< 1 Wathesalonike 5 >

1 Ndugu, hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya nyakati na majira yatakapotukia mambo haya.
But of the times and moments, brethren, you need not, that we should write to you;
2 Maana ninyi wenyewe mwajua kwamba Siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajavyo usiku.
For yourselves know perfectly, that the day of the Lord shall so come, as a thief in the night.
3 Watu watakapokuwa wanasema: “Kila kitu ni shwari na salama” ndipo uharibifu utakapowaangukia ghafla! Mambo hayo yatatukia ghafla kama uchungu wa uzazi unavyomjia mama anayejifungua, wala watu hawataweza kuepukana nayo.
For when they shall say, peace and security; then shall sudden destruction come upon them, as the pains upon her that is with child, and they shall not escape.
4 Lakini ninyi ndugu, hamko gizani, na siku hiyo haipaswi kuwajieni ghafla kama vile mwizi.
But you, brethren, are not in darkness, that that day should overtake you as a thief.
5 Ninyi nyote ni watu mnaoishi katika mwanga, watu wa mchana. Sisi si watu wa usiku, wala wa giza.
For all you are the children of light, and children of the day: we are not of the night, nor of darkness.
6 Basi, tusilale usingizi kama wengine; tunapaswa kukesha na kuwa na kiasi.
Therefore, let us not sleep, as others do; but let us watch, and be sober.
7 Wanaolala hulala usiku, na walevi hulewa usiku.
For they that sleep, sleep in the night; and they that are drunk, are drunk in the night.
8 Lakini sisi ni watu wa mchana na tunapaswa kuwa na kiasi. Tunapaswa kuvaa imani na upendo kama vazi la kujikinga kifuani, na tumaini letu la wokovu kama kofia ya chuma.
But let us, who are of the day, be sober, having on the breastplate of faith and charity, and for a helmet the hope of salvation.
9 Maana Mungu hakututeua ili tuangamizwe na ghadhabu yake, bali tuupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
For God hath not appointed us unto wrath, but unto the purchasing of salvation by our Lord Jesus Christ,
10 ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, iwe tu hai au tumekufa.
Who died for us; that, whether we watch or sleep, we may live together with him.
11 Kwa hiyo farijianeni na kusaidiana ninyi kwa ninyi kama mnavyofanya sasa.
For which cause comfort one another; and edify one another, as you also do.
12 Ndugu, tunawaombeni muwastahi wale wanaofanya kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwafundisheni kuhusu maisha ya Kikristo.
And we beseech you, brethren, to know them who labour among you, and are over you in the Lord, and admonish you:
13 Wapeni heshima kubwa na kuwapenda kwa sababu ya kazi wanayofanya. Muwe na amani kati yenu.
That you esteem them more abundantly in charity, for their work’s sake. Have peace with them.
14 Ndugu, tunawahimizeni muwaonye watu walio wavivu, muwatie moyo watu wanyonge, muwasaidie watu dhaifu, muwe na subira kwa wote.
And we beseech you, brethren, rebuke the unquiet, comfort the feeble minded, support the weak, be patient towards all men.
15 Angalieni mtu yeyote asimlipe mwingine maovu kwa maovu, ila nia yenu iwe kutendeana mema daima na kuwatendea mema watu wote.
See that none render evil for evil to any man; but ever follow that which is good towards each other, and towards all men.
16 Furahini daima,
Always rejoice.
17 salini kila wakati
Pray without ceasing.
18 na muwe na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.
In all things give thanks; for this is the will of God in Christ Jesus concerning you all.
19 Msimpinge Roho Mtakatifu;
Extinguish not the spirit.
20 msidharau unabii.
Despise not prophecies.
21 Pimeni kila kitu: zingatieni kilicho chema,
But prove all things; hold fast that which is good.
22 na epukeni kila aina ya uovu.
From all appearance of evil refrain yourselves.
23 Mungu anayetupatia amani awafanye ninyi watakatifu kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu—roho, mioyo na miili yenu—mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
And may the God of peace himself sanctify you in all things; that your whole spirit, and soul, and body, may be preserved blameless in the coming of our Lord Jesus Christ.
24 Yeye anayewaita ninyi atafanya hivyo kwani ni mwaminifu.
He is faithful who hath called you, who also will do it.
25 Ndugu, tuombeeni na sisi pia.
Brethren, pray for us.
26 Wasalimuni ndugu wote kwa ishara ya upendo.
Salute all the brethren with a holy kiss.
27 Nawahimizeni kwa jina la Bwana muwasomee ndugu zetu wote barua hii.
I charge you by the Lord, that this epistle be read to all the holy brethren.
28 Tunawatakieni neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.
The grace of our Lord Jesus Christ be with you. Amen.

< 1 Wathesalonike 5 >