< 1 Wakorintho 15 >

1 Sasa ndugu, napenda kuwakumbusha ile Habari Njema niliyowahubirieni nanyi mkaipokea na kusimama imara ndani yake.
Now, brothers, I want to remind you of the gospel I preached to you, which you received, and in which you stand firm.
2 Kwa njia yake mnaokolewa, ikiwa mnayazingatia maneno niliyowahubirieni, na kama kuamini kwenu hakukuwa bure.
By this gospel you are saved, if you hold firmly to the word I preached to you. Otherwise, you have believed in vain.
3 Mimi niliwakabidhi ninyi mambo muhimu sana ambayo mimi niliyapokea: kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na Maandiko Matakatifu;
For what I received I passed on to you as of first importance: that Christ died for our sins according to the Scriptures,
4 kwamba alizikwa, akafufuka siku ya tatu kama ilivyoandikwa;
that He was buried, that He was raised on the third day according to the Scriptures,
5 kwamba alimtokea Kefa, na baadaye aliwatokea wale kumi na wawili.
and that He appeared to Cephas and then to the Twelve.
6 Kisha aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano kwa mara moja; wengi wao wanaishi bado, lakini baadhi yao wamekwisha kufa.
After that, He appeared to more than five hundred brothers at once, most of whom are still living, though some have fallen asleep.
7 Baadaye alimtokea Yakobo kisha akawatokea mitume wote.
Then He appeared to James, then to all the apostles.
8 Baada ya wote, akanitokea hata mimi, mimi niliyekuwa kama mtu aliyezaliwa kabla ya wakati.
And last of all He appeared to me also, as to one of untimely birth.
9 Maana mimi ni mdogo kabisa miongoni mwa mitume na wala sistahili kuitwa mtume, kwa sababu nililidhulumu kanisa la Mungu.
For I am the least of the apostles and am unworthy to be called an apostle, because I persecuted the church of God.
10 Lakini, kwa neema yake Mungu, nimekuwa kama nilivyo. Na neema yake kwangu haikuwa bure. Mimi nimefanya kazi kuliko wote; si mimi hasa, ila ni neema ya Mungu ifanyayo kazi pamoja nami.
But by the grace of God I am what I am, and His grace to me was not in vain. No, I worked harder than all of them—yet not I, but the grace of God that was with me.
11 Lakini hata hivyo, iwe wao ndio wahubirio au mimi nihubiriye, haidhuru, hiki ndicho tunachuhubiri, na hiki ndicho mnachoamini.
Whether, then, it was I or they, this is what we preach, and this is what you believed.
12 Sasa, maadam inahubiriwa kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, baadhi yenu wanawezaje kusema kwamba hakuna ufufuo wa wafu?
But if it is preached that Christ has been raised from the dead, how can some of you say that there is no resurrection of the dead?
13 Kama hakuna ufufuo wa wafu, basi, Kristo naye hakufufuka;
If there is no resurrection of the dead, then not even Christ has been raised.
14 na kama Kristo hakufufuka, basi mahubiri yetu hayana maana na imani yenu haina maana.
And if Christ has not been raised, our preaching is worthless, and so is your faith.
15 Zaidi ya hayo sisi tungekuwa mashahidi wa uongo mbele ya Mungu, maana tulisema kwamba Mungu alimfufua Kristo kutoka wafu na kumbe yeye hakumfufua—kama ni kweli kwamba wafu hawafufuliwi.
In that case, we are also exposed as false witnesses about God. For we have testified about God that He raised Christ from the dead, but He did not raise Him if in fact the dead are not raised.
16 Maana, ikiwa ni kweli kwamba wafu hawafufuki, basi naye Kristo hakufufuka.
For if the dead are not raised, then not even Christ has been raised.
17 Na kama Kristo hakufufuliwa, basi, imani yenu ni ya bure; mngali bado katika dhambi zenu.
And if Christ has not been raised, your faith is futile; you are still in your sins.
18 Zaidi ya hayo, wale wote waliokufa wakiwa wameungana na Kristo wamepotea kabisa.
Then those also who have fallen asleep in Christ have perished.
19 Kama matumaini yetu katika Kristo yanahusu tu maisha haya ya sasa, basi, sisi ni watu wa kusikitikiwa zaidi kuliko wengine wote duniani.
If our hope in Christ is for this life alone, we are to be pitied more than all men.
20 Lakini ukweli ni kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, limbuko lao wale waliolala katika kifo.
But Christ has indeed been raised from the dead, the firstfruits of those who have fallen asleep.
21 Maana kama vile kifo kilivyoletwa duniani na mtu mmoja, vivyo hivyo nako kufufuka kutoka wafu kumesababishwa na mtu mmoja.
For since death came through a man, the resurrection of the dead comes also through a man.
22 Kama vile watu wote wanavyokufa kwa kujiunga na Adamu, vivyo hivyo wote watafufuliwa kwa kuungana na Kristo.
For as in Adam all die, so in Christ all will be made alive.
23 Lakini kila mmoja kwa mpango wake: Kristo kwanza, halafu wale walio wake Kristo wakati Kristo atakapokuja.
But each in his own turn: Christ the firstfruits; then at His coming, those who belong to Him.
24 Baada ya hayo, mwisho utafika wakati ambapo Kristo atamkabidhi Mungu Baba Utawala, baada ya kufutilia mbali kila tawala na mamlaka na nguvu.
Then the end will come, when He hands over the kingdom to God the Father after He has destroyed all dominion, authority, and power.
25 Maana Kristo sharti atawale mpaka Mungu atakapowashinda adui zake na kuwaweka chini ya miguu yake.
For He must reign until He has put all His enemies under His feet.
26 Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni kifo.
The last enemy to be destroyed is death.
27 Maana, Maandiko yasema: “Mungu ameweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Lakini, Maandiko yanaposema: “Vitu vyote vimewekwa chini ya miguu yake avitawale” ni dhahiri kwamba Mungu haingii katika kundi hilo la vitu, maana yeye ndiye anayeviweka vitu hivyo chini ya Kristo.
For “God has put everything under His feet.” Now when it says that everything has been put under Him, this clearly does not include the One who put everything under Him.
28 Lakini vitu vyote vitakapowekwa chini ya Utawala wa Kristo, ndipo naye Mwana atakapojiweka chini ya Mungu, aliyeweka vyote chini ya Utawala wake; ili Mungu atawale juu ya vyote.
And when all things have been subjected to Him, then the Son Himself will be made subject to Him who put all things under Him, so that God may be all in all.
29 Kama hakuna ufufuo, je watu wale wanaobatizwa kwa ajili ya wafu wanatumainia kupata nini? Kama wafu hawafufuliwi, ya nini kubatizwa kwa ajili yao?
If these things are not so, what will those do who are baptized for the dead? If the dead are not raised at all, why are people baptized for them?
30 Na sisi, ya nini kujitia hatarini kila saa?
And why do we endanger ourselves every hour?
31 Ndugu, mimi nakikabili kifo kila siku! Fahari niliyo nayo juu yenu katika kuungana na Kristo Yesu Bwana wetu inanifanya nitangaze jambo hili.
I face death every day, brothers, as surely as I boast about you in Christ Jesus our Lord.
32 Kama kusudi langu lingalikuwa la kibinadamu tu, kule kupigana kwangu na wanyama wakali hapa Efeso kungalinifaa kitu gani? Kama wafu hawafufuki, basi, “Tule na tunywe, maana kesho tutakufa.”
If I fought wild beasts in Ephesus for human motives, what did I gain? If the dead are not raised, “Let us eat and drink, for tomorrow we die.”
33 Msidanganyike! Urafiki mbaya huharibu tabia njema.
Do not be deceived: “Bad company corrupts good character.”
34 Amkeni! Anzeni kuishi vema, na acheni kutenda dhambi. Baadhi yenu hawamjui Mungu kabisa. Hii nawaambieni, ni aibu kubwa kwenu!
Sober up as you ought, and stop sinning; for some of you are ignorant of God. I say this to your shame.
35 Lakini mtu anaweza kuuliza: “Wafu watafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani wakati watakapokuja tena?”
But someone will ask, “How are the dead raised? With what kind of body will they come?”
36 Hayo ni maswali ya kijinga! Ukipanda mbegu, isipokufa kwanza haitaota.
You fool! What you sow does not come to life unless it dies.
37 Unachopanda ni mbegu tu, labda ya ngano au nafaka nyingine, na si mmea mzima ambao hutokea baadaye.
And what you sow is not the body that will be, but just a seed, perhaps of wheat or something else.
38 Mungu huipa hiyo mbegu mwili anaoutaka mwenyewe; kila mbegu hupata mwili wake wa pekee.
But God gives it a body as He has designed, and to each kind of seed He gives its own body.
39 Miili ya viumbe vyote si sawa. Miili ya binadamu ni ya namna moja, ya wanyama ni ya namna nyingine, ya ndege ni ya namna nyingine na miili ya samaki pia ni ya namna nyingine.
Not all flesh is the same: Men have one kind of flesh, animals have another, birds another, and fish another.
40 Iko miili ya mbinguni na miili ya duniani; uzuri wa miili ya mbinguni ni mwingine, na na uzuri wa miili ya duniani ni mwingine.
There are also heavenly bodies and earthly bodies. But the splendor of the heavenly bodies is of one degree, and the splendor of the earthly bodies is of another.
41 Uko uzuri wa jua, wa mwezi na wa nyota; hata nyota nazo huhitilafiana kwa uzuri.
The sun has one degree of splendor, the moon another, and the stars another; and star differs from star in splendor.
42 Ndivyo ilivyo kuhusu ufufuo wa wafu. Kama vile mbegu, mwili huzikwa ardhini ukiwa katika hali ya kuharibika, lakini hufufuliwa katika hali ya kutoharibika.
So will it be with the resurrection of the dead: What is sown is perishable; it is raised imperishable.
43 Huzikwa katika hali duni, hufufuliwa katika hali tukufu; huzikwa katika hali dhaifu, hufufuliwa ukiwa wenye nguvu.
It is sown in dishonor; it is raised in glory. It is sown in weakness; it is raised in power.
44 Unapozikwa ni mwili wa kawaida, unapofufuliwa ni mwili wa kiroho. Kuna mwili wa kawaida na kutakuwa na mwili wa kiroho.
It is sown a natural body; it is raised a spiritual body. If there is a natural body, there is also a spiritual body.
45 Maana Maandiko yasema: “Mtu wa kwanza, Adamu, alikuwa kiumbe mwenye uhai;” lakini adamu wa mwisho ni Roho awapaye watu uzima.
So it is written: “The first man Adam became a living being;” the last Adam a life-giving spirit.
46 Lakini unaotangulia kuwako si ule mwili wa kiroho, ila ule mwili wa kawaida kisha ule mwili wa kiroho.
The spiritual, however, was not first, but the natural, and then the spiritual.
47 Adamu wa kwanza aliumbwa kwa udongo, alitoka ardhini; mtu wa pili alitoka mbinguni.
The first man was of the dust of the earth, the second man from heaven.
48 Wote walio wa dunia wako kama huyo mtu aliyeumbwa kwa udongo; wale walio wa mbinguni wako kama yule aliyetoka mbinguni.
As was the earthly man, so also are those who are of the earth; and as is the heavenly man, so also are those who are of heaven.
49 Kama vile tulivyofanana na yule aliyeumbwa kwa udongo, vivyo hivyo tutafanana na huyohuyo aliyetoka mbinguni.
And just as we have borne the likeness of the earthly man, so also shall we bear the likeness of the heavenly man.
50 Basi, ndugu, nasema hivi: kile kilichofanywa kwa mwili na damu hakiwezi kuushiriki Ufalme wa Mungu; na chenye kuharibika hakiwezi kuwa na hali ya kutoharibika.
Now I declare to you, brothers, that flesh and blood cannot inherit the kingdom of God, nor does the perishable inherit the imperishable.
51 Sikilizeni, nawaambieni siri: sisi hatutakufa sote, ila sote tutageuzwa
Listen, I tell you a mystery: We will not all sleep, but we will all be changed—
52 wakati wa mbiu ya mwisho, kwa nukta moja, kufumba na kufumbua. Maana mbiu itakapolia, wafu watafufuliwa katika hali ya kutoweza kufa tena, na sisi tutageuzwa.
in an instant, in the twinkling of an eye, at the last trumpet. For the trumpet will sound, the dead will be raised imperishable, and we will be changed.
53 Maana ni lazima kila kiharibikacho kijivalie hali ya kutoharibika, mwili uwezao kufa ujivalie hali ya kutokufa.
For the perishable must be clothed with the imperishable, and the mortal with immortality.
54 Basi, mwili huu wenye kuharibika utakapojivalia hali ya kutoharibika, na kile chenye kufa kitakapojivalia hali ya kutokufa, hapo ndipo litakapotimia lile neno lililoandikwa: “Kifo kimeangamizwa ushindi umekamilika!”
When the perishable has been clothed with the imperishable and the mortal with immortality, then the saying that is written will come to pass: “Death has been swallowed up in victory.”
55 “Kifo, ushindi wako uko wapi? Uwezo wako wa kuumiza uko wapi?” (Hadēs g86)
“Where, O Death, is your victory? Where, O Death, is your sting?” (Hadēs g86)
56 Ukali wa kifo hutokana na dhambi, nayo dhambi hupata nguvu yake katika Sheria.
The sting of death is sin, and the power of sin is the law.
57 Lakini tumshukuru Mungu anayetupatia ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
But thanks be to God, who gives us the victory through our Lord Jesus Christ!
58 Basi, ndugu zangu wapenzi, simameni imara na thabiti. Endeleeni daima kuwa na bidii katika kazi ya Bwana, mkijua kwamba kazi mnayofanya katika utumishi wa Bwana haitapotea bure.
Therefore, my beloved brothers, be steadfast and immovable. Always excel in the work of the Lord, because you know that your labor in the Lord is not in vain.

< 1 Wakorintho 15 >