< 2 Wakorintho 6 >
1 Basi, tukiwa wafanyakazi pamoja na Mungu, tunawasihi msikubali ile neema mliyopokea kutoka kwa Mungu ipotee bure.
我們與天主合作的人,也勸你們不要白受天主的恩寵──
2 Mungu asema hivi: “Wakati wa kufaa nimekusikiliza, wakati wa wokovu nikakusaidia.” Basi, sasa ndio wakati wa kufaa, sasa ndiyo siku ya wokovu!
因為經上說:『在悅納的時候,我俯允了你;在救恩的時日,我幫助了你。』看,如今正是悅納的時候;看,如今正是救恩的時日──
3 Kusudi tusiwe na lawama yoyote katika utumishi wetu, hatupendi kumwekea mtu yeyote kizuio chochote.
我們在任何事上,為避免這職務受詆毀,不但沒有給任何人跌倒的因由,
4 Badala yake, tunajionyesha kuwa kweli watumishi wa Mungu kwa kila kitu: kwa uvumilivu mwingi wakati wa mateso, shida na taabu.
反而處處表現我們自己,有如天主的僕役,就是以持八久的堅忍,在艱難、貧乏、困苦之中,
5 Tumepigwa, tumetiwa gerezani na kuzomewa hadharani; tumefanya kazi tukachoka; tumekesha na kukaa bila kula.
在拷打、監禁、暴亂之中,在勞若、不寢、不食之中,
6 Tunajionyesha kuwa watumishi wa Mungu kwa usafi wa moyo, elimu, uvumilivu na wema; kwa Roho Mtakatifu, kwa upendo usio na unafiki,
以清廉,以明智,以容忍,以慈惠,以聖神,以無偽的愛情,
7 kwa ujumbe wa kweli na kwa nguvu ya Mungu. Uadilifu ndiyo silaha yetu upande wa kulia na upande wa kushoto.
以真理的言辭,以天主的德能,以左右兩手中正義的武器,
8 Tuko tayari kupata heshima na kudharauliwa, kulaumiwa na kusifiwa. Twadhaniwa kuwa waongo, kumbe twasema kweli;
歷經光榮的淩辱,惡名和美名;像是迷惑人的,卻是真誠的;
9 kama wasiojulikana, kumbe twajulikana kwa wote, kama waliokufa, lakini mwonavyo, sisi ni wazima kabisa.
像是人所不知的,卻是人所共知的;像是待死的,看,我們卻活著;像是受懲罰的,卻沒有置於死地;
10 Ingawa tumeadhibiwa, hatukuuawa; ingawa tunayo huzuni, twafurahi daima; ingawa tu maskini hohehahe, lakini twatajirisha watu wengi; twaonekana kuwa watu tusio na chochote, kumbe tuna kila kitu.
像是憂苦的,卻常常喜樂;像是貧困的,卻使許多人富足;像是一無所有的,卻無所不有。
11 Ndugu Wakorintho, tumezungumza nanyi kwa unyofu; mioyo yetu iko wazi kabisa.
格林多人啊! 我們的口向你們張開了,我們的心也敞開了。
12 Kama mnaona kuna kizuizi chochote kile, kizuizi hicho kiko kwenu ninyi wenyewe, na si kwa upande wetu.
你們在我們心內並不窄狹,而是你們的人腸窄狹。
13 Sasa nasema nanyi kama watoto wangu, wekeni mioyo yenu wazi kama nasi tulivyofanya.
為了以報還報,如今我對你們猶如對自己的孩子說:你們也敞開你們的心罷!
14 Msiambatane na watu wasioamini. Je, wema na uovu vyapatana kweli? Mwanga na giza vyawezaje kukaa pamoja?
你們不要與不信的人共負一軛,因為正義與不法之間,那能有什麼相通﹖或者,光明之黑暗,那能有什麼聯繫﹖
15 Kristo anawezaje kupatana na Shetani? Muumini ana uhusiano gani na asiyeamini?
基督之於貝里雅耳,那能有什麼協和﹖或者,信者與不信者,那能有什麼股份﹖
16 Hekalu la Mungu lina uhusiano gani na sanamu za uongo? Maana sisi ni hekalu la Mungu aliye hai. Kama Mungu mwenyewe alivyosema: “Nitafanya makao yangu kwao, na kuishi kati yao; Nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”
天主的殿與偶像,那能有什麼相合﹖的確,我們就是生活的天主的殿,正如天主所說的:『我要在他們內居住,我要在他們中俳徊;我要做他們的天主,他們要做我的百姓。』
17 Kwa hiyo Bwana asema pia: “Ondokeni kati yao, mkajitenge nao, msiguse kitu najisi, nami nitawapokea.
為此,『你們應當從他們中間出來,離開他們──這是上主說的──你們不可觸摸不潔之物,我要收納你們,
18 Mimi nitakuwa Baba yenu, nanyi mtakuwa watoto wangu, waume kwa wake, asema Bwana Mwenye Uwezo.”
我要做你們的父親,你們要做我的子女;這是全能的上主說的。』