< 1 Wakorintho 5 >

1 Ziko habari za kuaminika kwamba kuna uzinzi miongoni mwenu; tena ni uzinzi mbaya ambao haujapata kuwako hata kati ya watu wasiomjua Mungu. Nimeambiwa eti mmoja wenu anaishi na mke wa baba yake!
It is actually reported that there is fornication among you, a kind of fornication that is not even named among the Gentiles, for a man has his father's wife.
2 Mnawezaje kujivuna? Ingekuwa afadhali kwenu kuomboleza, na huyo aliyefanya kitu hicho aondolewe miongoni mwenu.
And you are puffed up! You should have mourned instead and removed the man who did this from among you.
3 Nami, kwa upande wangu, ingawa kwa mwili niko mbali nanyi, hata hivyo kwa roho niko hapo pamoja nanyi: na hivyo, kama vile nipo hapo, nimekwisha mhukumu huyo aliyefanya jambo hilo la aibu.
For though I am absent in body, I am present in spirit. And I have already judged the man who did this, just as though I were present.
4 Wakati mnapokusanyika pamoja kwa jina la Bwana Yesu, nami nikiwa pamoja nanyi kwa roho, basi, kwa uwezo wa Bwana wetu Yesu,
So when you are gathered together in the name of our Lord Jesus Christ and I am with you in spirit, along with the power of our Lord Jesus Christ,
5 mkabidhini mtu huyo kwa Shetani ili mwili wake uharibiwe na roho yake iweze kuokolewa Siku ile ya Bwana.
hand this man over to Satan for the destruction of his flesh, so that his spirit may be saved in the day of the Lord Jesus.
6 Majivuno yenu hayafai! Je, hamjui kwamba chachu kidogo huchachusha donge lote la unga?
Your boasting is not good. Do you not know that a little leaven leavens the whole lump?
7 Jitakaseni, mkatupe mbali chachu ya kale ili mpate kuwa donge jipya lisilotiwa chachu kama mnavyopaswa kuwa; maana, Kristo, Pasaka yetu, amekwisha tolewa tambiko.
Purge out the old leaven so that you may be a new lump of dough, since you really are unleavened. For Christ, our Passover lamb, has been sacrificed for us.
8 Basi, tufanye karamu hiyo si kwa chachu ile ya kale, chachu ya ubaya na uovu, bali kwa mkate usiotiwa chachu, mkate wa usafi na kweli.
So then, let us celebrate the feast, not with old leaven, nor with the leaven of malice and evil, but with the unleavened bread of sincerity and truth.
9 Niliwaandikia katika barua yangu msishirikiane na wazinzi.
I wrote to you in my letter not to associate with fornicators.
10 Ukweli ni kwamba sikuwa na maana ya watu wote duniani walio wazinzi, wachoyo, walaghai na wenye kuabudu sanamu. Maana, ili kuwaepa hao wote ingewalazimu ninyi kuihama dunia hii kabisa!
Yet I certainly did not mean the fornicators of this world or the greedy or swindlers or idolaters, since you would then need to go out of the world.
11 Nilichoandika ni hiki: msishirikiane na ndugu Mkristo aliye mzinzi, mchoyo, mwenye kuabudu sanamu, mchongezi mlevi na mlaghai. Mtu wa namna hiyo, hata kula msile naye.
But now I am writing to you not to associate with anyone who is named as a brother if he is a fornicator or greedy, an idolater or a reviler, a drunkard or a swindler; do not even eat with such a man.
12 Je, ni shauri langu kuwahukumu watu walio nje? Hao Mungu atawahukumu. Je, ninyi hampaswi kuwahukumu wale walio katika jamii yenu ninyi wenyewe?
For what have I to do with judging those who are outside the church? Do you not judge those who are inside the church?
13 Mfukuzeni mbali nanyi huyo mwovu!
God will judge those who are outside the church. “Therefore you must remove the evil person from among you.”

< 1 Wakorintho 5 >