< 1 Wathesalonike 3 >

1 Mwishowe hatukuweza kuvumilia zaidi. Basi, tuliamua kubaki kule Athene peke yetu,
C’est pourquoi ne supportant pas un plus long délai, nous préférâmes demeurer seuls à Athènes,
2 na kumtuma kwenu ndugu yetu Timotheo, ambaye ni mfanyakazi mwenzetu kwa ajili ya Mungu katika kuhubiri Habari Njema ya Kristo. Tulimtuma ili awaimarisheni na kuwafarijini,
Et nous envoyâmes Timothée, notre frère, et ministre de Dieu dans l’Evangile du Christ, pour vous affermir et vous encourager dans votre foi;
3 kusudi imani ya mtu yeyote miongoni mwenu isije ikafifia kwa sababu ya taabu hizo. Ninyi mnajua kwamba tunapaswa kupata mateso.
Afin que personne ne fût ébranlé dans ces tribulations; car vous savez vous-mêmes que c’est à cela que nous sommes destinés.
4 Maana, tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwaambieni kwamba tutateswa; na kama mjuavyo ndivyo ilivyotukia.
Et lors même que nous étions près de vous, nous vous prédisions que nous aurions à souffrir des tribulations; ce qui est arrivé, en effet, comme vous le savez.
5 Ndio maana nilimtuma Timotheo kwenu. Sikuweza kungoja zaidi, na hivyo nilimtuma nipate habari za imani yenu. Isije ikawa labda Mshawishi aliwajaribuni na kazi yote tuliyofanya miongoni mwenu imepotea bure!
Pour moi donc, ne supportant pas un plus long délai, j’envoyai pour connaître votre foi, de peur que celui qui tente ne vous eût tentés, et que notre travail ne devînt inutile.
6 Sasa Timotheo amekwisha rudi, naye ametupa habari za kufurahisha kuhusu imani na upendo wenu. Ametuarifu kwamba mnatukumbuka daima, na kwamba mna hamu ya kutuona sisi kama nasi tulivyo na hamu ya kuwaoneni.
Mais maintenant Timothée étant revenu d’auprès de vous vers nous, et nous ayant annoncé votre foi, votre charité, et que vous avez toujours un bon souvenir de nous, désirant nous voir, comme nous le désirons nous-mêmes,
7 Basi, habari za imani yenu zimetutia moyo katika taabu na mateso yetu yote,
Nous avons été ainsi consolés en vous par votre foi au milieu de toutes nos peines et de toutes nos tribulations.
8 kwani sasa tunaishi kweli ikiwa ninyi mnasimama imara katika kuungana na Bwana.
Car maintenant nous vivons, si vous demeurez fermes dans le Seigneur.
9 Sasa twaweza kumshukuru Mungu wetu kwa ajili yenu. Tunamshukuru kwa furaha tuliyo nayo mbele yake kwa sababu yenu.
Et quelles actions de grâces pourrions-nous rendre à Dieu pour toute la joie dont nous nous réjouissons devant notre Dieu à cause de vous,
10 Tunazidi kumwomba Mungu usiku na mchana kwa moyo wetu wote ili atupatie fursa ya kuwaoneni uso kwa uso ili tuweze kurekebisha chochote kilichopungua katika imani yenu.
Demandant avec instance nuit et jour de voir votre face, et de compléter ce qui manque à votre foi?
11 Tunamwomba Mungu, Baba yetu mwenyewe, na Bwana wetu Yesu atutayarishie njia ya kuja kwenu.
Que ce même Dieu donc, notre Père, et Notre Seigneur Jésus-Christ dirige notre voie vers vous.
12 Bwana awawezeshe ninyi kupendana na kuwapenda watu wote zaidi na zaidi, kama vile sisi tunavyowapenda ninyi.
Et que le Seigneur vous multiplie, et fasse abonder la charité que vous avez les uns envers les autres et envers tous, comme la nôtre abonde envers vous;
13 Hivyo ataiimarisha mioyo yenu, nanyi mtakuwa wakamilifu na watakatifu mbele ya Mungu na Baba yetu wakati Bwana wetu Yesu atakapokuja pamoja na wote walio wake.
Pour fortifier vos cœurs sans reproche en sainteté, devant notre Dieu et Père, à l’avènement de Notre Seigneur Jésus-Christ avec tous ses saints. Amen.

< 1 Wathesalonike 3 >