< 2 Wakorintho 3 >

1 Je, tunaanza tena kujipendekeza? Je, tunahitaji barua ya utambulisho kwenu, au kutoka kwenu, kama watu wengine?
Ka mimah ingkaw ka mimah kamik kyih qu nu? Thlangkhqi amyihna, nangmih a ven awhkaw aw, am awhtaw nangmih a ham aw kyihnaak cahawn kami ngaih nawh nu?
2 Ninyi wenyewe ni barua yetu; barua iliyoandikwa mioyoni mwetu kila mtu aione na kuisoma.
Nangmih taw, kaimih ak kawlung khuiawh qeena ak awm, thlang boeih ing sim nawh noet uhy, kaimih a capat na awm uhyk ti.
3 Ni dhahiri kwamba ninyi ni barua ya Kristo aliyoipeleka kwa mikono yetu. Barua yenyewe imeandikwa si kwa wino, bali kwa Roho wa Mungu hai; imeandikwa si juu ya kipande cha jiwe, bali juu ya mioyo ya watu.
Nangmih taw, kaimih a bibinaak a phu, Khrih a ven awhkaw capat na awm uhyk ti tice dangsak uhyk ti, catui ing a qee am nawh ak hqing Khawsa ang Myihla ing qee na awm uhyk ti, lungpei awhkaw qee am nawh thlanghqing kawlung awh ni qee na a awm.
4 Tunaweza kusema hayo kwa sababu ya tumaini letu tulilo nalo kwa Mungu kwa njia ya Kristo.
Ve ve Khrih ak caming Khawsa haiawh ningnih a ngaihdingnaak na awm hy.
5 Si kwamba sisi tunaweza kufanya chochote kwa nguvu zetu wenyewe, ila uwezo wetu wote hutoka kwa Mungu:
Ka mimah ak caming ik-oeih ak awm sak amyihna am poek unyng saw ak awm sakkung taw Khawsa ni.
6 maana yeye ndiye aliyetuwezesha kulihudumia Agano Jipya ambalo si agano la sheria iliyoandikwa, bali Agano la Roho. Maana sheria iliyoandikwa huleta kifo, lakini Roho huleta uzima.
Anih ing awikamnaak ak thai awh bibikungkhqi na ni tak khqi hy – cahawn bi amni bi unawh Myihla bi ce ni ni bi uhy; cahawn ingtaw him hlai hy, Myihla ingtaw hqingnaak pehy.
7 Sheria iliwekwa kwa kuandikwa juu ya vipande vya mawe. Ingawaje mwisho wake umekuwa kifo, utukufu wake ulikuwa mkuu mno hata wana wa Israeli wasiweze kuutazama uso wa Mose kwa sababu ya mng'ao wake. Tena mng'ao huo ulikuwa wa muda tu. Basi, ikiwa huduma ya kile ambacho kimesababisha kifo imefanyika kwa utukufu mwingi kiasi hicho,
Lungpei awh qee na ak awm, thihnaak ak law pyikung cahawn ce Mosi ing a haw law awh, cawhkaw bibinaak awh a boeimang haai ce Israelkhqi ing am toek thai uhy, cehlai anih a haai ce thi hqui didi hy,
8 basi, huduma ya Roho ina utukufu mkuu zaidi.
cawhtaw Myihla a bibinaak ak khqoet ikawmyihna a boeimangnaak kaw?
9 Ikiwa basi, kulikuwa na utukufu katika huduma ile iliyoleta hukumu, ni wazi kwamba huduma ile iletayo kukubaliwa kuwa waadilifu itakuwa na utukufu mkuu zaidi.
Thlang ak bo sak bibinaak zani a boeimang awhtaw, dyngnaak ak lawpyi bibinaak ak khqoet ce ikawmyihna nu a boeimangnaak hly!
10 Sasa utukufu mkuu zaidi umechukua nafasi ya ule utukufu uliokuja hapo awali, ambao fahari yake imekwisha toweka.
Ak kqym awh boeimang na ak awm ce tuh awhkaw boeimangnaak ing a poe voelh hawh dawngawh am boeimang voel hy.
11 Maana ikiwa kile kilichokuwa cha muda tu kilikuwa na utukufu wake, bila shaka kile chenye kudumu milele kitakuwa na utukufu mkuu zaidi.
Ak thi hqui didi zani boeimangnaak ing a law awhtaw, a poepa na ak boeimang taw bau khqoet kawm man!
12 Kwa vile hili ndilo tumaini letu, sisi twasema kwa uhodari mkuu.
Cemyih ngaih-unaak ce ni taak dawngawh nim thin cak hy.
13 Sisi hatufanyi kama Mose ambaye alilazimika kuufunika uso wake kwa kitambaa ili watu wa Israeli wasiuone ule mwisho wa mng'ao uliokuwa unafifia.
Mosi amyihna amni awm uhy, Anih ingtaw a hai awhkaw vangnaak a thih hqui voe voe awh Israelkhqi ing hu hau kawm uh, tinawh hi ing dah hy.
14 Lakini akili zao zilipumbazwa. Mpaka leo hii lisomwapo Agano la Kale, kifuniko hicho bado kipo. Kifuniko hicho kitaondolewa tu mtu anapoungana na Kristo.
Cehlai amik kaw mawh hy, tuh dy na awikam kqym ami noet noet awh ami haai dah hyn uhy. Hi ce hliip hlan uhy, Khrih doeng awh cawhkaw hi ce lawh thai na awm hy.
15 Naam, mpaka hivi leo kila isomwapo Sheria ya Mose akili zao huwa zimefunikwa.
Mosi ak cauk ce ami noet awh tuh dy na ami lingbyi dah pek khi hyn hy.
16 Lakini, wakati mtu amgeukiapo Bwana, kifuniko hicho huondolewa.
Cehlai u awm Bawipa benna ak mang taw, cawhkaw hi ce hliip pe hawh hy.
17 Hapa “Bwana” ni Roho; na pale alipo Roho wa Bwana ndipo ulipo uhuru.
Bawipa taw Myihla na awm hy, Bawipa Myihla a awmnaak hoei awh, ngaihdingnaak ce awm hy.
18 Basi, sisi sote ambao nyuso zetu hazikufunikwa, twaonyesha kama katika kioo, utukufu wa Bwana; tunabadilishwa tufanane zaidi na huo mfano wake kwa utukufu mwingi zaidi. Hiyo ni kazi yake Roho wa Bwana.
Ningmih haai dahnaak amak awmkhqi venawh Bawipa a boeimangnaak ce vang hy, amah mi ning myih qu voe voe unawh Myihla na ak awm, Bawipa a ven awhkaw Boeimangnaak ing ni be voe voe uhy.

< 2 Wakorintho 3 >