< 1 Wathesalonike 5 >
1 Ndugu, hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya nyakati na majira yatakapotukia mambo haya.
But, brethren, you have no need that I write to you of the times and seasons;
2 Maana ninyi wenyewe mwajua kwamba Siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajavyo usiku.
for you yourselves know perfectly that the day of the Lord so comes as a thief in the night:
3 Watu watakapokuwa wanasema: “Kila kitu ni shwari na salama” ndipo uharibifu utakapowaangukia ghafla! Mambo hayo yatatukia ghafla kama uchungu wa uzazi unavyomjia mama anayejifungua, wala watu hawataweza kuepukana nayo.
for when they shall say, Peace and safety, then sudden destruction comes upon them, as the pains of birth upon a woman with child, and they shall not escape.
4 Lakini ninyi ndugu, hamko gizani, na siku hiyo haipaswi kuwajieni ghafla kama vile mwizi.
But you, brethren, are not in darkness, that that day should overtake you as a thief.
5 Ninyi nyote ni watu mnaoishi katika mwanga, watu wa mchana. Sisi si watu wa usiku, wala wa giza.
You are all sons of light, and sons of day: we are not of night, nor of darkness.
6 Basi, tusilale usingizi kama wengine; tunapaswa kukesha na kuwa na kiasi.
Therefore, let us not sleep, as do others, but let us watch and be sober.
7 Wanaolala hulala usiku, na walevi hulewa usiku.
For those who sleep, sleep in the night; and those who are drunken, are drunken in the night.
8 Lakini sisi ni watu wa mchana na tunapaswa kuwa na kiasi. Tunapaswa kuvaa imani na upendo kama vazi la kujikinga kifuani, na tumaini letu la wokovu kama kofia ya chuma.
But let us, who are of the day, be sober, having on the breastplate of faith and love, and for a helmet, the hope of salvation:
9 Maana Mungu hakututeua ili tuangamizwe na ghadhabu yake, bali tuupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
for God has not appointed us to wrath, but to the obtaining of salvation through our Lord Jesus Christ,
10 ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, iwe tu hai au tumekufa.
who died for us, that, whether we wake or sleep, we might live together with him.
11 Kwa hiyo farijianeni na kusaidiana ninyi kwa ninyi kama mnavyofanya sasa.
Wherefore, exhort one another, and edify one another, as you also do.
12 Ndugu, tunawaombeni muwastahi wale wanaofanya kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwafundisheni kuhusu maisha ya Kikristo.
Now we beseech you, brethren, to have regard for those who labor among you, and preside over you in the Lord, and admonish you,
13 Wapeni heshima kubwa na kuwapenda kwa sababu ya kazi wanayofanya. Muwe na amani kati yenu.
and that you esteem them very highly in love on account of their work. Be at peace among yourselves.
14 Ndugu, tunawahimizeni muwaonye watu walio wavivu, muwatie moyo watu wanyonge, muwasaidie watu dhaifu, muwe na subira kwa wote.
We exhort you, brethren, admonish the unruly, comfort the faint-hearted, earnestly care for the weak-minded, be of a long-suffering disposition toward all.
15 Angalieni mtu yeyote asimlipe mwingine maovu kwa maovu, ila nia yenu iwe kutendeana mema daima na kuwatendea mema watu wote.
See that no one render evil for evil to any, but always pursue that which is good toward one another and toward all.
18 na muwe na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.
in every thing give thanks; for this is the will of God in Christ Jesus concerning you.
19 Msimpinge Roho Mtakatifu;
Quench not the Spirit.
Despise not prophesyings.
21 Pimeni kila kitu: zingatieni kilicho chema,
Prove all things; hold fast that which is good.
22 na epukeni kila aina ya uovu.
Abstain from every appearance of evil.
23 Mungu anayetupatia amani awafanye ninyi watakatifu kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu—roho, mioyo na miili yenu—mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
Now the God of peace himself sanctify you wholly; and may your whole spirit and soul and body be preserved blameless at the coming of our Lord Jesus Christ.
24 Yeye anayewaita ninyi atafanya hivyo kwani ni mwaminifu.
Faithful is he that calls you; and he will do what he has promised.
25 Ndugu, tuombeeni na sisi pia.
Brethren, pray for us.
26 Wasalimuni ndugu wote kwa ishara ya upendo.
Salute all the brethren with a holy kiss.
27 Nawahimizeni kwa jina la Bwana muwasomee ndugu zetu wote barua hii.
I adjure you by the Lord, that this letter be read to all the holy brethren.
28 Tunawatakieni neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.
The grace of our Lord Jesus Christ be with you.