< 1 Petro 1 >
1 Mimi Petro, mtume wa Yesu Kristo nawaandikia ninyi wateule wa Mungu Baba, ambao mmetawanyika na mnaishi kama wakimbizi huko Ponto, Galatia, Kapadokia, Asia na Bithunia.
Pierre, apôtre de Jésus-Christ, aux élus qui sont étrangers et dispersés dans le Pont, la Galatie, la Cappadoce, l'Asie et la Bithynie;
2 Mungu Baba aliwateua ninyi kufuatana na kusudi lake, na mmefanywa watakatifu na Roho, mpate kumtii Yesu Kristo na kusafishwa kwa damu yake. Nawatakieni neema na amani tele.
qui sont élus selon la prescience de Dieu, le Père, et sanctifiés par l'Esprit, pour obéir à Jésus-Christ et pour avoir part à l'aspersion de son sang: Que la grâce et la paix vous soient multipliées
3 Asifiwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa huruma yake kuu alitufanya tuzaliwe upya kwa kumfufua Yesu kutoka wafu. Ametujalia tumaini lenye uzima,
Béni soit Dieu, le Père de notre Seigneur Jésus-Christ, qui, dans sa grande miséricorde, nous a fait renaître, pour que nous ayons, par la résurrection de Jésus-Christ d'entre les morts, une espérance vivante,
4 na hivyo tunatazamia kupata baraka zile ambazo Mungu aliwawekea watu wake. Mungu amewawekeeni baraka hizo mbinguni ambako haziwezi kuoza au kuharibika au kufifia.
un héritage qui ne peut être ni corrompu, ni souillé, ni flétri, et qui vous est réservé dans les cieux,
5 Hizo zitakuwa zenu ninyi ambao kwa imani mnalindwa salama kwa nguvu ya Mungu kwa ajili ya wokovu ambao uko tayari kufunuliwa mwishoni mwa nyakati.
à vous que la puissance de Dieu garde par la foi, pour le salut qui est prêt à être manifesté dans les derniers temps!
6 Furahini kuhusu jambo hilo, ijapokuwa sasa, kwa kitambo kidogo, itawabidi kuhuzunika kwa sababu ya majaribio mbalimbali mnayoteseka.
Vous vous en réjouissez, quoique maintenant, puisqu'il le faut, vous soyez, pour un peu de temps, attristés par diverses épreuves;
7 Shabaha yake ni kuthibitisha imani yenu. Hata dhahabu yenyewe ambayo huharibika, hujaribiwa kwa moto; hali kadhalika na imani yenu ambayo ni ya thamani zaidi kuliko dhahabu, ni lazima ijaribiwe ipate kuwa thabiti. Hapo mtapokea sifa na utukufu na heshima Siku ile Yesu Kristo atakapofunuliwa.
afin que l'épreuve de votre foi, — beaucoup plus précieuse que l'or périssable qui pourtant est éprouvé par le feu, — tourne à votre louange, à votre honneur et à votre gloire, lorsque Jésus-Christ paraîtra,
8 Ninyi mnampenda ingawaje hamjamwona, na mnamwamini ingawa hamumwoni sasa. Hivyo, mnafurahi kwa furaha tukufu isiyoelezeka,
lui que vous aimez, sans l'avoir vu, en qui vous croyez, sans le voir encore. Et vous vous réjouissez d'une joie ineffable et glorieuse,
9 kwa sababu mnapokea wokovu wa roho zenu ambao ni lengo la imani yenu.
remportant le prix de votre foi, le salut de vos âmes.
10 Manabii walipeleleza kwa makini na kufanya uchunguzi juu ya wokovu huo, wakabashiri juu ya neema hiyo ambayo ninyi mngepewa.
Ce salut a été l'objet des recherches et des investigations des prophètes, qui ont prophétisé touchant la grâce qui vous était destinée.
11 Walijaribu kujua nyakati na mazingira ya tukio hilo, yaani wakati alioudokezea Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao, akibashiri juu ya mateso yatakayompata Kristo na utukufu utakaofuata.
Ils cherchaient à découvrir l'époque et les circonstances marquées par l'Esprit de Christ, qui était en eux, et qui rendait à l'avance témoignage aux souffrances de Christ et aux gloires qui devaient les suivre.
12 Mungu aliwafunulia kwamba wakati walipokuwa wanasema juu ya hayo mambo ambayo ninyi mmekwisha sikia sasa kutoka kwa wale wajumbe waliowatangazieni Habari Njema kwa nguvu ya Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni, hiyo kazi yao haikuwa kwa faida yao wenyewe, bali kwa ajili yenu. Hayo ndiyo mambo ambayo hata malaika wangependa kuyafahamu.
Il leur fut révélé que ce n'était pas pour eux-mêmes, mais pour vous, qu'ils étaient dispensateurs de ces choses, que vous ont maintenant annoncées ceux qui vous ont prêché l'Évangile, par l'Esprit saint envoyé du ciel, et au fond desquelles les anges désirent plonger leurs regards.
13 Kwa hiyo, basi, muwe tayari kabisa kwa nia, na kukesha. Wekeni tumaini lenu lote katika baraka ile mtakayopewa wakati Yesu Kristo atakapoonekana!
Vous donc, ayant ceint les reins de votre esprit, étant sobres, attendez avec une parfaite espérance la grâce qui doit vous être dispensée, lorsque Jésus-Christ paraîtra.
14 Kama watoto wa Mungu wenye utii, msikubali kamwe kufuata tena tamaa mbaya mlizokuwa nazo wakati mlipokuwa wajinga.
Comme des enfants obéissants, ne vous conformez pas aux convoitises qui régnaient autrefois en vous, au temps de votre ignorance.
15 Bali mnapaswa kuwa watakatifu katika mwenendo wenu wote, kama vile yule aliyewaiteni ni mtakatifu.
Mais, de même que celui qui vous a appelés est saint, vous aussi, soyez saints dans toute votre conduite,
16 Maandiko yasema: “Muwe watakatifu, kwa kuwa mimi ni mtakatifu.”
puisqu'il est écrit: «Soyez saints, car je suis saint»
17 Mnapomtaja Mungu ninyi humwita Baba. Basi, jueni kwamba yeye humhukumu kila mmoja kadiri ya matendo yake, bila ubaguzi. Hivyo tumieni wakati wenu uliowabakia hapa ugenini katika kumcha Mungu.
Et si vous invoquez comme Père celui qui, sans acception de personnes, juge chacun selon son oeuvre, conduisez-vous avec crainte pendant le temps de votre séjour sur la terre,
18 Maana mnajua kwamba ninyi mlikombolewa katika mwenendo wenu usiofaa ambao mliupokea kutoka kwa wazee wenu, si kwa vitu vyenye kuharibika: kwa fedha na dhahabu;
sachant que ce n'est point par des choses périssables, comme l'argent ou l'or, que vous avez été rachetés de la vaine manière de vivre que vos pères vous avaient transmise,
19 bali mlikombolewa kwa damu tukufu ya Kristo, ambaye alikuwa kama mwana kondoo asiye na dosari wala doa.
mais par le précieux sang de Christ, l'Agneau sans défaut et sans tache,
20 Yeye alikuwa ameteuliwa na Mungu kabla ya ulimwengu kuumbwa, akafunuliwa siku hizi za mwisho kwa ajili yenu.
déjà prédestiné avant la création du monde et manifesté à la fin des temps à cause de vous.
21 Kwa njia yake, ninyi mnamwamini Mungu aliyemfufua kutoka wafu na kumpa utukufu; na hivyo imani na matumaini yenu yako kwa Mungu.
Par lui aussi, vous croyez en Dieu qui l'a ressuscité des morts et qui l'a glorifié, de telle sorte que c'est en Dieu que reposent votre foi et votre espérance.
22 Maadamu sasa, kwa kuutii ukweli, ninyi mmezitakasa roho zenu na kuwapenda wenzenu bila unafiki, basi, pendaneni kwa moyo wote.
Quant à vous, en obéissant à la vérité, vous avez purifié vos âmes: ayez donc un sincère amour fraternel; aimez-vous ardemment les uns les autres, du fond du coeur,
23 Maana kwa njia ya neno hai la Mungu, ninyi mmezaliwa upya, si kama watoto wa baba awezaye kufa, bali baba asiyekufa milele. (aiōn )
vous qui avez été régénérés, non par une semence corruptible, mais par une semence incorruptible, par la parole de Dieu, qui est vivante et qui dure éternellement! (aiōn )
24 Kama Maandiko yasemavyo: “Kila binadamu ni kama nyasi, na utukufu wake wote ni kama maua ya porini. Nyasi hunyauka na maua huanguka.
Car toute créature est comme l'herbe, et toute sa gloire comme la fleur de l'herbe. L'herbe sèche, et sa fleur tombe,
25 Lakini neno la Bwana hudumu milele.” Neno hilo ni hiyo Habari Njema iliyohubiriwa kwenu. (aiōn )
mais la parole du Seigneur demeure éternellement. C'est cette parole qui vous a été annoncée par l'Évangile. (aiōn )