< Sefania 1 >

1 Hili ni neno la Yahwe ambalo lilikuja kwa Sefania mwana wa Kushi mwana wa Gedalia mwana wa Amaria mwana Hezekia, katika siku za Yosia mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda. “
La parole de Yahweh qui fut adressée à Sophonie, fils de Chusi, fils de Godolias, fils d’Amarias, fils d’Ézéchias, dans les jours de Josias, fils d’Amon, roi de Juda.
2 Nitaangamiza kabisa kila kitu kutoka usoni mwa dunia - hili ni tamko la Bwana mwenyewe.
J’enlèverai tout de dessus la face de la terre, — oracle de Yahweh;
3 Nitamwangamiza mtu na mnyama; Nitawaangamiza ndege wa mbinguni na samaki wa baharini, uharibifu pamoja na waovu. Hivyo nitamfutilia mbali mtu kutoka uso wa dunia - hili ni tamko la Bwana mwenyewe.
j’enlèverai les hommes et les bêtes, j’enlèverai les oiseaux du ciel et les poissons de la mer, et les scandales avec les impies, et j’exterminerai l’homme de dessus la face de la terre, – oracle de Yahweh.
4 Nitafika kwa mkono wangu juu ya Yuda na wote wenyeji wa Yerusalemu. Nitafutilia mbali kila mabaki ya Baali kutoka sehemu hii na majina ya watu waabuduo sanamu miongoni mwa makuhani,
Et j’étendrai ma main sur Juda, et sur tous les habitants de Jérusalem, et j’exterminerai de ce lieu le reste de Baal, le nom de ses ministres en même temps que les prêtres;
5 watu ambao juu ya nyumba huabudu miili ya mbinguni, na watu ambao huabudu na kuapa kwa Yahwe bali ambao pia huapa kwa mfalme wao.
et ceux qui se prosternent sur les toits, devant l’armée des cieux; et ceux qui se prosternent en faisant serment à Yahweh, tout en jurant par leur roi;
6 Nitawafutilia mbali pia wale ambao wamegeuka nyuma kutoka kumfuata Yahwe, wale ambao pia humtafuta Yahwe pasipo kuuliza ulinzi wake.
et ceux qui se détournent de Yahweh, qui ne cherchent pas Yahweh, et ne se soucient pas de lui.
7 Uwe kimya mbele ya Bwana Yahwe! Kwa kuwa siku ya Yahwe ni karibu, Yahwe ameandaa dhabihu na amewatenga wageni wake.
Silence devant le Seigneur Yahweh! Car le jour de Yahweh est proche; car Yahweh a préparé un sacrifice, il a consacré ses invités.
8 “Itakuja katika siku ya dhabihu ya Bwana, hivyo nitawapiga wakuu na wana wa mfalme, na kila mmoja aliyevikwa mavazi ya kigeni.
Et il arrivera: Au jour du sacrifice de Yahweh, je châtierai les princes, et les fils de roi, et tous ceux qui revêtent des vêtements étrangers.
9 Katika siku hiyo nitawapiga wote wale ambao huruka juu ya kizingiti, wale ambao hujaza nyumba ya bwana wao kwa vurugu na udanganyifu.
Et je châtierai en ce jour-là tous ceux qui sautent par-dessus le seuil, qui remplissent de violence et de fraude la maison de leur maître.
10 Itakuwa katika siku ile - hili ni tangazo la Yahwe - kwamba kilio cha huzuni kitakuja kutoka kwenye mlango wa samaki, ikipiga yowe kutoka Wilaya ya Pili, na sauti ya kishindo kikuu kutoka vilimani.
Et il arrivera en ce jour-là, — oracle de Yahweh: De la porte des poissons retentiront des cris, de la seconde ville des gémissements, et des collines un grand fracas.
11 Pigeni yowe, wenyeji wa Soko la Wilaya, kwa wote wafanyabiashara watakuwa wameharibiwa, wote wale ambao hupima fedha watakuwa wamefutiliwa mbali.
Gémissez, habitants du Mortier, car tout le peuple chananéen est anéanti, tous ceux qui sont chargés d’argent sont exterminés.
12 Itakuwa katika siku ile nitaitafuta Yerusalemu kwa taa na kuwapiga wanaume ambao watakuwa wamekaa kwenye mvinyo wao na kusema mioyoni mwao, 'Yahwe hatafanya chochote, ama kizuri au kiovu.'.
Et il arrivera en ce temps-là: Je fouillerai Jérusalem avec des lanternes, et je châtierai les hommes figés sur leur lie, qui disent en leur cœur: « Yahweh ne fait ni bien ni mal! »
13 Mali zao zitakuja kuporwa, na nyumba zao zitakuwa zimetelekezwa kwa maangamizi! Watajenga nyumba lakini hawataishi humo, na kupanda mizabibu lakini hawatakunywa mvinyo wake.
Leurs biens seront livrés au pillage, et leurs maisons à la dévastation; ils bâtiront des maisons, et ils n’y habiteront point; ils planteront des vignes, et ils n’en boiront pas le vin.
14 Siku kubwa ya Yahwe ni karibu, karibu na inaharakisha upesi! Sauti ya siku ya Yahwe itakuwa ya kilio cha uchungu wa kishujaa!
Il est proche le grand jour de Yahweh, il est proche, il vient en toute hâte! On l’entend venir, le jour de Yahweh! L’homme brave y poussera des cris amers.
15 Siku hiyo itakuwa siku ya ghadabu, siku ya huzuni na uchungu, siku ya dhoruba na maangamizi, siku ya giza na utusitusi, siku ya mawingu na giza nene.
C’est un jour de fureur que ce jour-là, un jour d’angoisse et d’affliction, un jour de désolation et de ruine, un jour de ténèbres et d’obscurité, un jour de nuages et d’épais brouillards,
16 Itakuwa siku ya parapanda na kengele dhidi ya ngome mijini na buruji ndefu.
un jour de trompette et d’alarme, sur les villes fortes et les créneaux élevés.
17 Hivyo nitaleta dhiki juu ya wanadamu, kwa hiyo watatembea karibu kama wanaume vipofu tangu walipofanya dhambi dhidi ya Yahwe. Damu yao itamwagwa kama vumbi, na sehemu zao za ndani kama kinyesi.
Je mettrai les hommes dans la détresse, et ils marcheront comme des aveugles, parce qu’ils ont péché contre Yahweh; leur sang sera répandu comme la poussière; et leur chair comme du fumier.
18 Wala fedha zao wala dhahabu zao hazitaweza kuwaokoa juu ya ghadhabu ya Yahwe. Ndani ya moto wa wivu wake dunia yote itateketezwa, hivyo ataleta ukamilifu, miwisho wa kutisha kwa wote wakaao duniani.”
Ni leur argent, ni leur or ne pourront les délivrer; au jour de la fureur de Yahweh; par le feu de sa jalousie, toute la terre sera dévorée; car il fera une destruction totale, une ruine soudaine, de tous les habitants de la terre.

< Sefania 1 >