< 1 Wakorintho 9 >
1 Je, mimi si mtu huru? Je, mimi si mtume? Je, mimi sikumwona Yesu Bwana wetu? Je, ninyi si matokeo ya kazi yangu kwa ajili ya Bwana?
Nene si huru? Nene si mtume? Nene nsmbwene lepi Yesu Bwana watete? muenga si matunda gha mbombo ya nene katika Bwana?
2 Hata kama kwa watu wengine mimi si mtume, lakini walau kwenu ninyi mimi ni mtume. Ninyi ni uthibitisho wa mtume wangu kwa sababu ya kuungana kwenu na Bwana.
Ikiwa nene si mtume kwa bhangi angalau ni mtume kwa yhomo muenga. Kwa maana muenga ni uthibitisho wa utume wanene katika Bwana.
3 Hoja yangu kwa wale wanaonipinga ndiyo hii:
Obho ndio utetezi wanene kwa bhala bhakanichunguza nene.
4 Je, hatuna haki ya kula na kunywa?
Je tuyelepi ni haki ya kulya ni kunywa?
5 Je, hatuna ruhusa kumchukua mke Mkristo katika ziara zetu, kama vile wafanyavyo mitume wengine, ndugu zake Bwana, na pia Kefa?
Tuyelepi ni haki kutola ndala ya amini kama yakibhikheta mitume bhangi, ni bhalongo bha Bwana, ni Kefa?
6 Au ni mimi tu na Barnaba ambao tunapaswa kujipatia maslahi yetu kwa kufanya kazi?
Au ni nene namwene ni Barnaba ambavo twipasibhwa kufuanya mbombo?
7 Je, mwanajeshi gani anayelipia utumishi wake jeshini? Mkulima gani asiyekula matunda ya shamba lake la mizabibu? Mchungaji gani asiyekunywa maziwa ya mifugo yake?
Niani yaifuanya ya muene? Ni niani yaipanda mzabibu na akolokulya matunda ghaki? Au ni niani yaichunga likundi yaibela kunywa maziwa ghaki?
8 Je, nasema mambo haya kibinadamu tu? Je, Sheria nayo haisemi hivyo?
Je nijobha agha kwa mamlaka gha kibinadamu? Sheria ni yhene yijobha hee naha?
9 Imeandikwa katika Sheria ya Mose: “Usimfunge kinywa ng'ombe anapoliwata nafaka.” Je, ndio kusema Mungu anajishughulisha na ng'ombe?
Kwa ndabha iyandikibhu katika sheria ya Musa, “Kolokuikhonga ng'ombi kinywa payilya nafaka.” Ni ukueli kwamba apa K'yara ijali ng'ombi?
10 Je, hakuwa anatufikiria sisi aliposema hivyo? Naam, haya yaliandikwa kwa ajili yetu; kwani yule anayelima na yule anayevuna, wote wawili wana haki ya kutumaini kupata sehemu ya mavuno.
Au je ijobhalepi kwa ajili ya tete? ujandikibhu kwa ajili ya tete, kwa ndabha yhola yailheme nafaka yikampasa kulhema kwa matumaini, ni muene yaifuna yikampasa afunai kwa matarajio gha kushiriki mu mavuno.
11 Ikiwa sisi tumepanda mbegu ya kiroho kati yenu, je, ni jambo kubwa tukichuma kwenu faida ya kidunia?
Ikiwa twapandili fhenu fya rohoni miongoni mwayhomo, Je! Ni lisu libhaha kwa tete tukavunai fhenu fya mumbhele kuhoma kwa yhomho?
12 Ikiwa wengine wanayo haki ya kutazamia hayo kutoka kwenu, je, sisi hatuna haki zaidi kuliko hao? Lakini, sisi hatukuitumia haki hiyo, Badala yake, tumestahimili kila kitu ili tusiiwekee kizuizi chochote Habari Njema ya Kristo.
Ikiwa bhangi bhakakabhili haki eye kuhoma kwa muenga, Je! tete si zaidi? Hata naha, tukadai hee haki eye. Badala yiaki, twavumilili mambo ghoa badala ya kuya kikwazo kya injili ya Kristu.
13 Je, hamjui kwamba wanaotumikia Hekaluni hupata chakula chao Hekaluni, na kwamba wanaotolea sadaka madhabahuni hupata sehemu ya hiyo sadaka?
Mumanyili lepi ya kuwa bhoa bhabhifuanya mbombo hekaluni? bhikabha kyakulya kya bhene kuhoma hekaluni? Mumanyili lepi ya kuwa bhoa bhabhitenda mbombo madhabahuni bhikabha sehemu ya khela kakitolibhu madhabahuni?
14 Bwana aliagiza vivyo hivyo; wahubiri wa Habari Njema wapate riziki zao kutokana nayo.
Kwa jinsi eyu eyu, Bwana alaghisi ya kuwa bhoa bhoa bhabhikaitangasya injili sheriti bhakabhai kuishikutokana ni eyu injili.
15 Lakini, mimi sikutumia hata mojawapo ya haki hizo. Na wala siandiki nijipatie haki hizo; kwangu mimi ni afadhali kufa kuliko kumfanya yeyote aone kwamba najisifu bure.
Lakini nikabhadai haki sioa esu. Na niyandika hee agha ilii jambo lilyoha lhela lifuanyikai kwa ajili ya nene. Ni heri nene nifwai kuliko munu yuywoha kubatilisya khoni kujisifu kwa nene.
16 Ikiwa ninaihubiri Habari Njema, hilo si jambo la kujivunia; hilo ni jukumu nililopewa. Na, ole wangu kama sitaihubiri Habari Njema!
Maana ikiwa nihubiri injili, niyelepi ni sababu ni lazima nifuanya naha, ni ole wangu nikabelai kuhubiri injili!
17 Ningekuwa nimeichagua kazi hii kwa hiari, basi, ningetazamia malipo; lakini maadam naifanya ikiwa ni wajibu, hiyo ina maana kwamba ni jukumu nililopewa nitekeleze.
Kwa maana nikafuanyai naha kwa hiari ya nene, nuja ni thawabu. Lakini ikiwa si kwa hiari, nakhona nujele ni jukumu lanipelibhu kuya wakili.
18 Mshahara wangu ni kitu gani, basi? Mshahara wangu ni fursa ya kuihubiri Habari Njema bure, bila kudai haki ninazostahili kwa kuihubiri.
Basi thawabu yanene kiki? ya kuwa panihubiri, nilola kuipisya injili pasipo gharama ni bila kutumila kwa utimilifu wa haki ya nene yaniyenayu mu injili.
19 Kwa hiyo, ingawa mimi si mtumwa wa mtu yeyote, nimejifanya mtumwa wa kila mtu ili nimpatie Kristo watu wengi iwezekanavyo.
Maana japo niyele huru kwa bhoa, nafuanyiki mtumwa wa bhoa, ili kwamba nibhuesyai kubha kabha bhingi zaidi.
20 Kwa Wayahudi nimeishi kama Myahudi ili niwapate Wayahudi; yaani, ingawa mimi siko chini ya Sheria, nimejiweka chini ya Sheria kwao, ili niwapate hao walio chini ya Sheria.
Kwa bhayahudi wayele kama myahudi ili nikabhakabhai bhayahudi kwa bhala bhabhayele chini ya sheria nayele kama mmonga wa bhene yayele chini ya sheria ili nibhakabhai bhala bhabhayele chini ya sheria. Nafuanyili naha ingawa nene binafsi nayelepi chini ya sheria.
21 Na kwa wale walio nje ya Sheria, naishi kama wao, nje ya Sheria, ili niwapate hao walio nje ya Sheria. Hii haimaanishi kwamba mimi niko nje ya sheria ya Mungu, maana nabanwa na sheria ya Kristo.
Kwa bhala bhabhayele nje ya sheria, nayele kama mmonga wa bhene nje ya sheria, ingawa nene binafsi nayelepi nje ya sheria ya K'yara, bali chini ya sheria ya Kristu. Nafuanyili naha ili nibhakabhai bhala bhabhayele nje ya sheria.
22 Kwao walio dhaifu nimejifanya dhaifu ili niwapate hao walio dhaifu. Nimejifanya kila kitu kwa wote ili nipate kuwaokoa baadhi yao kwa kila njia.
Kwa bhayele bhanyonge, ili nayele mnyonge ili nibhakabhai bhabhayele bhanyonge. Niyele hali sioa kwa bhanu bhoa ili kwa njela syoa nikabhai kubhaokola baadhi.
23 Nafanya haya yote kwa ajili ya Habari Njema, nipate kushiriki baraka zake.
Ninene nifuanya mambo ghoa kwa ajili ya injili, ili nikabhai kushiriki katika baraka.
24 Je, hamjui kwamba katika uwanja wa michezo, ingawa wapiga mbio wote hukimbia, ni mmoja tu anayejinyakulia zawadi?
Mumanyili lepi ya kuwa mu mbio bhoa bhabhishindana bhipinga mbio, lakini yaipokela tuzo ni mmonga? Henu mkembhelai mbio ili mkabhai tuzo.
25 Wanariadha hujipa mazoezi na nidhamu kali; hufanya hivyo ili wajipatie taji iharibikayo! Lakini sisi twafanya hivyo tupate taji ya kudumu daima.
Mwana michezo kajizuila mu ghoa pauja mu mafunzo. Abhu bhifuanya naha ili bhapokelai taji yaiharibika, lakini tete twivembhela hela ili tukabhaa taji yaibela kuharibika.
26 Ndivyo basi, ninavyopiga mbio nikiwa na nia ya kushinda; ndivyo ninavyopigana, na si kama bondia anayetupa ngumi zake hewani.
Henu nene nikhembhela lepi bila sababu au ni kukomana numi kama kutobha mpongho.
27 Naupa mwili wangu mazoezi magumu na kuutia katika nidhamu kamili, nisije mimi mwenyewe nikakataliwa baada ya kuwahubiria wengine.
Lakini ikautesya mbhele wa nne ni kuufuanya kama mtumwa, ili kwamba nijapokwisha kubhahubiri bhangi, nene na muene ni kholho kuya wa kubelekilibhwa.