wema na uovu vyapatana kweli? Mwanga na giza vyawezaje kukaa pamoja?
Do not be unequally yoked with unbelievers, for what fellowship have righteousness and iniquity? Or what fellowship has light with darkness?
15 Kristo anawezaje kupatana na Shetani? Muumini ana uhusiano gani na asiyeamini?
What agreement has Christ with Belial? Or what portion has a believer with an unbeliever?
16 Hekalu la Mungu lina uhusiano gani na sanamu za uongo? Maana sisi ni hekalu la Mungu aliye hai. Kama Mungu mwenyewe alivyosema: “Nitafanya makao yangu kwao, na kuishi kati yao; Nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”
What agreement has a temple of God with idols? For we are a temple of the living God. Even as God said, "I will dwell in them, and walk in them; and I will be their God, and they will be my people."
17 Kwa hiyo Bwana asema pia: “Ondokeni kati yao, mkajitenge nao, msiguse kitu najisi, nami nitawapokea.
Therefore, "'Go out from their midst, and be separate,' says the Lord, 'and touch no unclean thing,' and I will receive you.
18 Mimi nitakuwa Baba yenu, nanyi mtakuwa watoto wangu, waume kwa wake, asema Bwana Mwenye Uwezo.”
"And I will be a Father to you, and you will be my sons and daughters," says the Lord Almighty.

< 2 Wakorintho 6 >