< 1 Timotheo 6 >
1 Watumwa wote wanapaswa kuwaheshimu wakuu wao ili kusiwe na sababu ya watu kulitukana jina la Mungu na mafundisho yetu.
Let, as many as are servants under a yoke, be counting, their own masters, worthy, of all honour, lest, the name of God and the teaching, be defamed.
2 Watumwa ambao wakuu wao ni Wakristo wasiwadharau kwani ni ndugu zao. Badala yake, wanapaswa kuwatumikia hata vizuri zaidi, maana hao wanaopata faida kutokana na kazi yao ni waumini ambao wanawapenda. Unapaswa kufundisha na kuhubiri mambo haya.
They, however, that have believing masters, let them not despise them, because they are, brethren but, the more, be doing them service, because, believing and beloved, are they who, from the good workmanship, receive advantage. These things, be teaching, and exhorting: —
3 Mtu yeyote anayefundisha kinyume cha mambo haya, na ambaye hakubaliani na maneno ya kweli ya Bwana wetu Yesu Kristo na mafundisho ya dini,
If anyone doth otherwise teach, and doth not adhere to healthful discourses—those of our Lord Jesus Christ, and to the teaching that is, according to godliness,
4 huyo amejaa majivuno na wala hajui chochote. Ni mtu wa kupenda ubishi na magombano juu ya maneno matupu, na hiyo husababisha wivu, ugomvi, matusi, shuku mbaya,
He is beclouded, knowing, nothing, rightly, but is diseased about questionings, and word-battles—out of which spring envy, strife, defamations, wicked surmising,
5 na ubishi usio na kikomo kutoka kwa watu ambao akili zao zimeharibika, na ambao hawana tena ukweli. Wanadhani dini ni njia ya kujipatia utajiri.
incessant quarrellings of men wholly corrupt in their mind and bereft of the truth, —supposing godliness to be, a means of gain!
6 Kweli dini humfanya mtu awe tajiri sana, ikiwa anatosheka na vitu alivyo navyo.
Now it is a great means of gain—godliness, with a sufficiency of one’s own;
7 Maana hatukuleta kitu chochote hapa duniani, wala hatutachukua chochote.
For, nothing, brought we into the world, neither, to take anything out, are we able; —
8 Kwa hiyo basi, kama tunacho chakula na mavazi, tunapaswa kuridhika navyo.
And, having sustenance and covering, we shall be content;
9 Lakini wale wanaotaka kutajirika huanguka katika majaribu, na kunaswa katika mtego wa tamaa nyingi mbaya za kipumbavu, ambazo huwavuta mpaka kwenye uharibifu na maangamizi.
But, they who are determined to be rich, fall into temptation, and a snare, and many foolish and hurtful covetings, the which, sink men into ruin and destruction, —
10 Kwa maana kupenda sana fedha ni chanzo cha uovu wote. Watu wengine wametamani sana kupata fedha hata wakatangatanga mbali na imani, na wameivunja mioyo yao kwa huzuni nyingi.
For, a root of all the vices, is the love of money, which, some, being eager for, have been seduced from the faith, and have pierced, themselves, about with many pangs.
11 Lakini wewe, mtu wa Mungu, jiepushe na mambo hayo. Zingatia uadilifu, uchaji wa Mungu, imani, mapendo, subira na unyenyekevu.
But, thou, O man of God! from these things, flee! and pursue righteousness, godliness, faith, love, endurance, meekness;
12 Piga mbio kadiri uwezavyo katika shindano la mbio za imani, ukajipatie tuzo la uzima wa milele, uliloitiwa wakati ulipokiri imani yako mbele ya mashahidi wengi. (aiōnios )
Be contesting the noble contest of the faith, —lay hold of the age-abiding life—unto which thou wast called, and didst make the noble confession before many witnesses. (aiōnios )
13 Mbele ya Mungu anayevipa vitu vyote uhai, na mbele ya Yesu Kristo aliyetoa ushahidi na kukiri ukweli mbele ya Pontio Pilato,
I charge thee, before God, who engendereth life in all things, and Christ Jesus, who, before Pontius Pilate, witnessed the noble confession,
14 nakuamuru ushike maagizo yako na kuyatii kwa uaminifu mpaka Siku ile atakapotokea Bwana wetu Yesu Kristo.
That thou keep the commandment without spot, free from reproach, until the forthshining of our Lord Jesus Christ—
15 Kutokea kwake kutafanyika wakati ufaao uliopangwa na Mungu mwenye heri na aliye Mtawala pekee, Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana.
Which, in its own fit times, the happy and only Potentate will shew—the King of them that reign, and Lord of them that wield lordship,
16 Yeye peke yake anaishi milele, katika mwanga usioweza kukaribiwa na mtu. Hakuna mtu aliyepata kumwona au awezaye kumwona. Kwake iwe heshima na uwezo wa milele! Amina. (aiōnios )
Who alone hath immortality, dwelling in light unapproachable, —Whom no man hath seen—nor can see: unto whom, be honour and might age-abiding. Amen. (aiōnios )
17 Waamuru watu walio matajiri katika mambo ya maisha ya sasa, wasijivune, wasiweke tumaini lao katika mali isiyoweza kutegemewa; bali wamtegemee Mungu, ambaye kwa ukarimu hutupatia vitu vyote tuvifurahie. (aiōn )
Upon them who are rich in the present age, lay thou charge—not to be high-minded, nor to have set their hope on, riches’, uncertainty, —but on God, who offereth us all things richly for enjoying, (aiōn )
18 Waamuru watende mema, wawe matajiri katika matendo mema, na wawe wakarimu na walio tayari kuwashirikisha wengine mali zao.
To be doing good, to be rich in noble works, to be, generous in giving, ready for fellowship, —
19 Kwa namna hiyo watajiwekea hazina ambayo itakuwa kwao msingi imara kwa wakati ujao. Hapo wataweza kujipatia uzima ambao ni uzima wa kweli.
Treasuring up for themselves a good foundation for the future, that they may lay hold on the life [which is life] indeed.
20 Timotheo, tunza salama yote yale uliyokabidhiwa. Jiepushe na majadiliano ya kidunia na ubishi wa kipumbavu juu ya kile wanachokiita watu wengine: “Elimu”.
O Timothy! that which hath been entrusted, do thou guard, avoiding the profane pratings and oppositions of falsely named knowledge, —
21 Maana wengine wamejidai kuwa na hiyo elimu, na matokeo yake wamepoteza imani. Nawatakieni nyote neema!
Which, some professing, concerning the faith, have missed the mark! Favour be with you.