< 1 Wakorintho 15 >

1 Sasa ndugu, napenda kuwakumbusha ile Habari Njema niliyowahubirieni nanyi mkaipokea na kusimama imara ndani yake.
Now, brothers, I want to add information to the Gospel that I proclaimed to you, that you also received, and in which you stand;
2 Kwa njia yake mnaokolewa, ikiwa mnayazingatia maneno niliyowahubirieni, na kama kuamini kwenu hakukuwa bure.
through which also you are saved, if you hold fast that word that I proclaimed to you—unless you believed in vain.
3 Mimi niliwakabidhi ninyi mambo muhimu sana ambayo mimi niliyapokea: kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na Maandiko Matakatifu;
Because I transmitted to you at first that which I also received: that Christ died for our sins according to the Scriptures,
4 kwamba alizikwa, akafufuka siku ya tatu kama ilivyoandikwa;
and that He was buried, and that He was raised on the third day according to the Scriptures,
5 kwamba alimtokea Kefa, na baadaye aliwatokea wale kumi na wawili.
and that He was seen by Cephas, then by the Twelve.
6 Kisha aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano kwa mara moja; wengi wao wanaishi bado, lakini baadhi yao wamekwisha kufa.
After that He was seen by over five hundred brothers at once, most of whom are still living, while some have fallen asleep.
7 Baadaye alimtokea Yakobo kisha akawatokea mitume wote.
After that He was seen by James, then by all the apostles.
8 Baada ya wote, akanitokea hata mimi, mimi niliyekuwa kama mtu aliyezaliwa kabla ya wakati.
And last of all He was seen by me also, like one born out of season.
9 Maana mimi ni mdogo kabisa miongoni mwa mitume na wala sistahili kuitwa mtume, kwa sababu nililidhulumu kanisa la Mungu.
For I am the least of the apostles, who am not worthy to be called an apostle, because I persecuted the Church of God.
10 Lakini, kwa neema yake Mungu, nimekuwa kama nilivyo. Na neema yake kwangu haikuwa bure. Mimi nimefanya kazi kuliko wote; si mimi hasa, ila ni neema ya Mungu ifanyayo kazi pamoja nami.
But by the grace of God I am what I am, and His grace toward me has not been in vain; in fact, I have worked harder than all of them—well, not I, but the grace of God that was with me.
11 Lakini hata hivyo, iwe wao ndio wahubirio au mimi nihubiriye, haidhuru, hiki ndicho tunachuhubiri, na hiki ndicho mnachoamini.
So whether it was I or they, thus we preached and thus you believed.
12 Sasa, maadam inahubiriwa kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, baadhi yenu wanawezaje kusema kwamba hakuna ufufuo wa wafu?
Now if Christ is being proclaimed as having been raised from among the dead, how can some among you say that there is no resurrection of the dead?
13 Kama hakuna ufufuo wa wafu, basi, Kristo naye hakufufuka;
If there is no resurrection of the dead, not even Christ has been raised.
14 na kama Kristo hakufufuka, basi mahubiri yetu hayana maana na imani yenu haina maana.
And if Christ has not been raised, then our preaching is empty, and so is your faith!
15 Zaidi ya hayo sisi tungekuwa mashahidi wa uongo mbele ya Mungu, maana tulisema kwamba Mungu alimfufua Kristo kutoka wafu na kumbe yeye hakumfufua—kama ni kweli kwamba wafu hawafufuliwi.
Further, we are even discovered to be false witnesses of God, because we have testified about God that He raised the Christ, whom He did not raise, if in fact the dead are not raised.
16 Maana, ikiwa ni kweli kwamba wafu hawafufuki, basi naye Kristo hakufufuka.
For if no dead are raised, neither has Christ been raised.
17 Na kama Kristo hakufufuliwa, basi, imani yenu ni ya bure; mngali bado katika dhambi zenu.
And if Christ has not been raised, your faith is useless; you are still in your sins.
18 Zaidi ya hayo, wale wote waliokufa wakiwa wameungana na Kristo wamepotea kabisa.
Then those also who have fallen asleep in Christ are lost.
19 Kama matumaini yetu katika Kristo yanahusu tu maisha haya ya sasa, basi, sisi ni watu wa kusikitikiwa zaidi kuliko wengine wote duniani.
If it is only for this life that we have hoped in Christ, we are of all men most pitiable.
20 Lakini ukweli ni kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, limbuko lao wale waliolala katika kifo.
But indeed, Christ has been raised from the dead; He became the firstfruits of those who have fallen asleep.
21 Maana kama vile kifo kilivyoletwa duniani na mtu mmoja, vivyo hivyo nako kufufuka kutoka wafu kumesababishwa na mtu mmoja.
For since death came through a man, resurrection of the dead also came through a man.
22 Kama vile watu wote wanavyokufa kwa kujiunga na Adamu, vivyo hivyo wote watafufuliwa kwa kuungana na Kristo.
For as all in Adam are dying, so also all in the Christ will be made alive.
23 Lakini kila mmoja kwa mpango wake: Kristo kwanza, halafu wale walio wake Kristo wakati Kristo atakapokuja.
But each one in his own order: Christ the firstfruits, then those who belong to Christ at His coming;
24 Baada ya hayo, mwisho utafika wakati ambapo Kristo atamkabidhi Mungu Baba Utawala, baada ya kufutilia mbali kila tawala na mamlaka na nguvu.
then the end, when He hands over the Kingdom to the God and Father, whenever He puts an end to every ruler and all authority and power.
25 Maana Kristo sharti atawale mpaka Mungu atakapowashinda adui zake na kuwaweka chini ya miguu yake.
Because it is necessary that He reign until He has put all the enemies under His feet.
26 Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni kifo.
The last enemy that will be destroyed is death.
27 Maana, Maandiko yasema: “Mungu ameweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Lakini, Maandiko yanaposema: “Vitu vyote vimewekwa chini ya miguu yake avitawale” ni dhahiri kwamba Mungu haingii katika kundi hilo la vitu, maana yeye ndiye anayeviweka vitu hivyo chini ya Kristo.
For “He has put all things under His feet.” But when it says that all things have been subordinated, it is obvious that He who put all things under Him is excepted.
28 Lakini vitu vyote vitakapowekwa chini ya Utawala wa Kristo, ndipo naye Mwana atakapojiweka chini ya Mungu, aliyeweka vyote chini ya Utawala wake; ili Mungu atawale juu ya vyote.
Now whenever all things have been subjected to Him, then the Son Himself will also be subjected to Him who subjected all things to Him, so that God may be all in all.
29 Kama hakuna ufufuo, je watu wale wanaobatizwa kwa ajili ya wafu wanatumainia kupata nini? Kama wafu hawafufuliwi, ya nini kubatizwa kwa ajili yao?
Otherwise, what will they do who are being baptized in place of the dead? If the dead are not raised at all, just why are they being baptized in the place of the dead?
30 Na sisi, ya nini kujitia hatarini kila saa?
And why do we face danger every hour?
31 Ndugu, mimi nakikabili kifo kila siku! Fahari niliyo nayo juu yenu katika kuungana na Kristo Yesu Bwana wetu inanifanya nitangaze jambo hili.
I die every day—so I affirm by the boasting about you that I have in Christ Jesus our Lord.
32 Kama kusudi langu lingalikuwa la kibinadamu tu, kule kupigana kwangu na wanyama wakali hapa Efeso kungalinifaa kitu gani? Kama wafu hawafufuki, basi, “Tule na tunywe, maana kesho tutakufa.”
If I fought human ‘animals’ in Ephesus, what did I gain? If the dead are not raised, “Let us eat and drink, for tomorrow we die!”
33 Msidanganyike! Urafiki mbaya huharibu tabia njema.
Stop kidding yourselves: evil associations corrupt good habits.
34 Amkeni! Anzeni kuishi vema, na acheni kutenda dhambi. Baadhi yenu hawamjui Mungu kabisa. Hii nawaambieni, ni aibu kubwa kwenu!
Sober up righteously, and stop sinning, for some have no knowledge of God. I say this to your shame.
35 Lakini mtu anaweza kuuliza: “Wafu watafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani wakati watakapokuja tena?”
But someone will say, “How are the dead raised? With what kind of body do they come?”
36 Hayo ni maswali ya kijinga! Ukipanda mbegu, isipokufa kwanza haitaota.
Ignorant, what you plant is not brought to life unless it dies.
37 Unachopanda ni mbegu tu, labda ya ngano au nafaka nyingine, na si mmea mzima ambao hutokea baadaye.
And what you plant is a bare seed (perhaps of wheat or some one of the others); you do not plant the body that it will become.
38 Mungu huipa hiyo mbegu mwili anaoutaka mwenyewe; kila mbegu hupata mwili wake wa pekee.
But God gives it a body just as He determined, to each of the seeds its own body.
39 Miili ya viumbe vyote si sawa. Miili ya binadamu ni ya namna moja, ya wanyama ni ya namna nyingine, ya ndege ni ya namna nyingine na miili ya samaki pia ni ya namna nyingine.
All flesh is not the same flesh: that of humans is one kind, and the flesh of animals is another, that of fish is another, that of birds is yet another.
40 Iko miili ya mbinguni na miili ya duniani; uzuri wa miili ya mbinguni ni mwingine, na na uzuri wa miili ya duniani ni mwingine.
There are also celestial bodies and terrestrial bodies; but the glory of the heavenly is one, while that of the earthly is another.
41 Uko uzuri wa jua, wa mwezi na wa nyota; hata nyota nazo huhitilafiana kwa uzuri.
There is one splendor of the sun, another splendor of the moon, and another splendor of the stars; and star differs from star in brightness.
42 Ndivyo ilivyo kuhusu ufufuo wa wafu. Kama vile mbegu, mwili huzikwa ardhini ukiwa katika hali ya kuharibika, lakini hufufuliwa katika hali ya kutoharibika.
The resurrection of the dead is like that: the body is ‘planted’ in deterioration and it is raised in incorruptibility;
43 Huzikwa katika hali duni, hufufuliwa katika hali tukufu; huzikwa katika hali dhaifu, hufufuliwa ukiwa wenye nguvu.
it is ‘planted’ in dishonor and it is raised in glory; it is ‘planted’ in weakness and it is raised in power;
44 Unapozikwa ni mwili wa kawaida, unapofufuliwa ni mwili wa kiroho. Kuna mwili wa kawaida na kutakuwa na mwili wa kiroho.
it is ‘planted’ a natural body and it is raised a spiritual body. There is a natural body and there is a spiritual body.
45 Maana Maandiko yasema: “Mtu wa kwanza, Adamu, alikuwa kiumbe mwenye uhai;” lakini adamu wa mwisho ni Roho awapaye watu uzima.
So also it is written: “The first man, Adam, became a living being”; the last Adam became a life-giving spirit.
46 Lakini unaotangulia kuwako si ule mwili wa kiroho, ila ule mwili wa kawaida kisha ule mwili wa kiroho.
However, the spiritual is not first, but the natural, and then the spiritual.
47 Adamu wa kwanza aliumbwa kwa udongo, alitoka ardhini; mtu wa pili alitoka mbinguni.
The first man was of the earth, of soil; the second man was the Lord from heaven.
48 Wote walio wa dunia wako kama huyo mtu aliyeumbwa kwa udongo; wale walio wa mbinguni wako kama yule aliyetoka mbinguni.
As was the earth-man, just so are the earth-people; and as was the heaven-man, just so are the heaven-people.
49 Kama vile tulivyofanana na yule aliyeumbwa kwa udongo, vivyo hivyo tutafanana na huyohuyo aliyetoka mbinguni.
And just as we have borne the image of the earth-man, we should also bear the image of the heaven-man.
50 Basi, ndugu, nasema hivi: kile kilichofanywa kwa mwili na damu hakiwezi kuushiriki Ufalme wa Mungu; na chenye kuharibika hakiwezi kuwa na hali ya kutoharibika.
Now this I say, brothers, that flesh and blood cannot inherit the Kingdom of God; neither will deterioration inherit incorruptibility.
51 Sikilizeni, nawaambieni siri: sisi hatutakufa sote, ila sote tutageuzwa
And now, I tell you a mystery: we will not all sleep, but we will all be changed
52 wakati wa mbiu ya mwisho, kwa nukta moja, kufumba na kufumbua. Maana mbiu itakapolia, wafu watafufuliwa katika hali ya kutoweza kufa tena, na sisi tutageuzwa.
—in a split second, in an eye twinkle, at the last trumpet—the trumpet will blast and the dead will be raised incorruptible, and we will be changed.
53 Maana ni lazima kila kiharibikacho kijivalie hali ya kutoharibika, mwili uwezao kufa ujivalie hali ya kutokufa.
Because this corruptible must put on incorruption, and this mortal put on immortality.
54 Basi, mwili huu wenye kuharibika utakapojivalia hali ya kutoharibika, na kile chenye kufa kitakapojivalia hali ya kutokufa, hapo ndipo litakapotimia lile neno lililoandikwa: “Kifo kimeangamizwa ushindi umekamilika!”
So whenever this corruptible puts on incorruption and this mortal puts on immortality, then this written word will happen: “Death has been swallowed down into victory.”
55 “Kifo, ushindi wako uko wapi? Uwezo wako wa kuumiza uko wapi?” (Hadēs g86)
“Where, O Death, is your sting? Where, O Hades, is your victory?” (Hadēs g86)
56 Ukali wa kifo hutokana na dhambi, nayo dhambi hupata nguvu yake katika Sheria.
The stinger of death is sin, and the adjunct of sin is the law.
57 Lakini tumshukuru Mungu anayetupatia ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
Now thanks be to God who gives us the victory through our Lord Jesus Christ!
58 Basi, ndugu zangu wapenzi, simameni imara na thabiti. Endeleeni daima kuwa na bidii katika kazi ya Bwana, mkijua kwamba kazi mnayofanya katika utumishi wa Bwana haitapotea bure.
So then, my dear brothers, be steadfast, immovable, always abounding in the work of the Lord, knowing that your labor is not in vain in the Lord.

< 1 Wakorintho 15 >