< 1 Yohana 4 >
1 Wapenzi wangu, msimsadiki kila mtu asemaye kwamba ana Roho wa Mungu, bali chunguzeni kwa makini kama huyo mtu anaongozwa na Roho wa Mungu au la, Maana manabii wengi wa uongo wamezuka ulimwenguni.
Dear friends, many people [who have a false message] are teaching it to people [MTY]. So do not trust every [message that someone claims/says that God’s] Spirit [MTY] [gave to him]. Instead, (test/think carefully about) the teachings that [you hear] in order to know whether they are from God or not.
2 Hii ndiyo njia ya kujua kama mtu anaongozwa na Roho wa Mungu: Kila anayekiri kwamba Kristo alikuja, akawa binadamu, mtu huyo anaye Roho wa Mungu.
[I will tell] you how to recognize [teachings that come from] the Spirit of God: Those who affirm/say that Jesus Christ came [from God] to become a human [like us] are [teaching a message] that is from God.
3 Lakini mtu yeyote asiyemkiri Kristo hivyo, hana huyo Roho atokaye kwa Mungu. Mtu huyo ana roho ambaye ni wa Adui wa Kristo; nanyi mlikwisha sikia kwamba anakuja, na sasa tayari amekwisha wasili ulimwenguni!
But those who do not affirm/say [that about] Jesus are not [teaching a message] from God. [They are teachers who] oppose Christ. You have heard that people like that are coming [to be among us]. Even now they are already here!
4 Lakini ninyi, watoto, ni wake Mungu na mmekwisha washinda hao manabii wa uongo; maana Roho aliye ndani yenu ana nguvu zaidi kuliko roho aliye ndani ya hao walio wa ulimwengu.
As for you who are very dear to me, you belong to God, and you have refused [the false messages] that those people [teach], because [God], who enables you [to do what he wants], is (greater/more powerful) than ([Satan/the devil]), who enables (godless people/people who conduct their lives in a way that displeases God) [MTY].
5 Wao husema mambo ya ulimwengu, nao ulimwengu huwasikiliza kwani wao ni wa ulimwengu.
As for [those who are teaching what is false], they are (godless people/people whose lives are displeasing to God) [MTY]. Because of that, they teach what (godless people/people whose lives are displeasing to God) [MTY] want to hear. That is why the (godless people/people whose lives displease God) [MTY] listen to them.
6 Lakini sisi ni wake Mungu. Mtu anayemjua Mungu hutusikiliza, mtu asiye wa Mungu hatusikilizi. Basi, kwa njia hiyo tunaweza kutambua tofauti kati ya Roho wa ukweli na roho wa uongo.
As for us [(exc)], [because] we belong to God, whoever (knows/has a close relationship with) God listens to us. [But] those who do not belong to God do not listen to us. That is how we can know whether [the things that people are teaching] [MTY] are true or whether they are false, and deceiving [people].
7 Wapenzi wangu, tupendane, maana upendo hutoka kwa Mungu. Kila mtu aliye na upendo ni mtoto wa Mungu, na anamjua Mungu.
Dear friends, we must love each other, because God [enables us] to love [each other], and because those who love [their fellow believers] have become God’s children and (know/have a close relationship with) him.
8 Mtu asiye na upendo hamjui Mungu, maana Mungu ni upendo.
God’s [nature] is to love [all people]. So those who do not love [their fellow believers] do not (know/have a relationship with) God.
9 Na Mungu alionyesha upendo wake kwetu kwa kumtuma Mwanae wa pekee ulimwenguni, ili tuwe na uzima kwa njia yake.
I will tell you how God has shown us [that he] loves us: He sent (his only Son/the only one who was also God) [to live] on the earth to enable us to live [eternally] as a result of [our trusting in what] he [accomplished for us by dying for us].
10 Hivi ndivyo upendo ulivyo: si kwamba sisi tulikuwa tumempenda Mungu kwanza, bali kwamba yeye alitupenda hata akamtuma Mwanae awe sadaka ya kutuondolea dhambi zetu.
[And God] has shown [us what it means to] love [another person]: [It does] not [mean] that we loved God, but [it means] that God loved us and sent (his Son/the one who was also God) to sacrifice [his life] in order that [our sins might be forgiven] {[he might forgive] our sins}.
11 Wapenzi wangu, ikiwa Mungu alitupenda hivyo, basi, nasi tunapaswa kupendana.
Dear friends, since God loves us like that, we certainly ought to love each other!
12 Hakuna mtu aliyekwisha mwona Mungu kamwe; lakini kama tukipendana Mungu anaishi katika muungano nasi, na upendo wake unakamilika ndani yetu.
No one has ever seen God. [Nevertheless], if we love each other, [it is evident that] God lives within us and that we love others just like he [intends/wants us to do].
13 Tunajua kwamba tunaishi katika umoja na Mungu, naye Mungu anaishi katika umoja nasi, kwani yeye ametupa Roho wake.
[I will tell you] how we can be sure that we have a close relationship with God and that God is within us: He has put his Spirit within us.
14 Sisi tumeona na kuwaambia wengine kwamba Baba alimtuma Mwanae awe Mwokozi wa ulimwengu.
We [apostles] have seen (God’s Son/the one who is also God), and [we tell people] that the Father sent him to save [the people in] the world [MTY] [from being punished for their sins].
15 Kila mtu anayekiri kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu anaishi katika muungano na mtu huyo, naye anaishi katika muungano na Mungu.
[So] those who affirm/say that Jesus is the (Son of/one who is also) God, God is within them, and they have a close relationship with God.
16 Basi, sisi tunajua na tunaamini upendo alio nao Mungu kwetu sisi. Mungu ni upendo, na kila mtu aishiye katika upendo, anaishi katika muungano na Mungu, na Mungu anaishi katika muungano naye.
We have experienced how God loves us and we believe that he loves us. [As a result, we love others. Because] God’s [nature] is to love people, those who continue to love [others] have a close relationship with God, and God has a close relationship with them.
17 Upendo umekamilika ndani yetu kusudi tuweze kuwa na ujasiri Siku ile ya Hukumu; kwani maisha yetu hapa duniani ni kama yale ya Kristo.
We [should] love others completely. And if we do that, when the time comes for [him to] judge us, we will be confident [that he will not condemn us] (OR, [that we have a close relationship with him]). [We will be confident of that] because of our [conducting our lives] in this world as Christ did.
18 Palipo na upendo hapana uoga; naam, upendo kamili hufukuza uoga wote. Basi, mtu mwenye uoga hajakamilika bado katika upendo, kwani uoga huhusikana na adhabu.
We will not be afraid [of God] if we [truly] love [him], because those who love [God] completely cannot possibly be afraid [of him]. [We would be] afraid only [if we thought that he would] punish us. So those who are afraid [of God certainly] are not loving [God] completely.
19 Sisi tuna upendo kwa sababu Mungu alitupenda kwanza.
We love [God and our fellow believers] because God loved us first.
20 Mtu akisema kwamba anampenda Mungu, hali anamchukia ndugu yake, huyo ni mwongo. Maana mtu asiyempenda ndugu yake ambaye anamwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hamwoni.
[So] those who say “I love God” but hate a fellow believer are lying. Those who do not love one of their fellow believers, whom they have seen, certainly cannot be loving God, whom they have not seen.
21 Basi, hii ndiyo amri aliyotupa Kristo: Anayempenda Mungu anapaswa pia kumpenda ndugu yake.
Keep in mind that this is what God has commanded us: If we love him, we must also love our fellow believers.