< 1 Wathesalonike 2 >
1 Ndugu, ninyi wenyewe mnafahamu kwamba ziara yetu kwenu haikuwa bure.
For you yourselves know, brethren, our entrance among you, that it was not in vain.
2 Mnajua jinsi tulivyodhulumiwa na kutukanwa kule Filipi kabla ya kufika kwenu Thesalonike. Ingawa kulikuwa na upinzani mwingi, Mungu wetu alitujalia uhodari wa kuwahubirieni Habari Njema yake.
But having suffered before, and having been outraged, as you know, in Philippi, we were bold in our God to speak to you the gospel of God in the midst of great peril.
3 Jambo tunalosisitiza kwenu si jambo linalotegemea uongo au nia mbaya; wala hatupendi kumdanganya mtu yeyote.
For our exhortation arose not from deception, nor from uncleanness, nor was it with guile;
4 Sisi twanena daima kama atakavyo Mungu kwani yeye alituona kwamba tunafaa, akatukabidhi hii Habari Njema. Si nia yetu kuwapendeza watu hata kidogo, bali twataka kumpendeza Mungu ambaye anajua mioyo yetu mpaka ndani.
but as God had judged us worthy to be intrusted with the gospel, so we speak, not as pleasing men, but God, who tries our hearts.
5 Ninyi mnajua kwamba sisi hatukuja kwenu na maneno matamu ya kubembeleza wala hatukutumia maneno ya kijanja ya kuficha ubinafsi fulani; Mungu ni shahidi!
For neither nattering words did we at any time use, as you know, nor a pretext for covetousness; God is witness:
6 Hatukutafuta sifa kutoka kwa watu, wala kutoka kwenu, wala kutoka kwa mtu yeyote,
nor did we seek glory from men, neither from you nor from others; though we could have been burdensome as the apostles of Christ.
7 ingawa sisi tukiwa mitume wa Kristo, tungeweza kudai mambo fulani kwenu. Lakini sisi tulikuwa Wapole kati yenu kama alivyo mama kwa watoto wake.
But we were gentle among you. As a nurse nourishes her children,
8 Tuliwapenda ninyi sana hata tukawa tayari kuwashirikisha si tu Habari Njema ya Mungu, bali pia na maisha yetu. Ndivyo mlivyokuwa wapenzi wetu!
so, having a strong affection for you, we were well pleased to impart to you not only the gospel of God, but our own lives also, because you had become dear to us.
9 Ndugu, mnakumbuka jinsi tulivyofanya kazi na kutaabika. Tulipowaleteeni Habari Njema ya Mungu tulifanya kazi mchana na usiku kusudi tusiwe mzigo kwa mtu yeyote miongoni mwenu.
For you remember, brethren, our labor and toil; for, laboring night and day, that we might not be burdensome to any one of you, we preached to you the gospel of God.
10 Ninyi mnaweza kushuhudia, na Mungu pia ni shahidi, jinsi mwenendo wetu kati yenu ninyi mnaoamini ulivyokuwa mzuri, mwadilifu na usio na lawama.
You are witnesses, and God also, in how holy and just and blameless a manner we conducted ourselves among you that believe,
11 Mnajua kwamba sisi tulimtendea kila mmoja wenu kama vile baba anavyowatendea watoto wake mwenyewe.
as indeed you know how we exhorted and comforted and charged every one of you, as a father his children,
12 Tuliwapeni moyo, tuliwafarijini na kuwahimiza ili mpate kuishi maisha yampendezayo Mungu ambaye aliwaiteni mshiriki Utawala na utukufu wake.
that you should walk in a manner worthy of God, who has called you to his own kingdom and glory.
13 Tena tunayo sababu nyingine ya kumshukuru Mungu: tulipowaleteeni ujumbe wa Mungu, ninyi mliusikia mkaupokea, si kama vile ujumbe wa binadamu, bali kama ujumbe wa Mungu, na kweli ndivyo ulivyo. Maana Mungu anafanya kazi ndani yenu ninyi mnaoamini.
For this reason, also, we thank God without ceasing; because, when you received the word of God, as preached by us, you embraced it, not as the word of men, but, as it is in truth, the word of God, which effectually works in you that believe.
14 Ndugu, ninyi mmepatwa na mambo yaleyale yaliyoyapata makanisa ya Mungu kule Yudea, mambo yaliyowapata watu walio wake Kristo Yesu. Ninyi mlidhulumiwa na wananchi wenzenu kama vile wao walivyodhulumiwa na wenzao Wayahudi,
For you, brethren, became imitators of the churches of God in Judea which are in Christ Jesus; for you, also, have suffered the same things from your own countrymen, that they have suffered from the Jews,
15 ambao walimuua Bwana Yesu na manabii, wakatutesa na sisi pia. Watu hao wanamchukiza Mungu, tena ni adui za kila mtu!
who both killed the Lord Jesus and the prophets, and have persecuted us, and do not please God, and are opposed to all men,
16 Hata walijaribu kutuzuia kuwahubiria watu wa mataifa mengine ujumbe utakaowaletea wokovu. Ndivyo walivyokamilisha orodha ya dhambi zote walizotenda siku zote. Lakini sasa hasira ya Mungu imewaangukia.
forbidding us to speak to the Gentiles that they may be saved, in order that they may fill up their sins at all times: but the wrath is coming upon them to the full.
17 Ndugu, kuachana kwetu nanyi kulikuwa kwa muda tu, tena kuachana huko kulikuwa kwa mwili tu na si kwa roho. Kitambo kifupi baadaye, tulishikwa na hamu kubwa ya kuwaoneni tena!
But we, brethren, having been taken from you for a short time, in person, not in heart, did, with great desire, endeavor the more earnestly to see your face.
18 Kwa hiyo tuliamua kuwatembeleeni tena. Nami, Paulo, nilijaribu kuja kwenu zaidi ya mara moja, lakini Shetani alituzuia.
For this reason, we intended to go to you, (I Paul) both once and again, but Satan hindered us.
19 Je, tutakaposimama mbele ya Bwana Yesu wakati atakapokuja, fahari ya ushindi wetu itakuwa nini? Itakuwa ni ninyi wenyewe; ninyi ndio tumaini letu na furaha yetu.
For what is our hope, or joy, or crown of rejoicing? Are not even you, in the presence of our Lord Jesus Christ at his coming?
20 Naam, ninyi ni utukufu wetu na furaha yetu!
You indeed are our glory and joy.