< 1 Wakorintho 3 >
1 Ndugu, mimi sikuweza kusema nanyi kama watu mlio na huyo Roho. Nilipaswa kusema nanyi kama watu wa kidunia, kama watoto wachanga katika maisha ya Kikristo.
所以,弟兄們,我從前對你們說話,還不能把你們當作神的人,只能當作屬血肉的人,當作在基督內的嬰孩。
2 Ilinibidi kuwalisheni kwa maziwa, na si kwa chakula kigumu, kwani hamkuwa tayari kukipokea. Hata sasa hamko tayari.
我給你們喝的是奶,並非飯食,那時你們不能吃.就是如今你們還不能,
3 Maana bado mu watu wa kidunia. Je, si kweli kwamba bado uko wivu na magombano kati yenu? Mambo hayo yanaonyesha wazi kwamba ninyi bado ni watu wa kidunia, mnaishi mtindo wa kidunia.
你們還是屬血肉的人。你們中既有嫉妒和紛爭,你們豈還不是屬血肉的人,按照俗人的樣子行事嗎?
4 Mmoja wenu anaposema, “Mimi ni wa Paulo”, na mwingine, “Mimi ni wa Apolo”, je, hiyo haionyeshi kwamba mnaishi bado kama watu wa dunia hii tu?
這人說:「我是屬保祿,」那人說:「我是屬阿頗羅,」這樣,你們豈不是成了俗人嗎?
5 Apolo ni nani? na Paulo ni nani? Sisi ni watumishi tu ambao tuliwaleteeni ninyi imani. Kila mmoja wetu anafanya kazi aliyopewa na Bwana.
其實,阿頗羅算什麼?保祿算什麼?不過只是僕役,使你們獲得信仰,每人按照主所指派的而工作:
6 Mimi nilipanda mbegu, Apolo akamwagilia maji; lakini aliyeiotesha mbegu ni Mungu.
我栽種,阿頗羅澆灌,然而使之生長的,卻是天主。
7 Wa maana si yule aliyepanda mbegu, au yule aliyemwagilia maji; wa maana ni Mungu aliyeiwezesha mbegu kuota.
可見栽種的不算什麼,澆灌的也不算什麼,只在那使之生長的天主。
8 Yule aliyepanda na yule aliyemwagilia maji wote ni sawa, ingawa kila mmoja atapokea tuzo lake kufuatana na jitihada yake mwenyewe.
所以栽種的和澆灌的原是一事,不過各人將要按各人的勞苦領受自己的賞報。
9 Maana sisi ni ndugu, wafanyakazi pamoja na Mungu; na ninyi ni shamba lake; ninyi ni jengo lake.
我們原是天主的助手,你們是天主的莊田,是天主的建築物。
10 Kwa msaada wa neema aliyonipa Mungu, nimefaulu, kama mwashi stadi mwenye busara, kuweka msingi ambao juu yake mtu mwingine anajenga. Basi, kila mmoja awe mwangalifu jinsi anavyojenga juu yake.
按照天主所賜給我恩寵,我好像一個精明的建築師,奠立了根基,其他的人上面建築;但是各人應該注意怎麼在上面建築,
11 Hakuna mtu awezaye kuweka msingi mwingine badala ya ule uliokwisha wekwa, yaani Yesu Kristo.
因為除已奠立了的根基,即耶穌基督外,任何人不能再建立別的根基。
12 Juu ya msingi huo mtu anaweza kujenga kwa dhahabu, fedha au mawe ya thamani; anaweza kutumia miti, majani au nyasi.
人可用金、銀、寶石、木、草、禾皆,在這根基上建築,
13 Iwe iwavyo, ubora wa kazi ya kila mmoja utaonekana wakati Siku ile ya Kristo itakapoifichua. Maana, Siku hiyo itatokea na moto, na huo moto utaipima na kuonyesha ubora wake.
各人的工程將來終必顯露出來,因為主的日子要把它揭露出來;原來主的日子在火中出現,這火要試驗各人的工程怎麼。
14 Ikiwa alichojenga mtu juu ya huo msingi kitaustahimili huo moto, atapokea tuzo;
在那根基上所建築的工程,若存得住,他必要獲得賞報;
15 lakini kama alichojenga kitaunguzwa, basi, atapoteza tuzo lake; lakini yeye mwenyewe ataokolewa kana kwamba ameponyoka kutoka motoni.
但誰的工程若被焚了,他就要受到損失,自己固然可得救,可是仍像火中經過一樣。
16 Je, hamjui kwamba ninyi ni hekalu la Mungu, na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
你們知道,你們是天主的宮殿,天主聖神住你們內嗎?
17 Basi, mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu; maana hekalu la Mungu ni takatifu, na hekalu hilo ni ninyi wenyewe.
誰若毀壞天主的宮殿,天主必要毀滅壞他,因為天主的宮殿是聖的,這宮殿就是你們。
18 Msijidanganye! Mtu yeyote miongoni mwenu akijidhania mwenye hekima mtindo wa kidunia, heri awe mjinga kusudi apate kuwa na hekima ya kweli. (aiōn )
誰也不要自歟:你們中若有人在今世自以為是有智慧的人,該變為一個愚昧的人,為成一個有智慧的人, (aiōn )
19 Maana, hekima ya kidunia ni upumbavu mbele ya Mungu. Kwani Maandiko Matakatifu yasema: “Mungu huwanasa wenye hekima katika ujanja wao.”
因為這世界的智慧在天主前原是愚昧。經上記載說:『祂以智者的計謀捕捉智者;』
20 Na tena: “Bwana ajua kwamba mawazo ya wenye hekima hayafai.”
又說:『上主認透智者的思念,原來都是虛幻。
21 Basi, mtu asijivunie watu. Maana kila kitu ni chenu.
所以,誰也不可拿人來誇口,因為一切都是你們的:
22 Paulo, Apolo na Kefa, ulimwengu, maisha na kifo; mambo ya sasa na ya baadaye, yote ni yenu.
無論是保祿,或是阿頗羅,或是刻法,或是世界,或是生命,或是死亡,或是現在,或是將來,一切都是的;
23 Lakini ninyi ni wa Kristo naye Kristo ni wa Mungu.
你們卻是基督的,而基督是天主的。