< 1 Timotheo 6 >

1 Watumwa wote wanapaswa kuwaheshimu wakuu wao ili kusiwe na sababu ya watu kulitukana jina la Mungu na mafundisho yetu.
凡負軛為奴隸的,應認為自己的主人堪受各種尊敬,以免天主的名號和道理被人褻瀆。
2 Watumwa ambao wakuu wao ni Wakristo wasiwadharau kwani ni ndugu zao. Badala yake, wanapaswa kuwatumikia hata vizuri zaidi, maana hao wanaopata faida kutokana na kazi yao ni waumini ambao wanawapenda. Unapaswa kufundisha na kuhubiri mambo haya.
奴隸若是有信教的主人,也不可因他們是弟兄,便加以輕視,反要越發服事他們,因為得服事之惠的是信徒,是可愛的弟兄。你要拿這些事教訓人,勸勉人。
3 Mtu yeyote anayefundisha kinyume cha mambo haya, na ambaye hakubaliani na maneno ya kweli ya Bwana wetu Yesu Kristo na mafundisho ya dini,
若有人講異端道理,不順從我們的主耶穌基督的健全道理,與那合乎虔敬的教訓,
4 huyo amejaa majivuno na wala hajui chochote. Ni mtu wa kupenda ubishi na magombano juu ya maneno matupu, na hiyo husababisha wivu, ugomvi, matusi, shuku mbaya,
他必是妄自尊大,一無所知,患有辨論和舌戰之癖的人;由此而生出嫉妒、爭吵、謾罵、惡意的猜疑,
5 na ubishi usio na kikomo kutoka kwa watu ambao akili zao zimeharibika, na ambao hawana tena ukweli. Wanadhani dini ni njia ya kujipatia utajiri.
以及心思敗壞和喪失理智者的口角;他們以為虔敬是獲利之源。
6 Kweli dini humfanya mtu awe tajiri sana, ikiwa anatosheka na vitu alivyo navyo.
的確,虔敨是一種獲的富源,但應有知足的心,
7 Maana hatukuleta kitu chochote hapa duniani, wala hatutachukua chochote.
因為我們沒有帶什麼到世界上,同樣也不能帶走什麼,
8 Kwa hiyo basi, kama tunacho chakula na mavazi, tunapaswa kuridhika navyo.
只要我們有吃有穿,就當知足。
9 Lakini wale wanaotaka kutajirika huanguka katika majaribu, na kunaswa katika mtego wa tamaa nyingi mbaya za kipumbavu, ambazo huwavuta mpaka kwenye uharibifu na maangamizi.
至於那些想望致富的人,卻陷於誘感,墮入羅網和許多背理有害的慾望中,這慾望叫人沉溺於敗壞和滅亡人,
10 Kwa maana kupenda sana fedha ni chanzo cha uovu wote. Watu wengine wametamani sana kupata fedha hata wakatangatanga mbali na imani, na wameivunja mioyo yao kwa huzuni nyingi.
貪愛錢財乃萬惡的根源;有些人曾因求錢財而離棄了信德,使e 了許刺心的痛苦。
11 Lakini wewe, mtu wa Mungu, jiepushe na mambo hayo. Zingatia uadilifu, uchaji wa Mungu, imani, mapendo, subira na unyenyekevu.
至於你,天主的人哪,你要躲避這些事;但要追求正義、虔敬、信德愛德、堅忍和良善,
12 Piga mbio kadiri uwezavyo katika shindano la mbio za imani, ukajipatie tuzo la uzima wa milele, uliloitiwa wakati ulipokiri imani yako mbele ya mashahidi wengi. (aiōnios g166)
要奮力打這埸有關信仰的好仗,要爭取永生:你正是為此而蒙召,並為此在許多證人前宣示了你那美好的誓言。 (aiōnios g166)
13 Mbele ya Mungu anayevipa vitu vyote uhai, na mbele ya Yesu Kristo aliyetoa ushahidi na kukiri ukweli mbele ya Pontio Pilato,
我在使萬有有生活的天主前和曾對般雀比拉多宣過美好誓言的基督耶穌前命令你,
14 nakuamuru ushike maagizo yako na kuyatii kwa uaminifu mpaka Siku ile atakapotokea Bwana wetu Yesu Kristo.
務要保守這訓今,不受玷污,無可指摘,直到我們的主耶穌基督的顯現:
15 Kutokea kwake kutafanyika wakati ufaao uliopangwa na Mungu mwenye heri na aliye Mtawala pekee, Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana.
在預定的時期使人看見這顯現的,是那麼真福,惟一全能者,萬王之王,萬王之之主,
16 Yeye peke yake anaishi milele, katika mwanga usioweza kukaribiwa na mtu. Hakuna mtu aliyepata kumwona au awezaye kumwona. Kwake iwe heshima na uwezo wa milele! Amina. (aiōnios g166)
那獨不死不滅,住於不可接近的光中,沒有人看見過,也不能看見的天主。願尊崇和永遠的威權歸衪。亞們。 (aiōnios g166)
17 Waamuru watu walio matajiri katika mambo ya maisha ya sasa, wasijivune, wasiweke tumaini lao katika mali isiyoweza kutegemewa; bali wamtegemee Mungu, ambaye kwa ukarimu hutupatia vitu vyote tuvifurahie. (aiōn g165)
至於今世的富人,你要勸告他們,不要心高氣傲,也不要寄望於無常的財物,惟獨寄望於那將萬物豐富地供給我們享用的天主。 (aiōn g165)
18 Waamuru watende mema, wawe matajiri katika matendo mema, na wawe wakarimu na walio tayari kuwashirikisha wengine mali zao.
又要勸他們行善,在善工上致富,甘心施捨,樂意通財,
19 Kwa namna hiyo watajiwekea hazina ambayo itakuwa kwao msingi imara kwa wakati ujao. Hapo wataweza kujipatia uzima ambao ni uzima wa kweli.
為自己積蓄好的根基,以備將來能享受那真正的生命。
20 Timotheo, tunza salama yote yale uliyokabidhiwa. Jiepushe na majadiliano ya kidunia na ubishi wa kipumbavu juu ya kile wanachokiita watu wengine: “Elimu”.
弟茂德啊,要保管所受的寄托,要躲避凡俗的空談,和假冒知識之名的反論。
21 Maana wengine wamejidai kuwa na hiyo elimu, na matokeo yake wamepoteza imani. Nawatakieni nyote neema!
有些人自充有這知識,但終於失落了信德。願恩寵與你們同在!

< 1 Timotheo 6 >