< 1 Yohana 4 >

1 Wapenzi wangu, msimsadiki kila mtu asemaye kwamba ana Roho wa Mungu, bali chunguzeni kwa makini kama huyo mtu anaongozwa na Roho wa Mungu au la, Maana manabii wengi wa uongo wamezuka ulimwenguni.
Do not believe every spirit, beloved, but test the spirits to see whether they are of God; for many false prophets are gone out into the world.
2 Hii ndiyo njia ya kujua kama mtu anaongozwa na Roho wa Mungu: Kila anayekiri kwamba Kristo alikuja, akawa binadamu, mtu huyo anaye Roho wa Mungu.
By this you know the Spirit of God; every spirit that confesses that Jesus Christ is come in the flesh is from God;
3 Lakini mtu yeyote asiyemkiri Kristo hivyo, hana huyo Roho atokaye kwa Mungu. Mtu huyo ana roho ambaye ni wa Adui wa Kristo; nanyi mlikwisha sikia kwamba anakuja, na sasa tayari amekwisha wasili ulimwenguni!
and every spirit which confesses him not, is not from God. And this is that spirit of Antichrist of which you have heard that it is coming, and that now it is already in the world.
4 Lakini ninyi, watoto, ni wake Mungu na mmekwisha washinda hao manabii wa uongo; maana Roho aliye ndani yenu ana nguvu zaidi kuliko roho aliye ndani ya hao walio wa ulimwengu.
My little children, you are of God and have conquered them; because he that is within you is greater than he that is in the world.
5 Wao husema mambo ya ulimwengu, nao ulimwengu huwasikiliza kwani wao ni wa ulimwengu.
They are of the world, and for this reason they speak as of the world, and the world listens to them.
6 Lakini sisi ni wake Mungu. Mtu anayemjua Mungu hutusikiliza, mtu asiye wa Mungu hatusikilizi. Basi, kwa njia hiyo tunaweza kutambua tofauti kati ya Roho wa ukweli na roho wa uongo.
But you are of God. He who is beginning to know God listens to us; he who is not of God does not listen to us. By this we may distinguish the spirit of truth from the spirit of error.
7 Wapenzi wangu, tupendane, maana upendo hutoka kwa Mungu. Kila mtu aliye na upendo ni mtoto wa Mungu, na anamjua Mungu.
Beloved, let us love one another; for love is of God; and every one that loves us a child of God.
8 Mtu asiye na upendo hamjui Mungu, maana Mungu ni upendo.
He who does not love, does not know God; for God is love.
9 Na Mungu alionyesha upendo wake kwetu kwa kumtuma Mwanae wa pekee ulimwenguni, ili tuwe na uzima kwa njia yake.
In this was the love of God clearly shown toward us, by his sending his only Son into the world, so that we might live through him.
10 Hivi ndivyo upendo ulivyo: si kwamba sisi tulikuwa tumempenda Mungu kwanza, bali kwamba yeye alitupenda hata akamtuma Mwanae awe sadaka ya kutuondolea dhambi zetu.
In this is love, not that we loved God, but that he loved us, and sent his Son to be a propitiation for our sins.
11 Wapenzi wangu, ikiwa Mungu alitupenda hivyo, basi, nasi tunapaswa kupendana.
If God so loved us, beloved, we also ought to love one another.
12 Hakuna mtu aliyekwisha mwona Mungu kamwe; lakini kama tukipendana Mungu anaishi katika muungano nasi, na upendo wake unakamilika ndani yetu.
No man has ever gazed on God; but if we love one another, God ever abides in us, and his love is perfected in us.
13 Tunajua kwamba tunaishi katika umoja na Mungu, naye Mungu anaishi katika umoja nasi, kwani yeye ametupa Roho wake.
By this we come to know that we are abiding in him, and he in us, because he has given us of his Spirit;
14 Sisi tumeona na kuwaambia wengine kwamba Baba alimtuma Mwanae awe Mwokozi wa ulimwengu.
and we have beheld and do testify that the Father has sent the Son to be the Saviour of the world.
15 Kila mtu anayekiri kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu anaishi katika muungano na mtu huyo, naye anaishi katika muungano na Mungu.
If any man confesses that "Jesus is the Son of God." God is abiding in that man, and he in God.
16 Basi, sisi tunajua na tunaamini upendo alio nao Mungu kwetu sisi. Mungu ni upendo, na kila mtu aishiye katika upendo, anaishi katika muungano na Mungu, na Mungu anaishi katika muungano naye.
And we do know and have believed the love which God has for us. God is love; and he who is abiding in love is abiding in God, and God is abiding in him.
17 Upendo umekamilika ndani yetu kusudi tuweze kuwa na ujasiri Siku ile ya Hukumu; kwani maisha yetu hapa duniani ni kama yale ya Kristo.
In this is love made perfect with us, so that we may have cheerful confidence in the Day of Judgment, because we are living in this world as He lives.
18 Palipo na upendo hapana uoga; naam, upendo kamili hufukuza uoga wote. Basi, mtu mwenye uoga hajakamilika bado katika upendo, kwani uoga huhusikana na adhabu.
Fear does not exist in love; but love, when it is perfect, drives out fear. For fear has always torment, and he who has fear is not yet perfected in love.
19 Sisi tuna upendo kwa sababu Mungu alitupenda kwanza.
We love because He loved us first.
20 Mtu akisema kwamba anampenda Mungu, hali anamchukia ndugu yake, huyo ni mwongo. Maana mtu asiyempenda ndugu yake ambaye anamwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hamwoni.
If any one says, "I love God," and yet hates his brother, he is a liar; for he who does not love his brother whom he has seen, cannot possibly love God, whom he has not seen.
21 Basi, hii ndiyo amri aliyotupa Kristo: Anayempenda Mungu anapaswa pia kumpenda ndugu yake.
And we have this command from God. HE WHO LOVES GOD IS TO LOVE HIS BROTHER ALSO.

< 1 Yohana 4 >