< 1 Timotheo 2 >
1 Kwanza kabisa, basi naomba dua, sala, maombi na sala za shukrani zitolewe kwa Mungu kwa ajili ya watu wote,
I exhort therefore, first of all, that petitions, prayers, intercessions, and thanksgivings, be made for all people:
2 kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi maisha ya utulivu na amani pamoja na uchaji wa Mungu na mwenendo mwema.
for kings and all who are in high places; that we may lead a tranquil and quiet life in all godliness and reverence.
3 Jambo hili ni jema na lampendeza Mungu Mwokozi wetu,
For this is good and acceptable in the sight of God our Savior;
4 ambaye anataka watu wote waokolewe na wapate kuujua ukweli.
who desires all people to be saved and come to full knowledge of the truth.
5 Maana yuko Mungu mmoja, na pia yuko mmoja anayewapatanisha watu na Mungu, binadamu Kristo Yesu,
For there is one God, and one mediator between God and humanity, a human, Meshikha Yeshua,
6 ambaye alijitoa mwenyewe kuwakomboa watu wote. Huo ulikuwa uthibitisho, wakati ufaao ulipowadia.
who gave himself as a ransom for all; the testimony in its own times;
7 Kwa sababu hiyo mimi nilitumwa niwe mtume na mwalimu wa watu wa mataifa, niutangaze ujumbe wa imani na ukweli. Nasema ukweli; sisemi uongo!
to which I was appointed a preacher and an apostle (I am telling the truth, I am not lying), a teacher of the non-Jews in faith and truth.
8 Basi, popote mnapokutana kufanya ibada nataka wanaume wasali, watu waliojitolea kweli na ambao wanaweza kuinua mikono yao wakisali bila hasira wala ubishi.
I desire therefore that the men in every place pray, lifting up holy hands without anger and doubting.
9 Hali kadhalika, nawataka wanawake wawe wanyofu na wenye busara kuhusu mavazi yao; wavae sawasawa na si kwa urembo wa mitindo ya kusuka nywele, kujipamba kwa dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
In the same way, that women also adorn themselves in decent clothing, with modesty and propriety; not just with braided hair, gold, pearls, or expensive clothing;
10 bali kwa matendo mema kama iwapasavyo wanawake wamchao Mungu.
but (which becomes women professing godliness) with good works.
11 Wanawake wanapaswa kukaa kimya na kuwa wanyenyekevu wakati wa kujifunza.
Let a woman learn in quietness with all subjection.
12 Mimi simruhusu mwanamke amfundishe au amtawale mwanamume; anapaswa kukaa kimya.
But I do not permit a woman to teach, nor to exercise authority over a man, but to be in quietness.
13 Maana Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa.
For Adom was first formed, then Khawa.
14 Na wala si Adamu aliyedanganywa; bali mwanamke ndiye aliyedanganywa, akaivunja sheria ya Mungu.
Adom was not deceived, but the woman, being deceived, has fallen into disobedience;
15 Hata hivyo, mwanamke ataokolewa kwa kupata watoto, kama akidumu katika imani, upendo, utakatifu na unyofu.
but she will be delivered through the childbirth, if they continue in faith and love and holiness, with good judgment.