< 1 Wakorintho 15 >
1 Sasa ndugu, napenda kuwakumbusha ile Habari Njema niliyowahubirieni nanyi mkaipokea na kusimama imara ndani yake.
Men jeg kundgør eder, Brødre, det Evangelium, som jeg forkyndte eder, hvilket I ogsaa modtoge, i hvilket I ogsaa staa,
2 Kwa njia yake mnaokolewa, ikiwa mnayazingatia maneno niliyowahubirieni, na kama kuamini kwenu hakukuwa bure.
ved hvilket I ogsaa frelses, hvis I fastholde, med hvilket Ord jeg forkyndte eder det — ellers troede I forgæves.
3 Mimi niliwakabidhi ninyi mambo muhimu sana ambayo mimi niliyapokea: kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na Maandiko Matakatifu;
Jeg overleverede eder nemlig som noget af det første, hvad jeg ogsaa har modtaget: at Kristus døde for vore Synder, efter Skrifterne;
4 kwamba alizikwa, akafufuka siku ya tatu kama ilivyoandikwa;
og at han blev begravet; og at han er bleven oprejst den tredje Dag, efter Skrifterne;
5 kwamba alimtokea Kefa, na baadaye aliwatokea wale kumi na wawili.
og at han blev set af Kefas, derefter af de tolv;
6 Kisha aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano kwa mara moja; wengi wao wanaishi bado, lakini baadhi yao wamekwisha kufa.
derefter blev han set af over fem Hundrede Brødre paa een Gang, af hvilke de fleste endnu ere i Live, men nogle ere hensovede;
7 Baadaye alimtokea Yakobo kisha akawatokea mitume wote.
derefter blev han set af Jakob, dernæst af alle Apostlene;
8 Baada ya wote, akanitokea hata mimi, mimi niliyekuwa kama mtu aliyezaliwa kabla ya wakati.
men sidst af alle blev han set ogsaa af mig som det ufuldbaarne Foster;
9 Maana mimi ni mdogo kabisa miongoni mwa mitume na wala sistahili kuitwa mtume, kwa sababu nililidhulumu kanisa la Mungu.
thi jeg er den ringeste af Apostlene, jeg, som ikke er værd at kaldes Apostel, fordi jeg har forfulgt Guds Menighed.
10 Lakini, kwa neema yake Mungu, nimekuwa kama nilivyo. Na neema yake kwangu haikuwa bure. Mimi nimefanya kazi kuliko wote; si mimi hasa, ila ni neema ya Mungu ifanyayo kazi pamoja nami.
Men af Guds Naade er jeg det, jeg er, og hans Naade imod mig har ikke været forgæves; men jeg har arbejdet mere end de alle, dog ikke jeg, men Guds Naade, som er med mig.
11 Lakini hata hivyo, iwe wao ndio wahubirio au mimi nihubiriye, haidhuru, hiki ndicho tunachuhubiri, na hiki ndicho mnachoamini.
Hvad enten det da er mig eller de andre, saaledes prædike vi, og saaledes troede I.
12 Sasa, maadam inahubiriwa kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, baadhi yenu wanawezaje kusema kwamba hakuna ufufuo wa wafu?
Men naar der prædikes, at Kristus er oprejst fra de døde, hvorledes sige da nogle iblandt eder, at der ikke er dødes Opstandelse?
13 Kama hakuna ufufuo wa wafu, basi, Kristo naye hakufufuka;
Dersom der ikke er dødes Opstandelse, da er ikke heller Kristus oprejst.
14 na kama Kristo hakufufuka, basi mahubiri yetu hayana maana na imani yenu haina maana.
Men er Kristus ikke oprejst, da er vor Prædiken jo tom, og eders Tro ogsaa tom.
15 Zaidi ya hayo sisi tungekuwa mashahidi wa uongo mbele ya Mungu, maana tulisema kwamba Mungu alimfufua Kristo kutoka wafu na kumbe yeye hakumfufua—kama ni kweli kwamba wafu hawafufuliwi.
Men vi blive da ogsaa fundne som falske Vidner om Gud, fordi vi have vidnet imod Gud, at han oprejste Kristus, hvem han ikke har oprejst, saafremt døde virkelig ikke oprejses.
16 Maana, ikiwa ni kweli kwamba wafu hawafufuki, basi naye Kristo hakufufuka.
Thi dersom døde ikke oprejses, da er Kristus ikke heller oprejst.
17 Na kama Kristo hakufufuliwa, basi, imani yenu ni ya bure; mngali bado katika dhambi zenu.
Men dersom Kristus ikke er oprejst, da er eders Tro forgæves; saa ere I endnu i eders Synder;
18 Zaidi ya hayo, wale wote waliokufa wakiwa wameungana na Kristo wamepotea kabisa.
da gik altsaa ogsaa de, som ere hensovede i Kristus, fortabt.
19 Kama matumaini yetu katika Kristo yanahusu tu maisha haya ya sasa, basi, sisi ni watu wa kusikitikiwa zaidi kuliko wengine wote duniani.
Have vi alene i dette Liv sat vort Haab til Kristus, da ere vi de ynkværdigste af alle Mennesker.
20 Lakini ukweli ni kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, limbuko lao wale waliolala katika kifo.
Men nu er Kristus oprejst fra de døde, som Førstegrøde af de hensovede.
21 Maana kama vile kifo kilivyoletwa duniani na mtu mmoja, vivyo hivyo nako kufufuka kutoka wafu kumesababishwa na mtu mmoja.
Thi efterdi Død kom ved et Menneske, er ogsaa dødes Opstandelse kommen ved et Menneske.
22 Kama vile watu wote wanavyokufa kwa kujiunga na Adamu, vivyo hivyo wote watafufuliwa kwa kuungana na Kristo.
Thi ligesom alle dø i Adam, saaledes skulle ogsaa alle levendegøres i Kristus.
23 Lakini kila mmoja kwa mpango wake: Kristo kwanza, halafu wale walio wake Kristo wakati Kristo atakapokuja.
Dog hver i sit Hold: som Førstegrøde Kristus, dernæst de, som tilhøre Kristus, ved hans Tilkommelse.
24 Baada ya hayo, mwisho utafika wakati ambapo Kristo atamkabidhi Mungu Baba Utawala, baada ya kufutilia mbali kila tawala na mamlaka na nguvu.
Derpaa kommer Enden, naar han overgiver Gud og Faderen Riget, naar han har tilintetgjort hver Magt og hver Myndighed og Kraft.
25 Maana Kristo sharti atawale mpaka Mungu atakapowashinda adui zake na kuwaweka chini ya miguu yake.
Thi han bør være Konge, indtil han faar lagt alle Fjenderne under sine Fødder.
26 Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni kifo.
Den sidste Fjende, som tilintetgøres, er Døden.
27 Maana, Maandiko yasema: “Mungu ameweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Lakini, Maandiko yanaposema: “Vitu vyote vimewekwa chini ya miguu yake avitawale” ni dhahiri kwamba Mungu haingii katika kundi hilo la vitu, maana yeye ndiye anayeviweka vitu hivyo chini ya Kristo.
Han har jo „lagt alle Ting under hans Fødder”. Men naar han siger: „Alt er underlagt” — aabenbart med Undtagelse af den, som underlagde ham alt —
28 Lakini vitu vyote vitakapowekwa chini ya Utawala wa Kristo, ndipo naye Mwana atakapojiweka chini ya Mungu, aliyeweka vyote chini ya Utawala wake; ili Mungu atawale juu ya vyote.
naar da alle Ting ere blevne ham underlagte, da skal ogsaa Sønnen selv underlægge sig ham, som har underlagt ham alle Ting, for at Gud kan være alt i alle.
29 Kama hakuna ufufuo, je watu wale wanaobatizwa kwa ajili ya wafu wanatumainia kupata nini? Kama wafu hawafufuliwi, ya nini kubatizwa kwa ajili yao?
Hvad ville ellers de udrette, som lade sig døbe for de døde? Dersom døde overhovedet ikke oprejses, hvorfor lade de sig da døbe for dem?
30 Na sisi, ya nini kujitia hatarini kila saa?
Hvorfor udsætte da ogsaa vi os hver Time for Fare?
31 Ndugu, mimi nakikabili kifo kila siku! Fahari niliyo nayo juu yenu katika kuungana na Kristo Yesu Bwana wetu inanifanya nitangaze jambo hili.
Jeg dør daglig, saa sandt jeg har eder, Brødre, at rose mig af i Kristus Jesus, vor Herre.
32 Kama kusudi langu lingalikuwa la kibinadamu tu, kule kupigana kwangu na wanyama wakali hapa Efeso kungalinifaa kitu gani? Kama wafu hawafufuki, basi, “Tule na tunywe, maana kesho tutakufa.”
Hvis jeg som et almindeligt Menneske har kæmpet med vilde Dyr i Efesus, hvad Gavn har jeg saa deraf? Dersom døde ikke oprejses, da „lader os spise og drikke, thi i Morgen dø vi.”
33 Msidanganyike! Urafiki mbaya huharibu tabia njema.
Farer ikke vild; slet Omgang fordærver gode Sæder!
34 Amkeni! Anzeni kuishi vema, na acheni kutenda dhambi. Baadhi yenu hawamjui Mungu kabisa. Hii nawaambieni, ni aibu kubwa kwenu!
Vorder ædrue, som det bør sig, og synder ikke; thi nogle kende ikke Gud; til Skam for eder siger jeg det.
35 Lakini mtu anaweza kuuliza: “Wafu watafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani wakati watakapokuja tena?”
Men man vil sige: „Hvorledes oprejses de døde? hvad Slags Legeme komme de med?”
36 Hayo ni maswali ya kijinga! Ukipanda mbegu, isipokufa kwanza haitaota.
Du Daare! det, som du saar, bliver ikke levendegjort, dersom det ikke dør.
37 Unachopanda ni mbegu tu, labda ya ngano au nafaka nyingine, na si mmea mzima ambao hutokea baadaye.
Og hvad du end saar, da saar du ikke det Legeme, der skal vorde, men et nøgent Korn, være sig af Hvede eller af anden Art.
38 Mungu huipa hiyo mbegu mwili anaoutaka mwenyewe; kila mbegu hupata mwili wake wa pekee.
Men Gud giver det et Legeme, saaledes som han har villet, og hver Sædart sit eget Legeme.
39 Miili ya viumbe vyote si sawa. Miili ya binadamu ni ya namna moja, ya wanyama ni ya namna nyingine, ya ndege ni ya namna nyingine na miili ya samaki pia ni ya namna nyingine.
Ikke alt Kød er det samme Kød, men eet er Menneskers, et andet Kvægs Kød, et andet Fugles Kød, et andet Fiskes.
40 Iko miili ya mbinguni na miili ya duniani; uzuri wa miili ya mbinguni ni mwingine, na na uzuri wa miili ya duniani ni mwingine.
Og der er himmelske Legemer og jordiske Legemer; men een er de himmelskes Herlighed, en anden de jordiskes.
41 Uko uzuri wa jua, wa mwezi na wa nyota; hata nyota nazo huhitilafiana kwa uzuri.
Een er Solens Glans og en anden Maanens Glans og en anden Stjernernes Glans; thi den ene Stjerne er forskellig fra den anden i Glans.
42 Ndivyo ilivyo kuhusu ufufuo wa wafu. Kama vile mbegu, mwili huzikwa ardhini ukiwa katika hali ya kuharibika, lakini hufufuliwa katika hali ya kutoharibika.
Saaledes er det ogsaa med de dødes Opstandelse: det saaes i Forkrænkelighed, det oprejses i Uforkrænkelighed;
43 Huzikwa katika hali duni, hufufuliwa katika hali tukufu; huzikwa katika hali dhaifu, hufufuliwa ukiwa wenye nguvu.
det saaes i Vanære, det oprejses i Herlighed; det saaes i Skrøbelighed, det oprejses i Kraft;
44 Unapozikwa ni mwili wa kawaida, unapofufuliwa ni mwili wa kiroho. Kuna mwili wa kawaida na kutakuwa na mwili wa kiroho.
der saaes et sjæleligt Legeme, der oprejses et aandeligt Legeme. Naar der gives et sjæleligt Legeme, gives der ogsaa et aandeligt.
45 Maana Maandiko yasema: “Mtu wa kwanza, Adamu, alikuwa kiumbe mwenye uhai;” lakini adamu wa mwisho ni Roho awapaye watu uzima.
Saaledes er der ogsaa skrevet: „Det første Menneske, Adam, blev til en levende Sjæl;” den sidste Adam blev til en levendegørende Aand.
46 Lakini unaotangulia kuwako si ule mwili wa kiroho, ila ule mwili wa kawaida kisha ule mwili wa kiroho.
Men det aandelige er ikke det første, men det sjælelige; derefter det aandelige.
47 Adamu wa kwanza aliumbwa kwa udongo, alitoka ardhini; mtu wa pili alitoka mbinguni.
Det første Menneske var af Jord, jordisk; det andet Menneske er fra Himmelen.
48 Wote walio wa dunia wako kama huyo mtu aliyeumbwa kwa udongo; wale walio wa mbinguni wako kama yule aliyetoka mbinguni.
Saadan som den jordiske var, saadanne ere ogsaa de jordiske; og saadan som den himmelske er, saadanne ere ogsaa de himmelske.
49 Kama vile tulivyofanana na yule aliyeumbwa kwa udongo, vivyo hivyo tutafanana na huyohuyo aliyetoka mbinguni.
Og ligesom vi have baaret den jordiskes Billede, saaledes skulle vi ogsaa bære den himmelskes Billede!
50 Basi, ndugu, nasema hivi: kile kilichofanywa kwa mwili na damu hakiwezi kuushiriki Ufalme wa Mungu; na chenye kuharibika hakiwezi kuwa na hali ya kutoharibika.
Men dette siger jeg, Brødre! at Kød og Blod kan ikke arve Guds Rige, ej heller arver Forkrænkeligheden Uforkrænkeligheden.
51 Sikilizeni, nawaambieni siri: sisi hatutakufa sote, ila sote tutageuzwa
Se, jeg siger eder en Hemmelighed: Alle skulle vi ikke hensove, men vi skulle alle forvandles,
52 wakati wa mbiu ya mwisho, kwa nukta moja, kufumba na kufumbua. Maana mbiu itakapolia, wafu watafufuliwa katika hali ya kutoweza kufa tena, na sisi tutageuzwa.
i et Nu, i et Øjeblik, ved den sidste Basun; thi Basunen skal lyde, og de døde skulle oprejses uforkrænkelige, og vi skulle forvandles.
53 Maana ni lazima kila kiharibikacho kijivalie hali ya kutoharibika, mwili uwezao kufa ujivalie hali ya kutokufa.
Thi dette forkrænkelige maa iføre sig Uforkrænkelighed, og dette dødelige iføre sig Udødelighed.
54 Basi, mwili huu wenye kuharibika utakapojivalia hali ya kutoharibika, na kile chenye kufa kitakapojivalia hali ya kutokufa, hapo ndipo litakapotimia lile neno lililoandikwa: “Kifo kimeangamizwa ushindi umekamilika!”
Men naar dette forkrænkelige har iført sig Uforkrænkelighed, og dette dødelige har iført sig Udødelighed, da skal det Ord opfyldes, som er skrevet: „Døden er opslugt til Sejr.”
55 “Kifo, ushindi wako uko wapi? Uwezo wako wa kuumiza uko wapi?” (Hadēs )
„Død, hvor er din Sejr? Død, hvor er din Brod?” (Hadēs )
56 Ukali wa kifo hutokana na dhambi, nayo dhambi hupata nguvu yake katika Sheria.
Men Dødens Brod er Synden, og Syndens Kraft er Loven.
57 Lakini tumshukuru Mungu anayetupatia ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
Men Gud ske Tak, som giver os Sejren ved vor Herre Jesus Kristus!
58 Basi, ndugu zangu wapenzi, simameni imara na thabiti. Endeleeni daima kuwa na bidii katika kazi ya Bwana, mkijua kwamba kazi mnayofanya katika utumishi wa Bwana haitapotea bure.
Derfor, mine elskede Brødre! bliver faste, urokkelige, altid rige i Herrens Gerning, vidende, at eders Arbejde er ikke forgæves i Herren.