< 1 Wathesalonike 5 >

1 Ndugu, hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya nyakati na majira yatakapotukia mambo haya.
Now concerning the times and the seasons, brothers, you do not need to be written to,
2 Maana ninyi wenyewe mwajua kwamba Siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajavyo usiku.
for you yourselves know very well that the Day of the Lord comes just like a thief in the night.
3 Watu watakapokuwa wanasema: “Kila kitu ni shwari na salama” ndipo uharibifu utakapowaangukia ghafla! Mambo hayo yatatukia ghafla kama uchungu wa uzazi unavyomjia mama anayejifungua, wala watu hawataweza kuepukana nayo.
For whenever they say, “Peace and safety!” then sudden destruction is standing near them, like labor pains to a pregnant woman, and they will not escape.
4 Lakini ninyi ndugu, hamko gizani, na siku hiyo haipaswi kuwajieni ghafla kama vile mwizi.
But you, brothers, are not in darkness so that this Day should come upon you like a thief.
5 Ninyi nyote ni watu mnaoishi katika mwanga, watu wa mchana. Sisi si watu wa usiku, wala wa giza.
You are all sons of light and sons of day; we are not of night, nor of darkness.
6 Basi, tusilale usingizi kama wengine; tunapaswa kukesha na kuwa na kiasi.
So then, let us not sleep, like the rest, but let us stay alert and sober;
7 Wanaolala hulala usiku, na walevi hulewa usiku.
because those who sleep, sleep at night, and those who get drunk, get drunk at night;
8 Lakini sisi ni watu wa mchana na tunapaswa kuwa na kiasi. Tunapaswa kuvaa imani na upendo kama vazi la kujikinga kifuani, na tumaini letu la wokovu kama kofia ya chuma.
but we being of day, let us be sober, putting on a breastplate of faith and love, and a helmet of hope of salvation.
9 Maana Mungu hakututeua ili tuangamizwe na ghadhabu yake, bali tuupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
For God did not appoint us to undergo wrath but to obtain salvation through our Lord Jesus Christ,
10 ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, iwe tu hai au tumekufa.
who died for us so that whether awake or asleep we may live together with Him.
11 Kwa hiyo farijianeni na kusaidiana ninyi kwa ninyi kama mnavyofanya sasa.
Therefore encourage one another and build each other up, as in fact you do.
12 Ndugu, tunawaombeni muwastahi wale wanaofanya kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwafundisheni kuhusu maisha ya Kikristo.
Now we urge you, brothers, to recognize those who labor among you and are over you in the Lord and admonish you,
13 Wapeni heshima kubwa na kuwapenda kwa sababu ya kazi wanayofanya. Muwe na amani kati yenu.
and to esteem them very highly in love because of their work. Be at peace among yourselves.
14 Ndugu, tunawahimizeni muwaonye watu walio wavivu, muwatie moyo watu wanyonge, muwasaidie watu dhaifu, muwe na subira kwa wote.
Now we exhort you, brothers: admonish the disorderly, encourage the fainthearted, be supportive of the weak, be patient toward all.
15 Angalieni mtu yeyote asimlipe mwingine maovu kwa maovu, ila nia yenu iwe kutendeana mema daima na kuwatendea mema watu wote.
See that no one pays back bad for bad to anyone, but always pursue the good, both for one another and for all.
16 Furahini daima,
Rejoice always!
17 salini kila wakati
Pray continually!
18 na muwe na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.
Give thanks in everything, for this is God's will for you in Christ Jesus.
19 Msimpinge Roho Mtakatifu;
Do not quench the Spirit!
20 msidharau unabii.
Do not disdain prophesies,
21 Pimeni kila kitu: zingatieni kilicho chema,
but test everything; hold on to the good.
22 na epukeni kila aina ya uovu.
Keep away from every form of evil!
23 Mungu anayetupatia amani awafanye ninyi watakatifu kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu—roho, mioyo na miili yenu—mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
Now may the God of peace Himself sanctify you completely, and may your whole spirit and soul and body be preserved blameless at the coming of our Lord Jesus Christ.
24 Yeye anayewaita ninyi atafanya hivyo kwani ni mwaminifu.
He who calls you is faithful, and He will do it.
25 Ndugu, tuombeeni na sisi pia.
Brothers, pray for us.
26 Wasalimuni ndugu wote kwa ishara ya upendo.
Greet all the brothers with a holy kiss.
27 Nawahimizeni kwa jina la Bwana muwasomee ndugu zetu wote barua hii.
I adjure you by the Lord that this letter be read to all the holy brothers.
28 Tunawatakieni neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.
The grace of our Lord Jesus Christ be with you. Amen.

< 1 Wathesalonike 5 >