< 1 Petro 1 >

1 Mimi Petro, mtume wa Yesu Kristo nawaandikia ninyi wateule wa Mungu Baba, ambao mmetawanyika na mnaishi kama wakimbizi huko Ponto, Galatia, Kapadokia, Asia na Bithunia.
Peter, an apostle of Jesus Christ, to the strangers scattered through Pontus, Galatia, Cappadocia, Asia, and Bithynia,
2 Mungu Baba aliwateua ninyi kufuatana na kusudi lake, na mmefanywa watakatifu na Roho, mpate kumtii Yesu Kristo na kusafishwa kwa damu yake. Nawatakieni neema na amani tele.
chosen according to the foreknowledge of God the Father, in sanctification of the Spirit, unto obedience and sprinkling of the blood of Jesus Christ: Grace and peace be multiplied to you.
3 Asifiwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa huruma yake kuu alitufanya tuzaliwe upya kwa kumfufua Yesu kutoka wafu. Ametujalia tumaini lenye uzima,
Blessed be God, the Father of our Lord Jesus Christ, who, according to his abundant mercy, begot us again into a living hope through the resurrection of Jesus Christ from the dead,
4 na hivyo tunatazamia kupata baraka zile ambazo Mungu aliwawekea watu wake. Mungu amewawekeeni baraka hizo mbinguni ambako haziwezi kuoza au kuharibika au kufifia.
to an inheritance imperishable, and undefiled, and unfading, reserved in heaven for you,
5 Hizo zitakuwa zenu ninyi ambao kwa imani mnalindwa salama kwa nguvu ya Mungu kwa ajili ya wokovu ambao uko tayari kufunuliwa mwishoni mwa nyakati.
who are guarded by the power of God through faith unto a salvation ready to be revealed in the last time;
6 Furahini kuhusu jambo hilo, ijapokuwa sasa, kwa kitambo kidogo, itawabidi kuhuzunika kwa sababu ya majaribio mbalimbali mnayoteseka.
wherein ye greatly rejoice, though now for a short time, if need be, made sorrowful by manifold trials,
7 Shabaha yake ni kuthibitisha imani yenu. Hata dhahabu yenyewe ambayo huharibika, hujaribiwa kwa moto; hali kadhalika na imani yenu ambayo ni ya thamani zaidi kuliko dhahabu, ni lazima ijaribiwe ipate kuwa thabiti. Hapo mtapokea sifa na utukufu na heshima Siku ile Yesu Kristo atakapofunuliwa.
that the proof of your faith, much more precious than gold which perisheth, but is tried with fire, may be found unto praise and glory and honor at the manifestation of Jesus Christ;
8 Ninyi mnampenda ingawaje hamjamwona, na mnamwamini ingawa hamumwoni sasa. Hivyo, mnafurahi kwa furaha tukufu isiyoelezeka,
whom, having not seen, ye love; in whom, though now ye see him not, yet believing, ye rejoice with joy unspeakable and full of glory,
9 kwa sababu mnapokea wokovu wa roho zenu ambao ni lengo la imani yenu.
receiving the end of your faith, the salvation of your souls.
10 Manabii walipeleleza kwa makini na kufanya uchunguzi juu ya wokovu huo, wakabashiri juu ya neema hiyo ambayo ninyi mngepewa.
Concerning which salvation the prophets sought earnestly and searched earnestly, who prophesied of the grace that was to come to you;
11 Walijaribu kujua nyakati na mazingira ya tukio hilo, yaani wakati alioudokezea Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao, akibashiri juu ya mateso yatakayompata Kristo na utukufu utakaofuata.
searching what or what manner of time the Spirit of Christ which was in them signified, when it testified beforehand the sufferings to come upon Christ, and the glories that were to follow;
12 Mungu aliwafunulia kwamba wakati walipokuwa wanasema juu ya hayo mambo ambayo ninyi mmekwisha sikia sasa kutoka kwa wale wajumbe waliowatangazieni Habari Njema kwa nguvu ya Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni, hiyo kazi yao haikuwa kwa faida yao wenyewe, bali kwa ajili yenu. Hayo ndiyo mambo ambayo hata malaika wangependa kuyafahamu.
to whom it was revealed, that not to themselves, but to you, they were ministering the things, which have now been announced to you by them that have brought the glad tidings to you by the Holy Spirit sent down from heaven; which things angels desire to look into.
13 Kwa hiyo, basi, muwe tayari kabisa kwa nia, na kukesha. Wekeni tumaini lenu lote katika baraka ile mtakayopewa wakati Yesu Kristo atakapoonekana!
Wherefore gird up the loins of your mind, be sober, and hope undoubtingly for the grace that is to be brought to you at the manifestation of Jesus Christ;
14 Kama watoto wa Mungu wenye utii, msikubali kamwe kufuata tena tamaa mbaya mlizokuwa nazo wakati mlipokuwa wajinga.
as children of obedience, not conforming yourselves to the former lusts in your ignorance;
15 Bali mnapaswa kuwa watakatifu katika mwenendo wenu wote, kama vile yule aliyewaiteni ni mtakatifu.
but as he who called you is holy, be ye also holy in all your conduct;
16 Maandiko yasema: “Muwe watakatifu, kwa kuwa mimi ni mtakatifu.”
because it is written, “Ye shall be holy, for I am holy.”
17 Mnapomtaja Mungu ninyi humwita Baba. Basi, jueni kwamba yeye humhukumu kila mmoja kadiri ya matendo yake, bila ubaguzi. Hivyo tumieni wakati wenu uliowabakia hapa ugenini katika kumcha Mungu.
And if ye call him Father who without respect of persons judgeth according to each one's work, pass the time of your sojourning here in fear;
18 Maana mnajua kwamba ninyi mlikombolewa katika mwenendo wenu usiofaa ambao mliupokea kutoka kwa wazee wenu, si kwa vitu vyenye kuharibika: kwa fedha na dhahabu;
knowing that not with perishable things, silver or gold, were ye redeemed from your vain manner of life received by tradition from your fathers,
19 bali mlikombolewa kwa damu tukufu ya Kristo, ambaye alikuwa kama mwana kondoo asiye na dosari wala doa.
but with the precious blood of Christ, as of a lamb without blemish and without spot;
20 Yeye alikuwa ameteuliwa na Mungu kabla ya ulimwengu kuumbwa, akafunuliwa siku hizi za mwisho kwa ajili yenu.
who was foreknown indeed before the foundation of the world, but manifested in these last times for you,
21 Kwa njia yake, ninyi mnamwamini Mungu aliyemfufua kutoka wafu na kumpa utukufu; na hivyo imani na matumaini yenu yako kwa Mungu.
who through him have faith in God, who raised him from the dead and gave him glory, so that your faith and hope are in God.
22 Maadamu sasa, kwa kuutii ukweli, ninyi mmezitakasa roho zenu na kuwapenda wenzenu bila unafiki, basi, pendaneni kwa moyo wote.
Seeing ye have purified your souls in obeying the truth unto unfeigned brotherly love, love one another from the heart, fervently;
23 Maana kwa njia ya neno hai la Mungu, ninyi mmezaliwa upya, si kama watoto wa baba awezaye kufa, bali baba asiyekufa milele. (aiōn g165)
being born again, not of perishable seed, but of imperishable, through the word of God, which liveth and abideth. (aiōn g165)
24 Kama Maandiko yasemavyo: “Kila binadamu ni kama nyasi, na utukufu wake wote ni kama maua ya porini. Nyasi hunyauka na maua huanguka.
Because, “All flesh is as grass, and all its glory as the flower of grass; the grass withered, and its flower fell off;
25 Lakini neno la Bwana hudumu milele.” Neno hilo ni hiyo Habari Njema iliyohubiriwa kwenu. (aiōn g165)
but the word of the Lord abideth for ever;” and this is the word which was preached to you. (aiōn g165)

< 1 Petro 1 >