< 1 Wathesalonike 1 >

1 Mimi Paulo, Silwano na Timotheo tunawaandikia ninyi jumuiya ya kanisa la Thesalonike, ambao ni watu wake Mungu Baba, na wa Bwana Yesu Kristo.
Paul, Silvanus, and Timothy, to the church of the Thessalonians in God the Father and the Lord Jesus Christ: Grace to you and peace from God our Father and the Lord Jesus Christ.
2 Tunamshukuru Mungu daima kwa ajili yenu ninyi nyote na kuwakumbukeni daima katika sala zetu.
We always give thanks to God for you all, making mention of you in our prayers,
3 Maana, mbele ya Mungu Baba yetu, twakumbuka jinsi mnavyoonyesha imani yenu kwa matendo, jinsi upendo wenu unavyowawezesha kufanya kazi kwa bidii, na jinsi tumaini lenu katika Bwana wetu Yesu Kristo lilivyo thabiti.
remembering without ceasing, in the presence of our God and Father, your work of faith, your labor of love, and your endurance of hope in our Lord Jesus Christ.
4 Ndugu, twajua kwamba Mungu anawapenda na kwamba amewateua muwe watu wake,
For we know, brothers beloved by God, that you have been chosen,
5 maana wakati tulipowahubirieni ile Habari Njema haikuwa kwa maneno tu, bali pia kwa nguvu na kwa Roho Mtakatifu, tukiwa na hakika kwamba ujumbe huo ulikuwa wa kweli. Mnajua jinsi tulivyoishi pamoja nanyi; tuliishi kwa manufaa yenu.
because our gospel did not come to you in word only, but also in power and in the Holy Spirit and with much conviction. You know what sort of men we proved to be among you for your sake.
6 Ninyi mlifuata mfano wetu, na kumwiga Bwana. Ingawa mliteswa sana, mliupokea ujumbe huo kwa furaha itokayo kwa Roho Mtakatifu.
And you became imitators of us and of the Lord when you received the word in much affliction with the joy of the Holy Spirit.
7 Kwa hiyo ninyi mmekuwa mfano mzuri kwa waumini wote wa Makedonia na Akaya.
As a result you have become examples to all the believers in Macedonia and Achaia.
8 Maana, kutokana na bidii yenu ujumbe wa Bwana umesikika si tu huko Makedonia na Akaya, bali imani yenu kwa Mungu imeenea popote. Tena hatuhitaji kusema zaidi.
For not only has the word of the Lord sounded forth from you in Macedonia and Achaia, but reports of your faith in God have gone out everywhere, so that we have no need to say anything about it.
9 Watu hao wanazungumza juu ya ziara yetu kwenu: jinsi mlivyotukaribisha, jinsi mlivyoziacha sanamu mkamgeukia Mungu aliye hai na wa kweli,
For the people themselves report what kind of reception we had among you, and how you turned away from idols to serve the living and true God,
10 na sasa mwamngojea Mwanae ashuke kutoka mbinguni, Yesu, ambaye Mungu alimfufua kutoka wafu, na ambaye anatuokoa katika ghadhabu ya Mungu inayokuja.
as you wait for his Son Jesus to return from heaven, whom God raised from the dead, and who rescues us from the coming wrath.

< 1 Wathesalonike 1 >