< 1 Wathesalonike 5 >

1 Ndugu, hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya nyakati na majira yatakapotukia mambo haya.
But concerning the times and the seasons, brothers, you have no need that anything be written to you.
2 Maana ninyi wenyewe mwajua kwamba Siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajavyo usiku.
For you yourselves know well that the day of the Lord comes like a thief in the night.
3 Watu watakapokuwa wanasema: “Kila kitu ni shwari na salama” ndipo uharibifu utakapowaangukia ghafla! Mambo hayo yatatukia ghafla kama uchungu wa uzazi unavyomjia mama anayejifungua, wala watu hawataweza kuepukana nayo.
For when they are saying, “Peace and safety,” then sudden destruction will come on them, like birth pains on a pregnant woman. Then they will in no way escape.
4 Lakini ninyi ndugu, hamko gizani, na siku hiyo haipaswi kuwajieni ghafla kama vile mwizi.
But you, brothers, aren’t in darkness, that the day should overtake you like a thief.
5 Ninyi nyote ni watu mnaoishi katika mwanga, watu wa mchana. Sisi si watu wa usiku, wala wa giza.
You are all children of light and children of the day. We don’t belong to the night, nor to darkness,
6 Basi, tusilale usingizi kama wengine; tunapaswa kukesha na kuwa na kiasi.
so then let’s not sleep, as the rest do, but let’s watch and be sober.
7 Wanaolala hulala usiku, na walevi hulewa usiku.
For those who sleep, sleep in the night; and those who are drunk are drunk in the night.
8 Lakini sisi ni watu wa mchana na tunapaswa kuwa na kiasi. Tunapaswa kuvaa imani na upendo kama vazi la kujikinga kifuani, na tumaini letu la wokovu kama kofia ya chuma.
But since we belong to the day, let’s be sober, putting on the breastplate of faith and love, and for a helmet, the hope of salvation.
9 Maana Mungu hakututeua ili tuangamizwe na ghadhabu yake, bali tuupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
For God didn’t appoint us to wrath, but to the obtaining of salvation through our Lord Jesus Christ,
10 ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, iwe tu hai au tumekufa.
who died for us, that, whether we wake or sleep, we should live together with him.
11 Kwa hiyo farijianeni na kusaidiana ninyi kwa ninyi kama mnavyofanya sasa.
Therefore exhort one another, and build each other up, even as you also do.
12 Ndugu, tunawaombeni muwastahi wale wanaofanya kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwafundisheni kuhusu maisha ya Kikristo.
But we beg you, brothers, to know those who labour amongst you, and are over you in the Lord and admonish you,
13 Wapeni heshima kubwa na kuwapenda kwa sababu ya kazi wanayofanya. Muwe na amani kati yenu.
and to respect and honour them in love for their work’s sake. Be at peace amongst yourselves.
14 Ndugu, tunawahimizeni muwaonye watu walio wavivu, muwatie moyo watu wanyonge, muwasaidie watu dhaifu, muwe na subira kwa wote.
We exhort you, brothers: Admonish the disorderly; encourage the faint-hearted; support the weak; be patient towards all.
15 Angalieni mtu yeyote asimlipe mwingine maovu kwa maovu, ila nia yenu iwe kutendeana mema daima na kuwatendea mema watu wote.
See that no one returns evil for evil to anyone, but always follow after that which is good for one another and for all.
16 Furahini daima,
Always rejoice.
17 salini kila wakati
Pray without ceasing.
18 na muwe na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.
In everything give thanks, for this is the will of God in Christ Jesus towards you.
19 Msimpinge Roho Mtakatifu;
Don’t quench the Spirit.
20 msidharau unabii.
Don’t despise prophecies.
21 Pimeni kila kitu: zingatieni kilicho chema,
Test all things, and hold firmly that which is good.
22 na epukeni kila aina ya uovu.
Abstain from every form of evil.
23 Mungu anayetupatia amani awafanye ninyi watakatifu kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu—roho, mioyo na miili yenu—mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
May the God of peace himself sanctify you completely. May your whole spirit, soul, and body be preserved blameless at the coming of our Lord Jesus Christ.
24 Yeye anayewaita ninyi atafanya hivyo kwani ni mwaminifu.
He who calls you is faithful, who will also do it.
25 Ndugu, tuombeeni na sisi pia.
Brothers, pray for us.
26 Wasalimuni ndugu wote kwa ishara ya upendo.
Greet all the brothers with a holy kiss.
27 Nawahimizeni kwa jina la Bwana muwasomee ndugu zetu wote barua hii.
I solemnly command you by the Lord that this letter be read to all the holy brothers.
28 Tunawatakieni neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.
The grace of our Lord Jesus Christ be with you. Amen.

< 1 Wathesalonike 5 >