< 1 Wakorintho 10 >
1 Ndugu, nataka mjue kwamba babu zetu wote walikuwa chini ya ulinzi wa lile wingu, na kwamba wote walivuka salama ile bahari.
And I do not wish you to be ignorant, brothers, that all our fathers were under the cloud, and all passed through the sea,
2 Wote walibatizwa katika umoja na Mose kwa lile wingu na ile bahari.
and all were immersed into Moses in the cloud, and in the sea;
3 Wote walikula chakula kilekile cha kiroho,
and all ate the same spiritual food,
4 wakanywa pia kinywaji kilekile cha kiroho, maana walikunywa kutoka ule mwamba wa kiroho uliowafuata; mwamba huo ulikuwa Kristo mwenyewe.
and all drank the same spiritual drink, for they were drinking of a spiritual rock following them, and the rock was the Christ;
5 Hata hivyo, wengi wao hawakumpendeza Mungu, na maiti zao zilisambazwa jangwani.
but in the most of them God was not well pleased, for they were strewn in the wilderness,
6 Sasa, mambo hayo yote ni mfano tu kwetu; yanatuonya sisi tusitamani ubaya kama wao walivyotamani.
and those things became types of us, for our not passionately desiring evil things, as also these desired.
7 Msiwe waabudu sanamu kama baadhi yao walivyokuwa; kama yasemavyo Maandiko: “Watu waliketi kula na kunywa, wakasimama kucheza.”
Neither become idolaters, as certain of them, as it has been written: “The people sat down to eat and to drink, and stood up to play”;
8 Wala tusizini kama baadhi yao walivyozini, wakaangamia siku moja watu ishirini na tatu elfu.
neither may we commit whoredom, as certain of them committed whoredom, and there fell in one day twenty-three thousand;
9 Tusimjaribu Bwana kama baadhi yao walivyomjaribu, wakauawa na nyoka.
neither may we tempt the Christ, as also certain of them tempted, and perished by the serpents;
10 Wala msinung'unike kama baadhi yao walivyonung'unika, wakaangamizwa na Mwangamizi!
neither murmur, as also some of them murmured, and perished by the destroyer.
11 Basi, mambo hayo yaliyowapata wao ni kielelezo kwa wengine, na yaliandikwa ili kutuonya sisi, ambao mwisho wa nyakati unatukabili. (aiōn )
And all these things happened to those persons as types, and they were written for our admonition, to whom the end of the ages came, (aiōn )
12 Anayedhani amesimama imara ajihadhari asianguke.
so that he who is thinking to stand—let him observe, lest he fall.
13 Majaribu mliyokwisha pata ni ya kawaida kwa binadamu. Mungu ni mwaminifu, naye hataruhusu mjaribiwe kupita nguvu zenu, ila pamoja na majaribu, yeye atawapeni pia nguvu ya kustahimili na njia ya kutoka humo salama.
No temptation has taken you—except that of man; and God is faithful, who will not permit you to be tempted above what you are able, but He will make, with the temptation, also the outlet, for your being able to bear [it].
14 Kwa hiyo, wapenzi wangu, epeni ibada za sanamu.
For this reason, my beloved, flee from the idolatry;
15 Naongea nanyi, watu wenye busara; jiamulieni wenyewe hayo nisemayo.
as to wise men I speak—judge what I say.
16 Tunapomshukuru Mungu kwa kikombe kile cha baraka, je, huwa hatushiriki damu ya Kristo? Na tunapoumega mkate, je, huwa hatushiriki mwili wa Kristo?
The cup of the blessing that we bless—is it not the fellowship of the blood of the Christ? The bread that we break—is it not the fellowship of the body of the Christ?
17 Kwa kuwa mkate huo ni mmoja, sisi, ingawa ni wengi, tu mwili mmoja; maana sote twashiriki mkate huohuo.
Because one bread, one body, are we the many—for we all partake of the one bread.
18 Chukueni, kwa mfano, Wayahudi wenyewe: kwao, wenye kula vilivyotambikiwa madhabahuni waliungana na hiyo madhabahu.
See Israel according to the flesh! Are those not eating the sacrifices in the fellowship of the altar?
19 Nataka kusema nini, basi? Kwamba chakula kilichotambikiwa sanamu ni kitu zaidi ya chakula? Na hizo sanamu, je, ni kitu kweli zaidi ya sanamu?
What do I say then? That an idol is anything? Or that a sacrifice offered to an idol is anything?
20 Hata kidogo! Ninachosema ni kwamba tambiko wanazotoa watu wasiomjua Mungu wanawatolea pepo, sio Mungu. Sipendi kamwe ninyi muwe na ushirika na pepo.
[No, ] but that the things that the nations sacrifice—they sacrifice to demons and not to God; and I do not wish you to come into the fellowship of the demons.
21 Hamwezi kunywa kikombe cha Bwana na kikombe cha pepo; hamwezi kushiriki katika meza ya Bwana na katika meza ya pepo.
You are not able to drink the cup of the LORD and the cup of demons; you are not able to partake of the table of the LORD and of the table of demons;
22 Au je, tunataka kumfanya Bwana awe na wivu? Mnadhani tuna nguvu zaidi kuliko yeye?
do we arouse the LORD to jealousy? Are we stronger than He?
23 Vitu vyote ni halali, lakini si vyote vinafaa. Vitu vyote ni halali lakini si vyote vinajenga.
All things are lawful to me, but not all things are profitable; all things are lawful to me, but not all things build up;
24 Mtu asitafute faida yake mwenyewe, ila faida ya mwenzake.
let no one seek his own—but each another’s.
25 Kuleni chochote kile kiuzwacho sokoni bila ya kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu;
Eat whatever is sold in the meat-market, not inquiring, because of the conscience,
26 maana Maandiko yasema: “Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana.”
for the earth and its fullness [are] the LORD’s;
27 Kama mtu ambaye si muumini akiwaalikeni nanyi mkakubali kwenda, basi, kuleni vyote atakavyowaandalieni bila kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu.
and if anyone of the unbelieving calls you, and you wish to go, eat all that is set before you, inquiring nothing, because of the conscience;
28 Lakini mtu akiwaambieni: “Chakula hiki kimetambikiwa sanamu,” basi, kwa ajili ya huyo aliyewaambieni hivyo na kwa ajili ya dhamiri, msile.
and if anyone may say to you, “This is a thing sacrificed to an idol,” do not eat, because of that one who showed [it], and of the conscience, for the LORD’s [is] the earth and its fullness:
29 Nasema, “kwa ajili ya dhamiri,” si dhamiri yenu, bali dhamiri yake huyo aliyewaambieni. Mtaniuliza: “Kwa nini uhuru wangu utegemee dhamiri ya mtu mwingine?
and conscience, I say, not of yourself, but of the other, for why [is it] that my liberty is judged by another’s conscience?
30 Ikiwa mimi nashiriki chakula hicho huku namshukuru Mungu, kwa nini nilaumiwe kwa chakula ambacho kwa ajili yake nimemshukuru Mungu?”
And if I partake thankfully, why am I spoken of [as] evil, for that for which I give thanks?
31 Basi, chochote mfanyacho iwe ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.
Whether, then, you eat, or drink, or do anything, do all to the glory of God;
32 Msiwe kikwazo kwa Wayahudi au kwa Wagiriki au kwa kanisa la Mungu.
become offenseless, both to Jews and Greeks, and to the Assembly of God;
33 Muwe kama mimi; najaribu kuwapendeza wote kwa kila njia, bila kutafuta faida yangu mwenyewe ila faida ya wote, wapate kuokolewa.
as I also please all in all things, not seeking my own profit, but that of many—that they may be saved.