< 1 Timotheo 4 >

1 Roho asema waziwazi kwamba siku za baadaye watu wengine wataitupilia mbali imani; watazitii roho danganyifu na kufuata mafundisho ya pepo.
אבל הרוח אמר בפרוש כי באחרית הימים יהיו אנשים אשר יסורו מן האמונה בפנותם אל הרוחות המטעות ואל תורת השדים׃
2 Mafundisho ya namna hiyo yanaenezwa na watu waongo wadanganyifu, ambao dhamiri zao ziko kama zimechomwa kwa chuma cha moto.
דברי שקרים בחנפה ונכוים הם במדעת׃
3 Watu hao hufundisha kwamba ni makosa kuona na pia kula vyakula fulani. Lakini Mungu aliviumba vyakula hivyo, ili wale walio waumini na ambao wanapata kuujua ukweli, wavitumie kwa shukrani.
אסרים לקחת אשה ומנעים ממיני מאכל אשר בראם האלהים שיאכלות בתודה המאמינים וידעי האמת׃
4 Kila kitu alichoumba Mungu ni chema, wala hakuna kinachohitaji kukataliwa, bali vyote vipokelewe kwa sala ya shukrani,
כי כל בריאת אלהים טובה היא ואין דבר משקץ אם יאכל בתודה׃
5 kwa sababu neno la Mungu na sala hukifanya kitu hicho kikubalike kwa Mungu.
כי יקדש בדבר אלהים ובתפלה׃
6 Kama ukiwapa ndugu wote maagizo haya, utakuwa mtumishi mwema wa Kristo Yesu, ukijiendeleza kiroho kwa maneno ya imani na mafundisho ya kweli, ambayo wewe umeyafuata.
אם תשים כזאת לפני אחיך משרת טוב תהיה לישוע המשיח מגדל בדברי האמונה ובלקח הטוב אשר דבקת אחריו׃
7 Lakini achana na hadithi zile zisizo za kidini na ambazo hazina maana. Jizoeshe kuishi maisha ya uchaji wa Mungu.
אך התרחק מהגדות פסולות ובלות והרגל עצמך בחסידות׃
8 Mazoezi ya mwili yana faida yake, lakini mazoezi ya kiroho yana faida za kila namna, maana yanatuahidia uzima katika maisha ya sasa, na pia hayo yanayokuja.
כי הרגל הגוף יועיל מעט אבל החסידות תועיל לכל דבר ויש לה הבטחת חיי העולם הזה והעולם הבא׃
9 Usemi huo ni wa kusadikika kabisa na unastahili kukubaliwa.
נאמן הדבר הזה וראוי על כל להתקבל׃
10 Sisi tunajitahidi na kufanya kazi kwa bidii kwani tumemwekea tumaini letu Mungu aliye hai ambaye ni Mwokozi wa watu wote, na hasa wale wanaoamini.
כי לזאת אנחנו גם יגעים גם נעלבים על אשר הוחלנו לאלהים חיים שהוא המושיע לכל האדם וביותר למאמינים׃
11 Wape maagizo hayo na mafundisho hayo.
את זאת תצוה ותלמד׃
12 Usikubali mtu yeyote akudharau kwa sababu wewe ni kijana, lakini jitahidi uwe mfano kwa wanaoamini: katika usemi wako, mwenendo wako, upendo, imani na maisha safi.
אל יבוז איש את בחורותיך אך היה מופת למאמינים בדבור במעשה באהבה ברוח באמונה ובטהרה׃
13 Tumia wakati wako na juhudi yako katika kusoma hadharani Maandiko Matakatifu, kuhubiri na kufundisha, mpaka nitakapokuja.
והיה שקוד לקרות ולהוכיח ולהורת עד כי אבוא׃
14 Usiache kukitumia kile kipaji cha Kristo ndani yako ulichopewa kwa maneno ya manabii na kwa kuwekewa mikono na wazee.
ואל תקל בעיניך מתנת החסד אשר בך הנתונה לך בנבואה עם סמיכת ידי הזקנים׃
15 Fikiri kwa makini juu ya hayo yote na kuyatekeleza kusudi maendeleo yako yaonekane na wote.
לאלה תשית לבך ובהם היה למען תראה הצלחתך לכל׃
16 Angalia sana mambo yako mwenyewe, na mafundisho yako. Endelea kufanya hayo maana ukifanya hivyo utajiokoa mwenyewe na wale wanaokusikiliza.
שית לבך לנפשך ולהוראה והחזק בזה כי בעשותך כן תושיע את נפשך ואת נפש השמעים אליך׃

< 1 Timotheo 4 >