< 1 Yohana 3 >
1 Oneni basi, jinsi Baba alivyotupenda mno hata tunaitwa watoto wa Mungu! Na kweli, ndivyo tulivyo. Ndiyo maana ulimwengu haututambui sisi, kwani haumjui Mungu.
Behold what manner of love the Father has given us in allowing us to be called "Children of God!" And that is what we are. For this reason the world does not recognize us, because it did not know him.
2 Wapenzi wangu, sisi ni watoto wa Mungu sasa, lakini bado haijaonekana wazi jinsi tutakavyokuwa. Lakini tunajua kwamba wakati Kristo atakapotokea, tutafanana naye kwani tutamwona vile alivyo.
We are God’s children now, beloved; what we shall be has never yet been made manifest. But we know that when he is manifested we shall be like him; for we shall see him even as he is.
3 Basi, kila mtu aliye na tumaini hili katika Kristo, hujiweka safi kama vile Kristo alivyo safi kabisa.
And every one who is holding this hope in him is purifying himself, even as he is pure.
4 Kila mtu atendaye dhambi anavunja sheria ya Mungu, maana dhambi ni uvunjaji wa sheria.
Every one who commits sin commits also lawlessness. Sin is lawlessness.
5 Mnajua kwamba Kristo alikuja kuziondoa dhambi zetu, na kwamba kwake hamna dhambi yoyote.
And you know that he was manifested to take away sins; and in him is no sin.
6 Basi, kila aishiye katika muungano na Kristo hatendi dhambi; lakini kila mtu atendaye dhambi hakupata kamwe kumwona, wala kumjua Kristo.
Whoever continually abides in him does not habitually sin; whoever lives in sin has not seen him, nor come to know him.
7 Basi, watoto wangu, msikubali kupotoshwa na mtu yeyote. Mtu atendaye matendo maadilifu ni mwadilifu kama vile Kristo alivyo mwadilifu kabisa.
My children, let no one deceive you; he who is working righteousness is righteous, just as he is righteous.
8 Lakini atendaye dhambi ni wa Ibilisi, maana Ibilisi ametenda dhambi tangu mwanzo. Lakini Mwana wa Mungu alikuja duniani kuiharibu kazi ya Ibilisi.
He who is committing sin is of the devil, because from the beginning of the devil is sinning. It was for this cause that the Son of God was manifested, that he might destroy the works of the devil.
9 Kila aliye mtoto wa Mungu hatendi dhambi, maana anayo hali ya kimungu ndani yake; hawezi kutenda dhambi kwa sababu yeye ni mtoto wa Mungu.
Whoever is a child of God cannot go on sinning, because his seed is abiding in him; and he cannot go on sinning because he is a child of God.
10 Lakini yeyote asiyetenda mambo maadilifu, au asiyempenda ndugu yake, huyo si mtoto wa Mungu. Hiyo ndiyo tofauti iliyoko kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Ibilisi.
In this the children of God are manifest, and the children of the devil; for every one who does not work righteousness is not a child of God, nor is he who does not love his brother.
11 Na, ujumbe mliousikia tangu mwanzo ndio huu: Tunapaswa kupendana!
For this is the message that you have listened to from the beginning, "WE ARE TO LOVE ONE ANOTHER."
12 Tusiwe kama Kaini ambaye, kwa kuongozwa na yule Mwovu, alimuua ndugu yake. Na, kwa nini alimuua? Kwa sababu matendo yake yalikuwa maovu, lakini yale ya ndugu yake yalikuwa mema!
We are not to be like Cain, who belonged to the Evil One, and murdered his brother. And why did he murder him? It was because his own deeds were evil, and his brother’s, righteous.
13 Basi, ndugu zangu, msishangae kama ulimwengu unawachukia ninyi.
Do not wonder, brothers, if the world continues to hate you.
14 Sisi tunajua kwamba tumekwisha pita kutoka katika kifo na kuingia katika uzima kwa sababu tunawapenda ndugu zetu. Mtu asiye na upendo hubaki katika kifo.
We know that we have migrated, out of death into life, because we love our brothers. He who has no love is abiding in death.
15 Kila anayemchukia ndugu yake ni muuaji; nanyi mnajua kwamba muuaji yeyote yule hana uzima wa milele ndani yake. (aiōnios )
Every one who is hating his brother is a murderer, and you know that no murderer has eternal life abiding in him. (aiōnios )
16 Sisi tumepata kujua upendo ni nini, kwani Kristo aliyatoa maisha yake kwa ajili yetu. Nasi vilevile tunapaswa kuyatoa maisha yetu kwa ajili ya ndugu zetu.
By this we learn to know love, because he laid down his life for us; so we ought to lay down our lives for our brothers.
17 Basi, mtu akiwa na mali za hapa duniani, halafu akamwona ndugu yake ana shida, lakini akawa na moyo mgumu bila kumwonea huruma, anawezaje kusema kwamba anampenda Mungu?
But whoever has this world’s goods, and beholds his brother in need, and shuts up his heart against him, how can the love of God continue to abide in him?
18 Watoto wangu, upendo wetu usiwe maneno matupu, bali uwe upendo wa kweli na wa vitendo.
My children, let us not love in word nor in talk, but in deed and in truth.
19 Hivyo ndivyo tuwezavyo kuwa na hakika kwamba sisi ni watu wa ukweli; na hatutakuwa na wasiwasi mbele ya Mungu.
By this we shall come to know that we are really of the truth,
20 Kwa maana, hata kama dhamiri yetu yatuhukumu, twajua kwamba Mungu ni mkuu zaidi kuliko dhamiri, na kwamba yeye ajua kila kitu.
and shall persuade our heart in his presence whenever our heart condemns us, because God is greater than our heart and knows all things.
21 Wapenzi wangu, kama dhamiri yetu haina lawama juu yetu, basi, twaweza kuwa na uthabiti mbele ya Mungu,
Beloved, if our heart condemn us not, we have confidence toward God,
22 na twaweza kupokea kwake chochote tunachoomba, maana tunazitii amri zake na kufanya yale yanayompendeza.
and whatever we ask we are receiving from him, because we are keeping his commandments and doing those things that are pleasing in his sight.
23 Na, amri yake ndiyo hii: Kumwamini Mwanae Kristo, na kupendana kama alivyotuamuru.
His commandment is this, that we should believe in the name of his Son, Jesus Christ, and love one another as he has commanded us to do.
24 Anayezitii amri za Mungu anaishi katika muungano na Mungu na Mungu anaishi katika muungano naye. Kwa njia ya Roho ambaye Mungu ametujalia, sisi twajua kwamba Mungu anaishi katika muungano nasi.
He who keeps his commandments is abiding in Him, and Christ in him. By this we know that Christ is abiding in us, by the Spirit which he has given us.