< 1 Timotheo 1 >

1 Mimi Paulo, mtume wa Yesu Kristo kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na Yesu Kristo tumaini letu,
Paul, an apostle of Jesus Christ, according to the appointment of God our Savior, and the Lord Jesus Christ our hope,
2 nakuandikia Timotheo mwanangu halisi katika imani. Nakutakia neema, huruma na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Kristo Yesu Bwana wetu.
to Timothy, my true son in the faith; grace, mercy, peace from God our Father, and Christ Jesus our Lord.
3 Napenda ukae huko Efeso, kama nilivyokuomba nilipokuwa ninakwenda Makedonia. Wako watu fulani huko wanaofundisha mafundisho ya uongo. Wakomeshe watu hao.
As, on going into Macedonia, I besought you to remain in Ephesus, that you might charge some that they teach no other thing,
4 Waambie waachane na zile hadithi tupu na orodha ndefu za mababu, ambazo huleta tu ubishi, wala haviwajengi watu katika mpango ujulikanao kwa imani.
nor give heed to fables and endless genealogies, which produce disputes rather than godly edification, which is in faith;
5 Shabaha ya amri hii ni kuhimiza mapendo yatokayo katika moyo safi, dhamiri njema, na imani ya kweli.
(Now the end of the commandment is love out of a pure heart, and out of a good conscience, and out of faith unfeigned:
6 Watu wengine wamepotoka na kugeukia majadiliano yasiyo na maana.
which things some not having aimed at, have turned aside to idle disputation,
7 Wanapenda kuwa walimu wa Sheria, lakini hawaelewi maneno yao wenyewe au mambo wanayosisitiza.
desiring to be teachers of law, though understanding neither what they say nor of what they boldly affirm.
8 Twajua kwamba Sheria ni njema, kama ikitumiwa ipasavyo.
But we know that the law is good, if any one use it lawfully;
9 Lakini tunapaswa kukumbuka kwamba sheria haziwekwi kwa ajili ya watu wema, bali kwa ajili ya wahalifu na wasiotii, wasiomcha Mungu na wenye dhambi, watu wasio na dini na wa kidunia. Watu wanaowaua baba na mama zao, au wauaji wowote wale;
knowing this, that law is not made for a righteous man, but for the lawless and disobedient, for the ungodly and for sinners, for the unholy and for scorners, for murderers of fathers and murderers of mothers, for man-slayers,
10 sheria imewekwa kwa ajili ya waasherati, wafiraji, wanaowaiba watu, waongo, na wanaoapa uongo au wanaofanya chochote ambacho ni kinyume cha mafundisho ya kweli.
for lewd persons, for sodomites, for men-stealers, for liars, for perjured persons, and for whatever other thing is opposed to sound teaching,
11 Mafundisho hayo hupatikana katika Habari Njema ambayo mimi nimekabidhiwa niihubiri, Habari Njema ya Mungu mtukufu na mwenye heri.
according to the glorious gospel of the blessed God, which has been intrusted to me.
12 Namshukuru Bwana wetu Yesu Kristo aliyenipa nguvu kwa ajili ya kazi yangu. Namshukuru kwa kuniona mimi kuwa ni mwaminifu, akaniteua nimtumikie,
And I thank Christ Jesus our Lord, who has given me power, because he counted me faithful, and put me into the ministry;
13 ingawa pale awali mimi nilimtukana na kumtesa na kumdhulumu. Lakini Mungu alinionea huruma, kwa sababu sikuwa na imani bado, na hivyo sikujua nilichokuwa ninafanya.
me, I say, who before was a reviler and a persecutor and an overbearing man. But I obtained mercy, because I did it ignorantly in unbelief:
14 Lakini Bwana wetu alinijalia neema yake kwa wingi, akanipa imani na upendo katika kuungana na Kristo Yesu.
and the grace of our Lord was very abundant with faith, and love which is in Christ Jesus.
15 Usemi huu ni wa kuaminika, na tena unafaa kukubaliwa kabisa: Kristo Yesu alikuja ulimwenguni kuwaokoa wenye dhambi. Nami ni mkosefu zaidi kuliko hao wote,
Assuredly true and worthy of all acceptation is this saying: that Christ Jesus came into the world to save sinners, of whom I am chief.
16 lakini Mungu alinionea huruma, ili Kristo aonyeshe uvumilivu wake wote kwangu mimi, kama mfano kwa wale wote ambao baadaye watamwamini na kupokea uzima wa milele. (aiōnios g166)
But for this reason I obtained mercy, that in me first Jesus Christ might show all long-suffering, for an example to those who might afterward believe on him in order to life eternal. (aiōnios g166)
17 Kwake yeye aliye Mfalme wa milele na asiyekufa, yeye aliye Mungu pekee—kwake viwe heshima na utukufu milele na milele! Amina. (aiōn g165)
Now to the King of the ages, the incorruptible, invisible, only wise God, be honor and glory from age to age. Amen.) (aiōn g165)
18 Mwanangu Timotheo, nakukabidhi amri hii kufuatana na maneno ya unabii yaliyosemwa zamani juu yako. Yatumie maneno hayo yawe silaha yako katika kupigana vita vizuri,
This charge I commit to you, son Timothy, in accordance with the preceding prophecies concerning you, that by them you may war the good warfare,
19 na ushike imani yako na dhamiri njema. Watu wengine hawakusikiliza dhamiri zao na hivyo wakaiharibu imani yao.
holding faith and a good conscience, which some having thrust from them, as it respects faith have made shipwreck; of whom are Hymenæus and Alexander,
20 Miongoni mwao ni Humenayo na Aleksanda ambao nimewakabidhi kwa Shetani, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.
whom I have delivered to Satan, that they may learn not to revile.

< 1 Timotheo 1 >