< 2 Wakorintho 1 >
1 Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Timotheo, tunawaandikia ninyi mlio kanisa la Mungu huko Korintho, na watu wote wa Mungu kila mahali katika Akaya.
Paul, apôtre de Jésus-Christ par la volonté de Dieu, et Timothée, notre frère, à l'Église de Dieu qui est à Corinthe et à tous les saints qui sont dans toute l'Achaïe.
2 Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.
Que la grâce et la paix vous soient données de la part de Dieu, notre Père, et du Seigneur Jésus-Christ!
3 Atukuzwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba mwenye huruma na Mungu mwenye kuleta faraja yote.
Béni soit Dieu, le Père de notre Seigneur Jésus-Christ, le Père des miséricordes et le Dieu de toute consolation,
4 Yeye hutufariji sisi katika taabu zetu zote, ili nasi tupate kuwafariji wengine katika kila taabu kwa faraja hiyohiyo tunayopokea kutoka kwa Mungu.
qui nous console dans toutes nos afflictions, afin que, par la consolation dont Dieu nous console nous-mêmes, nous puissions aussi consoler les autres, dans quelque affliction qu'ils se trouvent!
5 Naam, kadiri mateso ya Kristo yanavyozidi ndani yetu, ni kadiri hiyohiyo tunazidi kufarijiwa naye.
En effet, de même que les souffrances du Christ abondent en nous, de même aussi notre consolation abonde par le Christ.
6 Ikiwa tunapata taabu, basi ni kwa ajili ya faraja na wokovu wenu. Tukifarijika, ni kwa ajili ya kuwafariji ninyi na kuwaunga mkono mpate nguvu ya kustahimili mateso yaleyale tunayoteseka sisi.
Ainsi, soit que nous soyons affligés, c'est pour votre consolation et votre salut; soit que nous soyons consolés, c'est pour votre consolation, dont la réalité se manifeste par votre patience à supporter les souffrances que nous endurons nous-mêmes.
7 Tena, matumaini tuliyo nayo kwa ajili yenu ni imara; tunajua kwamba mkishiriki mateso yetu, mtashiriki pia faraja yetu.
Et notre espérance à votre sujet est ferme; car nous savons que, comme vous avez part aux souffrances, vous aurez aussi part à la consolation.
8 Ndugu, tunataka kuwajulisheni taabu zilizotupata kule Asia; taabu hizo zilitulemea kupita kiasi, hata tukakata matumaini yote ya kuendelea kuishi.
En effet, mes frères, nous ne voulons pas vous laisser ignorer l'affliction qui nous est survenue en Asie, et dont nous avons été excessivement accablés, au delà même de nos forces, au point que nous désespérions de conserver la vie.
9 Naam, tulikuwa kama watu waliohukumiwa kuuawa, ili tufundishwe kumtegemea Mungu mwenye kuwafufua wafu, badala ya kutegemea nguvu zetu sisi wenyewe.
Bien plus, nous avions prononcé en nous-mêmes notre arrêt de mort, ne voulant pas mettre notre confiance en nous, mais en Dieu qui ressuscite les morts.
10 Yeye alituokoa katika hatari kubwa ya kifo, na anaendelea kutuokoa; sisi tumemwekea tumaini letu kwamba atatuokoa tena,
C'est lui qui nous a délivrés d'un si grand danger de mort, et qui nous en délivrera; oui, nous avons en lui cette espérance, qu'il nous délivrera encore.
11 ninyi mkiwa mnatuunga mkono kwa kutuombea. Hivyo neema tutakazokuwa tumepata kutokana na maombi ya watu wengi hivyo, ziwe sababu ya watu wengi zaidi kumshukuru Mungu kwa ajili yetu.
Et vous-mêmes, vous nous viendrez en aide par vos prières, afin que la grâce, obtenue pour nous par plusieurs personnes, soit aussi, pour plusieurs personnes, une occasion de rendre grâces à notre sujet.
12 Sisi tunajivunia kitu kimoja: dhamiri yetu inatuhakikishia kwamba tumeishi ulimwenguni hapa, na hasa kati yenu, kwa unyenyekevu na unyofu tuliojaliwa na Mungu; hatukuongozwa na hekima ya kibinadamu bali neema ya Mungu.
Quant à nous, ce qui fait notre gloire, c'est le témoignage que nous rend notre conscience de nous être conduits dans le monde, et surtout à votre égard, avec la sainteté et la sincérité qui viennent de Dieu, non pas dans un esprit de sagesse charnelle, mais avec le secours de la grâce divine.
13 Tunawaandikia ninyi mambo mnayoweza kuyasoma na kuyaelewa. Ninatumaini kwamba mtaelewa vizuri kabisa,
En effet, nous ne vous écrivons pas autre chose que ce que vous lisez dans nos lettres et que vous reconnaissez vous-mêmes; et j'espère que vous le reconnaîtrez jusqu'à la fin,
14 maana mpaka sasa mmenielewa kiasi fulani tu. Tunajua kwamba katika ile Siku ya Bwana Yesu mtaweza kutuonea sisi fahari kama nasi tunavyowaonea ninyi fahari.
de même que vous l'avez déjà reconnu, en partie du moins: c'est que nous sommes votre gloire, comme vous serez aussi la nôtre au jour de notre Seigneur Jésus.
15 Nikiwa na matumaini hayo, nilikusudia kuja kwenu hapo awali ili mpate baraka maradufu.
Dans cette confiance, et afin de vous procurer une double grâce, j'avais résolu d'aller premièrement vous voir.
16 Nilikusudia kupita kwenu nikiwa safarini kwenda Makedonia, na wakati wa kurudi pia, ili nipate msaada wenu kwa safari yangu kwenda Yudea.
J'aurais passé chez vous en allant en Macédoine, puis je serais revenu de la Macédoine chez vous, d'où vous m'auriez fait conduire en Judée.
17 Je, mnadhani nilipopanga hivyo nimekuwa kama mtu asiye na msimamo? Je, mnadhani kwamba ninafanya uamuzi wangu kwa fikira za kibinadamu na kwamba nasema “Ndiyo” na “Siyo” papo hapo?
Ce dessein, l'ai-je donc formé à la légère? Ou les résolutions que je prends sont-elles prises selon la chair, de sorte qu'il y ait en moi le oui et le non?
18 Mungu ni ukweli mtupu; basi, kile tulichowaambia ninyi si jambo la “Ndiyo” na “Siyo”.
Aussi vrai que Dieu est fidèle, la parole que nous vous adressons n'est pas tantôt oui, tantôt non.
19 Maana Kristo Yesu, Mwana wa Mungu, ambaye mimi, Silwano na Timotheo, tulimhubiri kwenu, hakuwa mtu wa “Ndiyo” na “Siyo”; bali yeye daima ni “Ndiyo” ya Mungu.
Le Fils de Dieu, Jésus-Christ, que nous avons prêché parmi vous, — moi, Silvain et Timothée, — n'a pas été tout à la fois «oui et non»; mais il n'y a eu que «oui en lui».
20 Maana ndani yake ahadi zote za Mungu zimekuwa “Ndiyo”. Kwa sababu hiyo, “Amina” yetu husemwa kwa njia ya Kristo kwa ajili ya kumtukuza Mungu.
Car, de même que toutes les promesses de Dieu sont «oui en lui», c'est aussi par lui que nous disons: Amen! — à la gloire de Dieu.
21 Mungu mwenyewe ndiye mwenye kutuimarisha sisi na ninyi pia katika Kristo, na ndiye anayetuweka wakfu;
Or, celui qui nous affermit avec vous en Christ et qui nous a oints, c'est Dieu;
22 ndiye aliyetutia mhuri wa kuwa mali yake yeye na kutujalia Roho mioyoni mwetu kama dhamana ya mambo yote ambayo ametuwekea.
c'est lui aussi qui nous a marqués de son sceau, et nous a donné, dans nos coeurs, les arrhes de l'Esprit.
23 Mungu ndiye shahidi wangu—yeye anajua moyo wangu! Mimi sikuja tena Korintho, kwa sababu tu ya kuwahurumieni.
Je prends Dieu à témoin sur mon âme, que c'est par ménagement pour vous que je ne suis pas encore allé à Corinthe;
24 Hatutaki kutumia mabavu juu ya imani yenu; ninyi mko imara katika imani yenu. Wajibu wetu ni kufanya kazi pamoja kwa ajili ya furaha yenu.
non pas que nous cherchions à dominer sur votre foi, mais nous voulons contribuer à votre joie, puisque vous demeurez fermes dans la foi.