< 2 Wakorintho 3 >

1 Je, tunaanza tena kujipendekeza? Je, tunahitaji barua ya utambulisho kwenu, au kutoka kwenu, kama watu wengine?
ܡܫܪܝܢܢ ܠܢ ܬܘܒ ܡܢ ܕܪܝܫ ܕܢܚܘܝܟܘܢ ܡܢܐ ܚܢܢ ܐܘ ܕܠܡܐ ܤܢܝܩܝܢܢ ܐܝܟ ܐܚܪܢܐ ܕܐܓܪܬܐ ܕܦܘܩܕܐ ܢܬܟܬܒܢ ܠܟܘܢ ܥܠܝܢ ܐܘ ܕܐܢܬܘܢ ܬܟܬܒܘܢ ܬܦܩܕܘܢ ܥܠܝܢ
2 Ninyi wenyewe ni barua yetu; barua iliyoandikwa mioyoni mwetu kila mtu aione na kuisoma.
ܐܓܪܬܢ ܕܝܢ ܕܝܠܢ ܐܢܬܘܢ ܐܢܘܢ ܕܟܬܝܒܐ ܒܠܒܢ ܘܝܕܝܥܐ ܘܡܬܩܪܝܐ ܡܢ ܟܠܢܫ
3 Ni dhahiri kwamba ninyi ni barua ya Kristo aliyoipeleka kwa mikono yetu. Barua yenyewe imeandikwa si kwa wino, bali kwa Roho wa Mungu hai; imeandikwa si juu ya kipande cha jiwe, bali juu ya mioyo ya watu.
ܝܕܥܝܬܘܢ ܓܝܪ ܕܐܓܪܬܗ ܐܢܬܘܢ ܕܡܫܝܚܐ ܕܐܫܬܡܫܬ ܡܢܢ ܕܟܬܝܒܐ ܠܐ ܒܕܝܘܬܐ ܐܠܐ ܒܪܘܚܐ ܕܐܠܗܐ ܚܝܐ ܠܐ ܒܠܘܚܐ ܕܟܐܦܐ ܐܠܐ ܒܠܘܚܐ ܕܠܒܐ ܕܒܤܪܐ
4 Tunaweza kusema hayo kwa sababu ya tumaini letu tulilo nalo kwa Mungu kwa njia ya Kristo.
ܬܘܟܠܢܐ ܕܝܢ ܗܟܢܐ ܐܝܬ ܠܢ ܒܡܫܝܚܐ ܠܘܬ ܐܠܗܐ
5 Si kwamba sisi tunaweza kufanya chochote kwa nguvu zetu wenyewe, ila uwezo wetu wote hutoka kwa Mungu:
ܠܘ ܕܚܢܢ ܤܦܩܝܢܢ ܕܢܬܪܥܐ ܡܕܡ ܐܝܟ ܕܡܢ ܢܦܫܢ ܐܠܐ ܚܝܠܢ ܡܢ ܐܠܗܐ ܗܘ
6 maana yeye ndiye aliyetuwezesha kulihudumia Agano Jipya ambalo si agano la sheria iliyoandikwa, bali Agano la Roho. Maana sheria iliyoandikwa huleta kifo, lakini Roho huleta uzima.
ܗܘ ܕܐܫܘܝܢ ܕܢܗܘܐ ܡܫܡܫܢܐ ܕܕܝܬܩܐ ܚܕܬܐ ܠܐ ܒܟܬܒܐ ܐܠܐ ܒܪܘܚܐ ܟܬܒܐ ܓܝܪ ܩܛܠ ܪܘܚܐ ܕܝܢ ܡܚܝܐ
7 Sheria iliwekwa kwa kuandikwa juu ya vipande vya mawe. Ingawaje mwisho wake umekuwa kifo, utukufu wake ulikuwa mkuu mno hata wana wa Israeli wasiweze kuutazama uso wa Mose kwa sababu ya mng'ao wake. Tena mng'ao huo ulikuwa wa muda tu. Basi, ikiwa huduma ya kile ambacho kimesababisha kifo imefanyika kwa utukufu mwingi kiasi hicho,
ܐܢ ܕܝܢ ܬܫܡܫܬܐ ܕܡܘܬܐ ܒܟܬܒܐ ܐܬܪܫܡܬ ܒܟܐܦܐ ܘܗܘܬ ܒܬܫܒܘܚܬܐ ܐܝܟܢܐ ܕܠܐ ܢܫܟܚܘܢ ܒܢܝ ܐܝܤܪܝܠ ܠܡܚܪ ܒܦܪܨܘܦܗ ܕܡܘܫܐ ܡܛܠ ܫܘܒܚܐ ܕܦܪܨܘܦܗ ܗܘ ܕܐܬܒܛܠ
8 basi, huduma ya Roho ina utukufu mkuu zaidi.
ܐܝܟܢܐ ܗܟܝܠ ܬܫܡܫܬܐ ܕܪܘܚܐ ܠܐ ܝܬܝܪܐܝܬ ܬܗܘܐ ܒܫܘܒܚܐ
9 Ikiwa basi, kulikuwa na utukufu katika huduma ile iliyoleta hukumu, ni wazi kwamba huduma ile iletayo kukubaliwa kuwa waadilifu itakuwa na utukufu mkuu zaidi.
ܐܢ ܓܝܪ ܠܬܫܡܫܬܐ ܕܚܘܝܒܐ ܗܘܐ ܫܘܒܚܐ ܚܕ ܟܡܐ ܬܬܝܬܪ ܬܫܡܫܬܐ ܕܙܕܝܩܘܬܐ ܒܫܘܒܚܐ
10 Sasa utukufu mkuu zaidi umechukua nafasi ya ule utukufu uliokuja hapo awali, ambao fahari yake imekwisha toweka.
ܐܝܟ ܗܘ ܓܝܪ ܕܐܦܠܐ ܡܫܒܚܐ ܗܝ ܕܐܫܬܒܚܬ ܒܦܘܚܡܐ ܕܗܢܐ ܫܘܒܚܐ ܡܝܬܪܐ
11 Maana ikiwa kile kilichokuwa cha muda tu kilikuwa na utukufu wake, bila shaka kile chenye kudumu milele kitakuwa na utukufu mkuu zaidi.
ܐܢ ܓܝܪ ܡܕܡ ܕܐܬܒܛܠ ܒܫܘܒܚܐ ܗܘܐ ܝܬܝܪܐܝܬ ܐܝܢܐ ܕܡܩܘܐ ܒܫܘܒܚܐ ܢܗܘܐ
12 Kwa vile hili ndilo tumaini letu, sisi twasema kwa uhodari mkuu.
ܡܛܠ ܕܐܝܬ ܠܢ ܗܟܝܠ ܗܢܐ ܤܒܪܐ ܝܬܝܪܐܝܬ ܒܓܠܐ ܥܝܢ ܡܬܕܒܪܝܢܢ
13 Sisi hatufanyi kama Mose ambaye alilazimika kuufunika uso wake kwa kitambaa ili watu wa Israeli wasiuone ule mwisho wa mng'ao uliokuwa unafifia.
ܘܠܐ ܐܝܟ ܡܘܫܐ ܕܪܡܐ ܗܘܐ ܬܚܦܝܬܐ ܥܠ ܐܦܘܗܝ ܕܠܐ ܢܚܘܪܘܢ ܒܢܝ ܐܝܤܪܝܠ ܒܫܘܠܡܗ ܕܗܘ ܕܡܬܒܛܠ
14 Lakini akili zao zilipumbazwa. Mpaka leo hii lisomwapo Agano la Kale, kifuniko hicho bado kipo. Kifuniko hicho kitaondolewa tu mtu anapoungana na Kristo.
ܐܠܐ ܐܬܥܘܪܘ ܒܡܕܥܝܗܘܢ ܥܕܡܐ ܓܝܪ ܠܝܘܡܢܐ ܐܡܬܝ ܕܕܝܬܩܐ ܥܬܝܩܬܐ ܡܬܩܪܝܐ ܗܝ ܗܝ ܬܚܦܝܬܐ ܩܝܡܐ ܥܠܝܗܘܢ ܘܠܐ ܡܬܓܠܝܐ ܕܒܡܫܝܚܐ ܗܘ ܡܬܒܛܠܐ
15 Naam, mpaka hivi leo kila isomwapo Sheria ya Mose akili zao huwa zimefunikwa.
ܘܥܕܡܐ ܠܝܘܡܢܐ ܐܡܬܝ ܕܡܬܩܪܐ ܡܘܫܐ ܬܚܦܝܬܐ ܥܠ ܠܒܗܘܢ ܪܡܝܐ
16 Lakini, wakati mtu amgeukiapo Bwana, kifuniko hicho huondolewa.
ܘܐܡܬܝ ܕܐܢܫ ܡܢܗܘܢ ܢܬܦܢܐ ܠܘܬ ܡܪܝܐ ܡܫܬܩܠܐ ܡܢܗ ܬܚܦܝܬܐ
17 Hapa “Bwana” ni Roho; na pale alipo Roho wa Bwana ndipo ulipo uhuru.
ܡܪܝܐ ܕܝܢ ܗܘܝܘ ܪܘܚܐ ܘܐܬܪ ܕܪܘܚܗ ܕܡܪܝܐ ܚܐܪܘܬܐ ܗܝ
18 Basi, sisi sote ambao nyuso zetu hazikufunikwa, twaonyesha kama katika kioo, utukufu wa Bwana; tunabadilishwa tufanane zaidi na huo mfano wake kwa utukufu mwingi zaidi. Hiyo ni kazi yake Roho wa Bwana.
ܚܢܢ ܕܝܢ ܟܠܢ ܒܐܦܐ ܓܠܝܬܐ ܬܫܒܘܚܬܗ ܕܡܪܝܐ ܐܝܟ ܕܒܡܚܙܝܬܐ ܚܙܝܢܢ ܘܠܗ ܠܕܡܘܬܐ ܡܫܬܚܠܦܝܢܢ ܡܢ ܫܘܒܚܐ ܠܫܘܒܚܐ ܐܝܟ ܕܡܢ ܡܪܝܐ ܪܘܚܐ

< 2 Wakorintho 3 >