< 2 Wakorintho 1 >
1 Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Timotheo, tunawaandikia ninyi mlio kanisa la Mungu huko Korintho, na watu wote wa Mungu kila mahali katika Akaya.
Paul an apostle of Jesus Christ by the will of God, and Timothy our brother, to the church of God which is at Corinth, and all the saints that are in Achaia:
2 Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.
grace be to you, and peace from God our Father, and from the Lord Jesus Christ.
3 Atukuzwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba mwenye huruma na Mungu mwenye kuleta faraja yote.
Blessed be the God and Father of our Lord Jesus Christ, the Father of mercies, and God of all consolation; who comforteth us in all our affliction,
4 Yeye hutufariji sisi katika taabu zetu zote, ili nasi tupate kuwafariji wengine katika kila taabu kwa faraja hiyohiyo tunayopokea kutoka kwa Mungu.
that we may be able to comfort those, that are in any trouble, by the consolation wherewith we ourselves are comforted by God.
5 Naam, kadiri mateso ya Kristo yanavyozidi ndani yetu, ni kadiri hiyohiyo tunazidi kufarijiwa naye.
For as the sufferings for the sake of Christ abound on us, so our consolation by Christ doth also abound.
6 Ikiwa tunapata taabu, basi ni kwa ajili ya faraja na wokovu wenu. Tukifarijika, ni kwa ajili ya kuwafariji ninyi na kuwaunga mkono mpate nguvu ya kustahimili mateso yaleyale tunayoteseka sisi.
And whether we be afflicted, it is for your consolation and salvation, which is wrought out by the patient enduring of the same sufferings which we also suffer: or if we be comforted, it is for your consolation and salvation.
7 Tena, matumaini tuliyo nayo kwa ajili yenu ni imara; tunajua kwamba mkishiriki mateso yetu, mtashiriki pia faraja yetu.
And our hope is firm concerning you, knowing that as ye are partakers of the sufferings, so also of the consolation.
8 Ndugu, tunataka kuwajulisheni taabu zilizotupata kule Asia; taabu hizo zilitulemea kupita kiasi, hata tukakata matumaini yote ya kuendelea kuishi.
For we would not have you ignorant, brethren, concerning our affliction which befel us in Asia, that we were exceedingly pressed above our strength, so that we despaired even of life:
9 Naam, tulikuwa kama watu waliohukumiwa kuuawa, ili tufundishwe kumtegemea Mungu mwenye kuwafufua wafu, badala ya kutegemea nguvu zetu sisi wenyewe.
but we had the sentence of death within ourselves, that we might not trust in ourselves, but in God who raiseth the dead:
10 Yeye alituokoa katika hatari kubwa ya kifo, na anaendelea kutuokoa; sisi tumemwekea tumaini letu kwamba atatuokoa tena,
who delivered us from so great a death, and doth deliver, in whom we trust that He will yet deliver us:
11 ninyi mkiwa mnatuunga mkono kwa kutuombea. Hivyo neema tutakazokuwa tumepata kutokana na maombi ya watu wengi hivyo, ziwe sababu ya watu wengi zaidi kumshukuru Mungu kwa ajili yetu.
you also assisting by prayer for us, that the favor obtained for us by the prayers of many might be thankfully acknowledged by many on our account.
12 Sisi tunajivunia kitu kimoja: dhamiri yetu inatuhakikishia kwamba tumeishi ulimwenguni hapa, na hasa kati yenu, kwa unyenyekevu na unyofu tuliojaliwa na Mungu; hatukuongozwa na hekima ya kibinadamu bali neema ya Mungu.
For this is our rejoicing, the testimony of our conscience, that in simplicity and pious sincerity, not with carnal wisdom, but by the grace of God, we have had our conversation in the world, and especially towards you.
13 Tunawaandikia ninyi mambo mnayoweza kuyasoma na kuyaelewa. Ninatumaini kwamba mtaelewa vizuri kabisa,
For we write no other things to you, but what ye own and acknowledge, and I hope ye will always acknowledge.
14 maana mpaka sasa mmenielewa kiasi fulani tu. Tunajua kwamba katika ile Siku ya Bwana Yesu mtaweza kutuonea sisi fahari kama nasi tunavyowaonea ninyi fahari.
As ye have acknowledged us in part, that we are your boasting, as ye also are ours, in the day of the Lord Jesus.
15 Nikiwa na matumaini hayo, nilikusudia kuja kwenu hapo awali ili mpate baraka maradufu.
And in this confidence I had a mind to come to you first, (that ye might have a second benefit, ) and to pass by you into Macedonia;
16 Nilikusudia kupita kwenu nikiwa safarini kwenda Makedonia, na wakati wa kurudi pia, ili nipate msaada wenu kwa safari yangu kwenda Yudea.
and then to come to you again from Macedonia, and by you to be forwarded on my way to Judea.
17 Je, mnadhani nilipopanga hivyo nimekuwa kama mtu asiye na msimamo? Je, mnadhani kwamba ninafanya uamuzi wangu kwa fikira za kibinadamu na kwamba nasema “Ndiyo” na “Siyo” papo hapo?
Now when I intended this, was I chargeable with levity? or what I purpose, do I purpose from carnal motives, that with me there should be yea, yea, and then no, no?
18 Mungu ni ukweli mtupu; basi, kile tulichowaambia ninyi si jambo la “Ndiyo” na “Siyo”.
But the faithful God, He knows, that our word to you was not yes and no.
19 Maana Kristo Yesu, Mwana wa Mungu, ambaye mimi, Silwano na Timotheo, tulimhubiri kwenu, hakuwa mtu wa “Ndiyo” na “Siyo”; bali yeye daima ni “Ndiyo” ya Mungu.
For Jesus Christ the Son of God, who was preached among you by us, even by me, and Silvanus, and Timothy, was not yea and nay,
20 Maana ndani yake ahadi zote za Mungu zimekuwa “Ndiyo”. Kwa sababu hiyo, “Amina” yetu husemwa kwa njia ya Kristo kwa ajili ya kumtukuza Mungu.
but was yea in Him, (for all the promises of God are in Him yea, and in Him amen, ) to the glory of God by us:
21 Mungu mwenyewe ndiye mwenye kutuimarisha sisi na ninyi pia katika Kristo, na ndiye anayetuweka wakfu;
but He that establisheth us as well as you in Christ, and hath anointed us, is God; who hath also sealed us,
22 ndiye aliyetutia mhuri wa kuwa mali yake yeye na kutujalia Roho mioyoni mwetu kama dhamana ya mambo yote ambayo ametuwekea.
and given us the earnest of the Spirit in our hearts.
23 Mungu ndiye shahidi wangu—yeye anajua moyo wangu! Mimi sikuja tena Korintho, kwa sababu tu ya kuwahurumieni.
But I call God to witness on my soul, that to spare you I came not as yet to Corinth:
24 Hatutaki kutumia mabavu juu ya imani yenu; ninyi mko imara katika imani yenu. Wajibu wetu ni kufanya kazi pamoja kwa ajili ya furaha yenu.
not that we are lords over your faith, but are helpers of your joy: for by faith ye stand.