< 1 Wakorintho 1 >

1 Mimi Paulo, niliyeitwa kuwa mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Sosthene,
Paul, called to be an emissary of Yeshua the Messiah through the will of God, and our brother Sosthenes,
2 tunawaandikia ninyi mlio kanisa la Mungu huko Korintho. Ninyi mmefanywa watakatifu katika kuungana na Kristo Yesu, mkaitwa muwe watu wa Mungu, pamoja na watu wote popote wanaomwomba Bwana wetu Yesu Kristo aliye Bwana wao na wetu pia.
to the assembly of God which is at Corinth—those who are sanctified in Messiah Yeshua, called holy ones, with all who call on the name of our Lord Yeshua the Messiah in every place, both theirs and ours:
3 Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
Grace to you and peace from God our Father and the Lord Yeshua the Messiah.
4 Ninamshukuru Mungu wangu daima kwa ajili yenu kwa sababu amewatunukia ninyi neema yake kwa njia ya Kristo Yesu.
I always thank my God concerning you for the grace of God which was given you in Messiah Yeshua,
5 Maana, kwa kuungana na Kristo mmetajirishwa katika kila kitu. Mmejaliwa elimu yote na uwezo wote wa kuhubiri,
that in everything you were enriched in him, in all speech and all knowledge—
6 kwani, ujumbe juu ya Kristo umethibitishwa ndani yenu,
even as the testimony of Messiah was confirmed in you—
7 hata hampungukiwi kipaji chochote cha kiroho mkiwa mnangojea kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
so that you come behind in no gift, waiting for the revelation of our Lord Yeshua the Messiah,
8 Yeye atawaimarisha ninyi mpaka mwisho mpate kuonekana bila hatia Siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.
who will also confirm you until the end, blameless in the day of our Lord Yeshua the Messiah.
9 Mungu ni mwaminifu; yeye aliwaita ninyi muwe na umoja na Mwanae Yesu Kristo Bwana wetu.
God is faithful, through whom you were called into the fellowship of his Son, Yeshua the Messiah our Lord.
10 Ndugu, ninawasihi kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo: pataneni nyote katika kila jambo msemalo; yasiweko mafarakano kati yenu; muwe na fikira moja na nia moja.
Now I beg you, brothers, through the name of our Lord, Yeshua the Messiah, that you all speak the same thing, and that there be no divisions among you, but that you be perfected together in the same mind and in the same judgment.
11 Ndugu zangu, habari nilizopata kutoka kwa watu kadhaa wa jamaa ya Kloe, zaonyesha wazi kwamba kuna kutoelewana kati yenu.
For it has been reported to me concerning you, my brothers, by those who are from Chloe’s household, that there are contentions among you.
12 Nataka kusema hivi: kila mmoja anasema chake: mmoja husema, “Mimi ni wa Paulo,” mwingine: “Mimi ni wa Apolo,” mwingine: “Mimi ni wa Kefa,” na mwingine: “Mimi ni wa Kristo,”.
Now I mean this, that each one of you says, “I follow Paul,” “I follow Apollos,” “I follow Kefa,” and, “I follow Messiah.”
13 Je, Kristo amegawanyika? Je, Paulo ndiye aliyesulubiwa kwa ajili yenu? Au je, mlibatizwa kwa jina la Paulo?
Is Messiah divided? Was Paul crucified for you? Or were you immersed into the name of Paul?
14 Namshukuru Mungu kwamba sikumbatiza mtu yeyote miongoni mwenu isipokuwa tu Krispo na Gayo.
I thank God that I immersed none of you except Crispus and Gaius,
15 Kwa hiyo hakuna awezaye kusema amebatizwa kwa jina langu.
so that no one should say that I had immersed you into my own name.
16 (Samahani, nilibatiza pia jamaa ya Stefana; lakini zaidi ya hawa, sidhani kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote.)
(I also immersed the household of Stephanas; besides them, I don’t know whether I immersed any other.)
17 Kristo hakunituma kubatiza, bali kuhubiri Habari Njema; tena, niihubiri bila kutegemea maarifa ya hotuba za watu kusudi nguvu ya kifo cha Kristo msalabani isibatilishwe.
For Messiah sent me not to immerse, but to proclaim the Good News—not in wisdom of words, so that the cross of Messiah wouldn’t be made void.
18 Maana ujumbe kuhusu kifo cha Kristo msalabani ni jambo la kipumbavu kwa wale walio katika mkumbo wa kupotea, lakini kwetu sisi tulio katika njia ya wokovu ujumbe huo ni nguvu ya Mungu.
For the word of the cross is foolishness to those who are dying, but to us who are being saved it is the power of God.
19 Maana Maandiko Matakatifu yasema: “Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, na elimu ya wataalamu nitaitupilia mbali.”
For it is written, “I will destroy the wisdom of the wise. I will bring the discernment of the discerning to nothing.”
20 Yu wapi basi, mwenye hekima? Yu wapi basi, mwalimu wa Sheria? Naye bingwa wa mabishano wa nyakati hizi yuko wapi? Mungu ameifanya hekima ya ulimwengu kuwa upumbavu. (aiōn g165)
Where is the wise? Where is the scribe? Where is the debater of this age? Hasn’t God made foolish the wisdom of this world? (aiōn g165)
21 Maana, kadiri ya hekima ya Mungu, watu hawawezi kumjua Mungu kwa njia ya hekima yao wenyewe. Badala yake, Mungu amependa kuwaokoa wale wanaoamini kwa njia ya kile ambacho wenye hekima wanakiona kuwa ni upumbavu, yaani ujumbe tunaohubiri.
For seeing that in the wisdom of God, the world through its wisdom didn’t know God, it was God’s good pleasure through the foolishness of the proclaiming to save those who believe.
22 Wayahudi wanataka ishara, na Wagiriki wanatafuta hekima;
For Jews ask for signs, Greeks seek after wisdom,
23 lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa. Kwa Wayahudi jambo hili ni kikwazo, na kwa watu wa mataifa ni upumbavu;
but we proclaim Messiah crucified, a stumbling block to Jews and foolishness to Greeks,
24 lakini kwa wale walioitwa, Wayahudi kwa Wagiriki, Kristo ni nguvu ya Mungu na hekima ya Mungu.
but to those who are called, both Jews and Greeks, Messiah is the power of God and the wisdom of God;
25 Maana kinachoonekana kuwa ni upumbavu wa Mungu, kina busara zaidi kuliko hekima ya binadamu; na kinachoonekana kuwa ni udhaifu wa Mungu, kina nguvu zaidi kuliko nguvu za binadamu.
because the foolishness of God is wiser than men, and the weakness of God is stronger than men.
26 Ndugu, kumbukeni wakati mlipoitwa: wengi wenu hawakuwa wenye hekima hata kwa fikira za binadamu; wengi hawakuwa wenye nguvu au watu wa tabaka ya juu.
For you see your calling, brothers, that not many are wise according to the flesh, not many mighty, and not many noble;
27 Ndiyo kusema, Mungu aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni upumbavu, ili awaaibishe wenye hekima; na aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni dhaifu, ili awaaibishe wenye nguvu.
but God chose the foolish things of the world that he might put to shame those who are wise. God chose the weak things of the world that he might put to shame the things that are strong.
28 Mungu ameyachagua yale ambayo kwa fikira za dunia ni mambo yaliyo duni na yanayodharauliwa, mambo ambayo hata hayakuwako, ili kwa hayo ayafutilie mbali yale ambayo kwa fikira za binadamu ni mambo ya maana.
God chose the lowly things of the world, and the things that are despised, and the things that don’t exist, that he might bring to nothing the things that exist,
29 Basi, hakuna mtu awezaye kujivunia chochote mbele ya Mungu.
that no flesh should boast before God.
30 Mungu mwenyewe ndiye aliyewaunganisha ninyi na Kristo Yesu. Mungu amemfanya Kristo awe hekima yetu; kwa njia yake sisi tunapatanishwa na Mungu, tunakuwa watu wake Mungu na kukombolewa.
Because of him, you are in Messiah Yeshua, who was made to us wisdom from God, and righteousness and sanctification, and redemption,
31 Basi, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Mwenye kutaka kujivuna, basi, na ajivunie kazi ya Bwana.”
that, as it is written, “He who boasts, let him boast in the Lord.”

< 1 Wakorintho 1 >