< 1 Wakorintho 2 >
1 Ndugu, mimi nilipokuja kwenu sikuwahubiria siri ya ujumbe wa Mungu kwa ufasaha wa lugha, au kwa hekima ya binadamu.
When I came to you, brothers, I did not come proclaiming to you the testimony of God with lofty speech or wisdom.
2 Nilipokuwa kwenu niliamua kutojua chochote kile isipokuwa tu kumjua Yesu Kristo; naam, Kristo aliyesulubiwa.
For I resolved to know nothing among you except Jesus Christ and him crucified.
3 Nilipokuwa kwenu nilikuwa dhaifu, natetemeka kwa hofu nyingi.
I came to you in weakness and fear, and with much trembling.
4 Hotuba zangu na mahubiri yangu sikuyatoa kwa maneno ya kuvutia na ya hekima, bali kwa uthibitisho mwingi na nguvu ya Roho.
And my word and my preaching were not with persuasive words of human wisdom, but with a demonstration of the Spirit and of power,
5 Nilifanya hivyo kusudi imani yenu ipate kutegemea nguvu ya Mungu, na si hekima ya binadamu.
so that your faith would not be based on the wisdom of men, but on the power of God.
6 Hata hivyo, sisi tunatumia lugha ya hekima kwa wale waliokomaa kiroho; lakini hekima hiyo si ya hapa duniani, wala si ya watawala wa dunia hii ambao wako katika mkumbo wa kupotea. (aiōn )
Now we speak wisdom among the mature, but not a wisdom of this age or of the rulers of this age, who are being brought to nothing. (aiōn )
7 Hekima tunayotumia ni hekima ya siri ya Mungu, hekima iliyofichika, ambayo Mungu aliiazimia tangu mwanzo kwa ajili ya utukufu wetu. (aiōn )
On the contrary, we speak the hidden wisdom of God in a mystery, which God foreordained for our glory before time began. (aiōn )
8 Ni hekima ambayo watawala wa dunia hii hawakuielewa; maana wangalielewa, hawangalimsulubisha Bwana wa utukufu. (aiōn )
None of the rulers of this age understood this wisdom, for if they had understood it, they would not have crucified the Lord of glory. (aiōn )
9 Lakini, ni kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Mambo ambayo jicho halijapata kuyaona wala sikio kuyasikia, mambo ambayo binadamu hajapata kuyafikiria moyoni, hayo ndiyo Mungu aliyowatayarishia wale wampendao.”
But, as it is written, “No eye has seen, no ear has heard, and no heart has imagined what God has prepared for those who love him.”
10 Hayo ndiyo mambo Mungu aliyotufunulia kwa njia ya Roho wake. Maana Roho huchunguza kila kitu hata mambo ya ndani kabisa ya Mungu.
Now God has revealed these things to us through his Spirit. For the Spirit searches everything, even the depths of God.
11 Nani awezaye kujua mambo ya ndani ya mtu isipokuwa roho yake mtu huyo? Hali kadhalika, hakuna ajuaye mambo ya Mungu isipokuwa Roho wa Mungu.
For who among men knows the thoughts of a man except the man's spirit within him? In the same way, no one knows the thoughts of God except the Spirit of God.
12 Sasa sisi hatukuipokea roho ya ulimwengu, bali tumepokea Roho atokaye kwa Mungu ili atuwezeshe kujua yale tuliyojaliwa na Mungu.
Now we did not receive the spirit of the world, but the Spirit who is from God, so that we might understand what God has freely given us.
13 Basi sisi twafundisha, si kwa maneno tuliyofundishwa kwa hekima ya binadamu, bali kwa maneno tuliyofundishwa na Roho, tukifafanua mambo ya kiroho kwa walio na huyo Roho.
We speak about this, not with words taught by human wisdom but with words taught by the Holy Spirit, interpreting spiritual things to spiritual people.
14 Mtu wa kidunia hapokei mambo ya Roho wa Mungu. Kwake mtu huyo mambo hayo ni upumbavu mtupu; yanapita akili yake; maana yanaweza tu kutambuliwa kwa msaada wa Roho.
The natural man does not accept what comes from the Spirit of God, because it is foolishness to him; he is not able to understand it because it is spiritually discerned.
15 Lakini mtu aliye na huyo Roho anaweza kubainisha ubora wa kila kitu, naye mwenyewe hahukumiwi na mtu mwingine.
But he who is spiritual makes judgments about all things, and yet he himself is not subject to any man's judgment.
16 Maandiko yasema: “Nani awezaye kuifahamu akili ya Bwana? Nani awezaye kumshauri?” Lakini sisi tunayo akili ya Kristo.
“For who has known the mind of the Lord so as to advise him?” But we have the mind of Christ.