< 1 Petro 1 >
1 Mimi Petro, mtume wa Yesu Kristo nawaandikia ninyi wateule wa Mungu Baba, ambao mmetawanyika na mnaishi kama wakimbizi huko Ponto, Galatia, Kapadokia, Asia na Bithunia.
Peter, an apostle of Jesus Christ, to the elect sojourners of the Dispersion in Pontus, Galatia, Cappadocia, Asia and Bithynia,
2 Mungu Baba aliwateua ninyi kufuatana na kusudi lake, na mmefanywa watakatifu na Roho, mpate kumtii Yesu Kristo na kusafishwa kwa damu yake. Nawatakieni neema na amani tele.
elect according to the foreknowledge of God the Father, by the setting apart of the Spirit, unto obedience and sprinkling with the blood of Jesus Christ: May grace and peace be multiplied to you.
3 Asifiwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa huruma yake kuu alitufanya tuzaliwe upya kwa kumfufua Yesu kutoka wafu. Ametujalia tumaini lenye uzima,
Blessed be the God and Father of our Lord Jesus Christ, who according to His great mercy has given us another birth into a living hope through the resurrection of Jesus Christ from among the dead,
4 na hivyo tunatazamia kupata baraka zile ambazo Mungu aliwawekea watu wake. Mungu amewawekeeni baraka hizo mbinguni ambako haziwezi kuoza au kuharibika au kufifia.
into an imperishable and undefiled and unfading inheritance, already reserved in the heavens for you,
5 Hizo zitakuwa zenu ninyi ambao kwa imani mnalindwa salama kwa nguvu ya Mungu kwa ajili ya wokovu ambao uko tayari kufunuliwa mwishoni mwa nyakati.
who are being guarded by the power of God through faith unto a salvation ready to be revealed in the last time.
6 Furahini kuhusu jambo hilo, ijapokuwa sasa, kwa kitambo kidogo, itawabidi kuhuzunika kwa sababu ya majaribio mbalimbali mnayoteseka.
You should be overjoyed about this, even if just now, briefly, of necessity, you have been distressed by a variety of trials,
7 Shabaha yake ni kuthibitisha imani yenu. Hata dhahabu yenyewe ambayo huharibika, hujaribiwa kwa moto; hali kadhalika na imani yenu ambayo ni ya thamani zaidi kuliko dhahabu, ni lazima ijaribiwe ipate kuwa thabiti. Hapo mtapokea sifa na utukufu na heshima Siku ile Yesu Kristo atakapofunuliwa.
so that the demonstrated genuineness of your faith (much more precious than gold that perishes, albeit tested through fire) may translate into praise, glory and honor at the revelation of Jesus Christ
8 Ninyi mnampenda ingawaje hamjamwona, na mnamwamini ingawa hamumwoni sasa. Hivyo, mnafurahi kwa furaha tukufu isiyoelezeka,
—whom not having understood you love, into whom believing (not yet seeing) you exult with joy inexpressible, already glorified,
9 kwa sababu mnapokea wokovu wa roho zenu ambao ni lengo la imani yenu.
obtaining for yourselves the end result of your faith, the salvation of your souls.
10 Manabii walipeleleza kwa makini na kufanya uchunguzi juu ya wokovu huo, wakabashiri juu ya neema hiyo ambayo ninyi mngepewa.
Concerning this salvation the prophets, who prophesied about the grace that would come to you, searched and inquired diligently,
11 Walijaribu kujua nyakati na mazingira ya tukio hilo, yaani wakati alioudokezea Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao, akibashiri juu ya mateso yatakayompata Kristo na utukufu utakaofuata.
investigating into whom, or what sort of time, the Spirit of Christ who was in them was indicating as He testified beforehand the sufferings that would be inflicted on Christ and the glories that would follow them.
12 Mungu aliwafunulia kwamba wakati walipokuwa wanasema juu ya hayo mambo ambayo ninyi mmekwisha sikia sasa kutoka kwa wale wajumbe waliowatangazieni Habari Njema kwa nguvu ya Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni, hiyo kazi yao haikuwa kwa faida yao wenyewe, bali kwa ajili yenu. Hayo ndiyo mambo ambayo hata malaika wangependa kuyafahamu.
It was revealed to them that they were not ministering these things to themselves, but to you; which things have now been announced to you by those who proclaimed the gospel to you, with the Holy Spirit sent from heaven—things that angels really desire to look into.
13 Kwa hiyo, basi, muwe tayari kabisa kwa nia, na kukesha. Wekeni tumaini lenu lote katika baraka ile mtakayopewa wakati Yesu Kristo atakapoonekana!
Therefore, having girded up the loins of your mind, staying sober, rest your hope fully upon the grace being brought to you in the revelation of Jesus Christ—
14 Kama watoto wa Mungu wenye utii, msikubali kamwe kufuata tena tamaa mbaya mlizokuwa nazo wakati mlipokuwa wajinga.
as children of obedience, not conforming yourselves to the former lusts as in your ignorance,
15 Bali mnapaswa kuwa watakatifu katika mwenendo wenu wote, kama vile yule aliyewaiteni ni mtakatifu.
but just as He who called you is holy, you also be holy in all your way of life,
16 Maandiko yasema: “Muwe watakatifu, kwa kuwa mimi ni mtakatifu.”
because it is written, “You shall be holy, for I am holy.”
17 Mnapomtaja Mungu ninyi humwita Baba. Basi, jueni kwamba yeye humhukumu kila mmoja kadiri ya matendo yake, bila ubaguzi. Hivyo tumieni wakati wenu uliowabakia hapa ugenini katika kumcha Mungu.
Also, since you invoke as Father the One who without partiality judges according to each one's work, conduct yourselves during the time of your sojourn here in fear,
18 Maana mnajua kwamba ninyi mlikombolewa katika mwenendo wenu usiofaa ambao mliupokea kutoka kwa wazee wenu, si kwa vitu vyenye kuharibika: kwa fedha na dhahabu;
knowing that it was not with perishable things (silver or gold) that you were redeemed from the futile way of life handed down by your forefathers,
19 bali mlikombolewa kwa damu tukufu ya Kristo, ambaye alikuwa kama mwana kondoo asiye na dosari wala doa.
but with the precious blood of Christ, as of a faultless and pure lamb;
20 Yeye alikuwa ameteuliwa na Mungu kabla ya ulimwengu kuumbwa, akafunuliwa siku hizi za mwisho kwa ajili yenu.
who was foreknown indeed before the foundation of the world, but was revealed in these last times for your sake,
21 Kwa njia yake, ninyi mnamwamini Mungu aliyemfufua kutoka wafu na kumpa utukufu; na hivyo imani na matumaini yenu yako kwa Mungu.
who through Him are believing into God, who raised Him out from the dead and gave Him glory, so that your faith and hope are into God.
22 Maadamu sasa, kwa kuutii ukweli, ninyi mmezitakasa roho zenu na kuwapenda wenzenu bila unafiki, basi, pendaneni kwa moyo wote.
Since you have purified your souls by obeying the truth through the Spirit, resulting in sincere brotherly love, you must love one another fervently from a pure heart,
23 Maana kwa njia ya neno hai la Mungu, ninyi mmezaliwa upya, si kama watoto wa baba awezaye kufa, bali baba asiyekufa milele. (aiōn )
having been begotten again, not from a corruptible seed but an incorruptible, through the living Word of God that remains valid forever. (aiōn )
24 Kama Maandiko yasemavyo: “Kila binadamu ni kama nyasi, na utukufu wake wote ni kama maua ya porini. Nyasi hunyauka na maua huanguka.
For: “All flesh is as grass, and all man's glory as flower of grass. The grass withers and its flower falls off, but the Lord's word endures forever.”
25 Lakini neno la Bwana hudumu milele.” Neno hilo ni hiyo Habari Njema iliyohubiriwa kwenu. (aiōn )
Now this is the good word that was proclaimed to you. (aiōn )