< 1 Wathesalonike 1 >

1 Mimi Paulo, Silwano na Timotheo tunawaandikia ninyi jumuiya ya kanisa la Thesalonike, ambao ni watu wake Mungu Baba, na wa Bwana Yesu Kristo.
[I], Paul, [am writing this letter]. Silas and Timothy [are with me]. [We(exc) are sending this letter] to [you who are] the congregation [of believers] in Thessalonica [city]. We [(inc)] all [worship] (OR, [trust in]) God [our] Father [MET] and [our] Lord Jesus Christ. [We three desire/pray that God, our Father, and Jesus Christ, our Lord, will continue to] act kindly toward you and [will continue to] cause you to have [inner] peace.
2 Tunamshukuru Mungu daima kwa ajili yenu ninyi nyote na kuwakumbukeni daima katika sala zetu.
We always thank God for you all [when] we mention you while we pray (OR, [when] we pray [for you]).
3 Maana, mbele ya Mungu Baba yetu, twakumbuka jinsi mnavyoonyesha imani yenu kwa matendo, jinsi upendo wenu unavyowawezesha kufanya kazi kwa bidii, na jinsi tumaini lenu katika Bwana wetu Yesu Kristo lilivyo thabiti.
[We thank God because] we continually remember that you work [for God because] you trust [in him] and you earnestly/energetically help people because you love them. You also endure [it when people cause you to suffer]. You endure it because you confidently expect that our Lord Jesus Christ [will soon return from heaven to rescue you]!
4 Ndugu, twajua kwamba Mungu anawapenda na kwamba amewateua muwe watu wake,
My fellow believers whom God loves, we [also thank him because] we know that he chose you [to become his people].
5 maana wakati tulipowahubirieni ile Habari Njema haikuwa kwa maneno tu, bali pia kwa nguvu na kwa Roho Mtakatifu, tukiwa na hakika kwamba ujumbe huo ulikuwa wa kweli. Mnajua jinsi tulivyoishi pamoja nanyi; tuliishi kwa manufaa yenu.
We know that he chose you because [when] we told that message to you, we did not speak only words. The Holy Spirit [helped us to speak] powerfully/effectively, and he strongly assured [us that he was powerfully working in you by means of] the message [about Christ] that we [told to you. You yourselves know that], because you know how we spoke and how we conducted ourselves when we were with you, in order that [we might help] you.
6 Ninyi mlifuata mfano wetu, na kumwiga Bwana. Ingawa mliteswa sana, mliupokea ujumbe huo kwa furaha itokayo kwa Roho Mtakatifu.
We also [know that God chose you] because we have now heard that you have endured your troubles when [people] caused you to suffer very much [because you believed in Christ]. You endured just like the Lord [Jesus Christ] endured, and just like we did [when people caused us to suffer]. At that time you were joyful because the Holy Spirit caused you to be joyful.
7 Kwa hiyo ninyi mmekuwa mfano mzuri kwa waumini wote wa Makedonia na Akaya.
As a result [of your joyfully enduring your troubles], all the believers who live in Macedonia and Achaia [provinces have heard how firmly you trust God. So they know that they should firmly trust in God] as you do.
8 Maana, kutokana na bidii yenu ujumbe wa Bwana umesikika si tu huko Makedonia na Akaya, bali imani yenu kwa Mungu imeenea popote. Tena hatuhitaji kusema zaidi.
Other people have heard you tell the message [from] the Lord [Jesus]. Then they also have proclaimed the message to people who live throughout Macedonia and Achaia [provinces]. Not only that, but [people who live] in many far-away places [HYP] have heard that you trust in God. As a result, we do not need to tell people [what God has done in your lives].
9 Watu hao wanazungumza juu ya ziara yetu kwenu: jinsi mlivyotukaribisha, jinsi mlivyoziacha sanamu mkamgeukia Mungu aliye hai na wa kweli,
People [who live far from you are telling others what happened when we were with you]. They also report that you stopped [worshipping things that] ([you/your ancestors]) [considered to be] gods and now you worship God. [As a result], you serve the God who is all-powerful and who is the real God.
10 na sasa mwamngojea Mwanae ashuke kutoka mbinguni, Yesu, ambaye Mungu alimfufua kutoka wafu, na ambaye anatuokoa katika ghadhabu ya Mungu inayokuja.
They tell us that now you wait expectantly for his Son [to return to earth] from heaven. You firmly believe that God caused him to live again after he died. You believe also that Jesus will rescue [all of] us, [who trust in him], from [God’s] punishing us [MTY].

< 1 Wathesalonike 1 >